JamiiForums Members Vs. TWAWEZA Tutafute Ukweli

JamiiForums Members Vs. TWAWEZA Tutafute Ukweli

Uchaguzi Wa Urais Ukiitishwa Leo Nani atashinda?


  • Total voters
    273
  • Poll closed .
MIMI sio Mungu ila na amini katika kuishi kwngu ipo siku nitshuhudia mzlendo wa kweli mwenye specie kama ya Dr Slaa anaongoza nchi hii ilio jaa udhalimu kwa sasa.
 
Kuna watu wana ID zaidi ya 8, sasa hapo unategemea kura sitakuwa fair......Utafiti wa TWAWEZA ndiyo wenyewe
 
Jf kuna watu wa aina fulani hivi i can say educated ,informed and elites wakati Tanzania ina % kubwa ya wajinga etc so statistics za humu i dare to say ni very wrong to pick(underestimated) na wala zisimvimbishe kichwa mtu !!simlazimishi mtu kuamini my instincts but kutokuamini pia (underestimation)ndo moja ya ticket au mtaji wa hao wanaoshinda uchaguzi wakati watu wa humu hawawapendi -its a challenge
 
Ikiwa ni mwaka kamili hadi pale tutakapompata rais mpya, tassisi ya TWAWEZA ilitoa ripoti ambayo wengi hawakukuliana nayo. Nasi kama raia ambao wanapenda ukweli, sinabudi kuanzisha huu uzi kuangalia ukweli kwamba uchaguzi ukiitishwa leo kati ya Dr. Slaa, Edward Lowassa, Mizengo Pinda na Samwel Sitta nani atashinda?

Tafadhalini kila mwanajukwaa aliyesajiliwa apige Kura tujue mbivu na mbichi wa TWAWEZA

Dr. Slaa
 
Kama wahusika wenyewe hawakubariani na tu tafiti na sisi tutakubari vp???utafiti c sahihi soma hiii chanzo gazeti la nipashe leo 17November 14

NIPASHE
Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa
Kimataifa Bernard Membe ameishukia Taasis
ya Utafiti wa Twaweza kuwa haina uwezo wa
kufanya tafiti za kisayansi.
Twaweza jumatano iliyopita ilitoa utafiti
pamoja na mambo mengine ikionyesha baadhi
ya majina ya wagombea urais
wanavyokubalika na wannachi ikiwa uchaguzi
ungefanyika September mwaka huu.
Katika orodha hiyo Membe alishika nafasi ya
tano huku akitanguliwa na Waziri mkuu wa
zamani Edward Lowassa aliyeongoza kwa
kupata asilimia13.
Membe alisema tafiti zimefanyika mapema
kabla ya wakati kufika na bila kuzngatia
misingi kanuni na sera za kiutafiti na kwamba
zinaweza kuichonganisha nchi nzima na dunia.
Alisema kila kipindi cha uchaguzi kote duniani
unapokaribia kunakua na utafiti ambao hutoa
muelekeo wa nchi hususani na uchaguzi
huo,hivyo ni jambo jema.
 
Haya nayo ni maneno mmmmmh

Chanzo mwananchi gazeti la leo 17 November 14

MWANANCHI
Waziri wa Maji Professa Jumanne Maghembe
ameshangazwa na utitiri wa watu wanaotaka
kugombea urais kwenye uchaguzi mkuu 2015
akisema nafasi hiyo ya juu nchini haifanani na
mashindano ya urembo ambayo mtu yoyote
anaweza kujaribu.
Alisema watu hao wanaojitokeza kugombea
urais hawaelezi wanataka kulifanyia nini Taifa
na akashauri wasioweza kueleza hoja zao
wasichaguliwe kushika nafasi hiyo.
“Urais unahitaji kuwa na sifa,dira na ajenda
kwa Taifa,lazima mtu anayetaka kuwa rais
atueleze uchumi utakua vipi,naona watu
wengi wametangaza nia,ni wazo zuri lakini
wajitathmini kwanza”alisema Maghembe
Hata hivyo Maghembe alipuuza mjadala wa
umri wa mgombea akisema kwamba hauna
msingi na kwamba sifa kuu ya mgombea urais
ni ajenda ya kuliletea Taifa maendeleo
endelevu.
Alisema kwa kipindi hiki ni lazima mtu
anayetaka urais awaeleze Watanzania
atawezaje kuivusha nchi katika uchumi wa
kati,vnginevyo hafai kushika wadhifa huo.
 
Dr Slaa hudanganywa na multiple id za bavicha hapa jf! Kamwe hawezi kushinda kwenye sanduku...
 
Ikiwa ni mwaka kamili hadi pale tutakapompata rais mpya, tassisi ya TWAWEZA ilitoa ripoti ambayo wengi hawakukuliana nayo. Nasi kama raia ambao wanapenda ukweli, sinabudi kuanzisha huu uzi kuangalia ukweli kwamba uchaguzi ukiitishwa leo kati ya Dr. Slaa, Edward Lowassa, Mizengo Pinda na Samwel Sitta nani atashinda?

Tafadhalini kila mwanajukwaa aliyesajiliwa apige Kura tujue mbivu na mbichi wa TWAWEZA

Ungewaomba wataalam wa IT wakutengeneze poll chart ambayo inahesbu kura yenyewe na percentages.
 
Back
Top Bottom