JamiiTalks JamiiForums yatoa mafunzo kwa bloggers wa Tanzania kuhusu ubora wa maudhui na Sheria zihusuzo kazi zao

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
Mnamo tarehe 19 Oktoba 2018, JamiiForums ilifanya mafunzo mahususi kwa ajili ya bloggers wa Tanzania. Mafunzo hayo yalijikita katika kuwapa uwezo bloggers wa kufanya kazi zao za kuhabarisha, kuburudisha na kufundisha jamii.

0N4A0996.jpg

Mafunzo yalifanyika katika hoteli ya New Africa iliyopo Posta jijini Dar es Salaam kwa siku nzima na yalihusisha bloggers 21 kutoka nyanja mbalimbali kama habari za kitaifa, siasa, mitindo, michezo na burudani.

Mkufunzi ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa JamiiForums, Bwana Maxence Melo alifundisha kuhusu mambo mbalimbali kuanzia jinsi ya kuchagua jina kwa ajili ya blog au tovuti yako, kupata hakimiliki na jinsi ya kuwekea blog yako ulinzi.

0N4A1054.jpg

Pia kulikuwa na mjadala kuhusu ubora wa maudhui(content quality) na jinsi ya kutengeneza maudhui yanayoridhisha. Hapa bloggers walipewa mbinu za kuwawezesha kuwa na maudhui anuai na yaliyoshiba kwa ajili ya watumiaji wa mtandao ili kupata wasomaji wengi zaidi.

Miongoni kwa bloggers waliohudhuria, wapo pia waliositisha kazi zao kutokana na Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni kuwabana kwa kushindwa kulipa kiasi kilichowekwa ili kuendelea na shughuli mtandaoni.

0N4A1037.jpg

Katika kulizungumzia hili, Maxence aliwaambia licha ya kushindwa kufanya kazi kutokana na kukosa pesa lakini kama bloggers kwa ujumla wao ni muhimu kuangalia mbali zaidi katika athari za kanuni hata pale watakapolipia leseni.

Katika kufunga mafunzo haya, Maxence aliwaachia bloggers Kazi ya kuhakikisha wanawalisha watanzania maudhui yaliyo bora na yenye lengo la kukuza nchi kiuchumi, kiutamaduni na kujenga jamii bora.

Pia aliwaasa kutokata tamaa na kuendelea kupambana hata katika nyakati ngumu ili kutimiza ndoto zao.
 
Tanzania tuko nyuma kwenye quality video blogging; content haziridhishi. Most of youtube channels za Tanzania ni video tu Wema Sepetu kasema hiki, Makonda kasema yeye ndo Dar Sweetheart etc. Dunia inapokwenda hivi sasa video ndo kila kitu. I hope mlizungumzia hili pia
 
Hawa bloggers na vLoggers waendelee kupewa elimu tena sana hadi waelewe wanachokifanya. Wanakuletea habari ya rais Magufuli ataja umuhimu wa Stiegler's Gorge. Halafu wanakuambia bonyeza hapa, ukibonyeza wanasema bonyeza tena. Ukibonyeza unakutana na mambo ya Konki Konki Konki Master yaani ndindi imooo.

Hii inafanya mtu asitembelee kiblog chake wala channel yako tena na anazifutilia mbali. Hivyo ni muhimu kuelewa jamii unayoihudumia inataka nini. Kwa habari zaidi, BONYEZA HAPA
 
Unasoma kichwa, "hawa ndio waliomteka Mo"....ukiingia ndani unakuta mambo tofauti kabisa.

Kazi kutumalizia MB tu....hata MiladAyo kuna wakati alikuwa upuuzi sana anaweka video ya habari halafu dakika nzima ya kwanza ni tangazo...

Bora siku hizi kujirekebisha.
 
Na kuna kunguru walamba viatu bado wanamchukia MELO japo wanatumia JF kuandika upupu wao
 
Pascal Mayalla: Sababu ya JamiiForums kuwa kimbilio la wengi kuhusu habari mchanganyiko za uhakika za Tanzania na kimataifa.



Source: JamiiForums
 
Pamoja na yote bado kuna umuhimu mkubwa nyanja ya uandishi kupitia hizi social media as blog kuangalia aina ya uandishi kwa mtazamo unao mgusa msomaji badala ya baadhi ya wenye blog kuandika wanayopenda wao.

NAWASILISHA.
 
Pamoja na yote bado kuna umuhimu mkubwa nyanja ya uandishi kupitia hizi social media as blog kuangalia aina ya uandishi kwa mtazamo unao mgusa msomaji badala ya baadhi ya wenye blog kuandika wanayopenda wao.

NAWASILISHA.
Mkuu kwa mtazamo wangu Blogging haiwezi kuwa na mtindo mmoja wa kiundishi kwasababu anayeweka maudhui ndio mmliki wa wazo

Labda wapewe mafunzo ya kujua aina bora za uwasilishaji wa taarifa hata kama ni zao binafsi
 
SOMA UNIELEWE MKUU.
Mkuu kwa mtazamo wangu Blogging haiwezi kuwa na mtindo mmoja wa kiundishi kwasababu anayeweka maudhui ndio mmliki wa wazo

Labda wapewe mafunzo ya kujua aina bora za uwasilishaji wa taarifa hata kama ni zao binafsi
 
Mnamo tarehe 19 Oktoba 2018, JamiiForums ilifanya mafunzo mahususi kwa ajili ya bloggers wa Tanzania. Mafunzo hayo yalijikita katika kuwapa uwezo bloggers wa kufanya kazi zao za kuhabarisha, kuburudisha na kufundisha jamii.


Mafunzo yalifanyika katika hoteli ya New Africa iliyopo Posta jijini Dar es Salaam kwa siku nzima na yalihusisha bloggers 21 kutoka nyanja mbalimbali kama habari za kitaifa, siasa, mitindo, michezo na burudani.

Mkufunzi ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa JamiiForums, Bwana Maxence Melo alifundisha kuhusu mambo mbalimbali kuanzia jinsi ya kuchagua jina kwa ajili ya blog au tovuti yako, kupata hakimiliki na jinsi ya kuwekea blog yako ulinzi.


Pia kulikuwa na mjadala kuhusu ubora wa maudhui(content quality) na jinsi ya kutengeneza maudhui yanayoridhisha. Hapa bloggers walipewa mbinu za kuwawezesha kuwa na maudhui anuai na yaliyoshiba kwa ajili ya watumiaji wa mtandao ili kupata wasomaji wengi zaidi.

Miongoni kwa bloggers waliohudhuria, wapo pia waliositisha kazi zao kutokana na Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni kuwabana kwa kushindwa kulipa kiasi kilichowekwa ili kuendelea na shughuli mtandaoni.


Katika kulizungumzia hili, Maxence aliwaambia licha ya kushindwa kufanya kazi kutokana na kukosa pesa lakini kama bloggers kwa ujumla wao ni muhimu kuangalia mbali zaidi katika athari za kanuni hata pale watakapolipia leseni.

Katika kufunga mafunzo haya, Maxence aliwaachia bloggers Kazi ya kuhakikisha wanawalisha watanzania maudhui yaliyo bora na yenye lengo la kukuza nchi kiuchumi, kiutamaduni na kujenga jamii bora.

Pia aliwaasa kutokata tamaa na kuendelea kupambana hata katika nyakati ngumu ili kutimiza ndoto zao.
Le baharia alikuwepo?
 
Tanzania tuko nyuma kwenye quality video blogging; content haziridhishi. Most of youtube channels za Tanzania ni video tu Wema Sepetu kasema hiki, Makonda kasema yeye ndo Dar Sweetheart etc. Dunia inapokwenda hivi sasa video ndo kila kitu. I hope mlizungumzia hili pia
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom