Jana nimekula kitimoto bila kujua!

Jana nimekula kitimoto bila kujua!

Kwa waislam wengi wasiojua dini dhambi kuu na alama Yao ya dini ni kutokula nyama ya nguruwe.

Lakini mtu Huyo utakuta anakunywa pombe, anazini, anatembea mpaka na mashoga, anaua, anaita wengine makafiri nk.

Hivi kweli kwenu ni Kula kitimoto tu?

Nakumbuka mafundisho ya dini yanaruhusu Kula kitimoto Katika mazingira ya aina mbili. Either Uko sehemu ambapo Hakuna chakula kabisa na usipopata chakula Unaweza kufa,
Au ule kitimoto bila kujua km ni kitimoto!
Kwanini mbio mbio umekimbilia kujenga hoja kuhusu Imani, kwabi mtoa hoja amekuambia yeye ni Muislamu? Unavoamini wewe wakristo wote wanatumia hiyo kiumbe kwa kitoweo..?? Je, wakristo hakuna waasi kwa mujibu wa Imani yao? Kwanini uhoji uhalali wa maasi ktk dini fulani kwa kuhesabu matendo ya baadhi ya watu??

ACHA CHUKI DHIDI YA IMANI ZINGINE, WATANZANIA TUNA UNDUGU WA DAMU NJE YA IMANI ZETU, UBAGUZI WOWOTE WA KIIMANI UNAWEZA KUHATARISHA USTAWI WA JAMII ZETU..!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikaribishwa na rafiki yangu kwenye sherehe ya miaka10 ya ndoa.
Mwandazi hakujua km situmii na mwenyeji wangu alitoka
Kwa vile ilkuwa usiku nikala.
NB.Najihisi kichefuchefu kula haram.
Ni ushahidi kuwa kuumwa kuko akilini mwako!
Usingeambiwa ungekuwa freshi ile bomba, na kutamani more.
 
Acha unafiki mleta mada,kwani kitimoto kitu gani?
Watu mnakula 0713 a.k.a jicho nahamuoni haramu.
Acha hizo mazee!!
 
Rafiki yangu mmoja job tulikiwa tukitoka kwenda lunch nnaagiza nusu na ugali ye anakula samaki nkashangaa siku ya kwanza kaanza kudowea rojo la kitimoto rost, siku nyingine akabeba nyama, baada ya hapo ye ndio anajua machimbo yote ya kitimoto,i nilimwambia uzinzi unafanya, pombe na starehe sana ila nguruwe kwako ndio haramu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom