Jamii yatunyooshea vidole kisa kila ndoa inavunjika

Jamii yatunyooshea vidole kisa kila ndoa inavunjika

Papillon 1906

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
203
Reaction score
687
Hili tatizo limeota mizizi katika familia nimekuwa nikishuhudia ndugu zangu wakike hawaolewi na wakiolewa ndoa hazidumu. Nafikiri labda mizimu ya ukoo imekasirika au vipi lakini sio jambo la kawaida.

Nimejaribu kuunganisha doti maana babu alimuoa bibi akiwa na miaka 70+ huko na baada ya ndoa kupita hawakudumu wakapumzika kwa amani.
 
Hili tatizo limeota mizizi katika familia nimekuwa nikishuhudia ndugu zangu wakike hawaolewi na wakiolewa ndoa hazidumu. Nafikiri labda mizimu ya ukoo imekasirika au vipi lakini sio jambo la kawaida.

Nimejaribu kuunganisha doti maana babu alimuoa bibi akiwa na miaka 70+ huko na baada ya ndoa kupita hawakudumu wakapumzika kwa amani.
Tatizo hatuendi ndoani kama Mungu alivyoagiza ,wanaume wanavutiwa na inye gwedegwede na mwanamke mkwanja.
 
Hizi story za ndoa kuvunjika sana, naziona humu Jf. Mbona huku mtaani watu wanaishi vyema na familia zao na ndoa zao ? Sio kama watu wanavyokuza mitandaoni
 
Ugumu wa maisha unachangia kuvunjika kwa ndoa nyingi, teknolojia imewafanya watu kutamani vitu vizuri kutoka kwa wenza wao.​
 
Hili tatizo limeota mizizi katika familia nimekuwa nikishuhudia ndugu zangu wakike hawaolewi na wakiolewa ndoa hazidumu. Nafikiri labda mizimu ya ukoo imekasirika au vipi lakini sio jambo la kawaida.

Nimejaribu kuunganisha doti maana babu alimuoa bibi akiwa na miaka 70+ huko na baada ya ndoa kupita hawakudumu wakapumzika kwa amani.
Mteja wa Mwamposa huyu hapa.
 
Hili tatizo limeota mizizi katika familia nimekuwa nikishuhudia ndugu zangu wakike hawaolewi na wakiolewa ndoa hazidumu. Nafikiri labda mizimu ya ukoo imekasirika au vipi lakini sio jambo la kawaida.

Nimejaribu kuunganisha doti maana babu alimuoa bibi akiwa na miaka 70+ huko na baada ya ndoa kupita hawakudumu wakapumzika kwa amani.
Katika muktadha wa kimila na kiimani, jamii nyingi za Kiafrika huamini uwepo wa laana za kifamilia, maagano ya kale, au mizimu iliyokasirika kutokana na makosa ya mababu.

Kama unaamini upande huu, mara nyingi suluhisho hutafutwa kwa kukutanisha wazee wa ukoo kufanya matambiko ya kusafisha familia, au kupitia viongozi wa dini (makanisani au msikitini) kufanya maombi mazito ya toba ili kuvunja vifungo hivyo vya kiroho.Kwa upande wa kisayansi na kisaikolojia, wataalamu wanaeleza kuwa kuna tabia za kurithi za kisaikolojia (generational patterns) ambapo watoto hujifunza namna ya kuishi kwenye mahusiano kwa kuiga mifumo ya malezi waliyoiona nyumbani.

Wakati mwingine, kuona ndugu mmoja akishindwa ndoa hutengeneza hofu kubwa ya kisaikolojia kwa ndugu wengine, jambo linaloweza kuwafanya washindwe kuvumilia changamoto za kawaida za ndoa na kupelekea kutengana kwao.
Kuhusu historia ya babu na bibi kuoana katika umri wa miaka 70+ na kisha kupumzika kwa amani, kiuhalisia hili linaweza kuwa tukio la sadfa tu linalotokana na umri mkubwa na sababu za kibiolojia.

Ndoa katika umri huo mara nyingi hulenga kutafuta kampani ya uzee mwema na kusaidiana kimaisha, hivyo kufariki kwao baada ya muda mfupi hakuhusiani moja kwa moja na mikosi au laana ya vizazi vyenu vya sasa.

Hata hivyo Kutokana na mtazamo wa kiroho wa kiislamu na kikristo, changamoto kama hizi hutazamwa kama vifungo vya kiroho au laana za vizazi vilivyosababishwa na makosa ya mababu wa kale.

Maandiko yanaeleza kuwa ahadi, matambiko, au maagano yaliyofanywa na wazee wetu yanaweza kufungua milango ya kiroho inayoruhusu nguvu za giza kufuatilia maisha ya vizazi vinavyofuata, hususan katika maeneo muhimu kama ndoa.

Ili kukabiliana na hali hii, waumini hushauriwa kufanya maombi mazito ya toba ya kuomba msamaha kwa niaba ya ukoo, kufunga, na kuvunja madhabahu hizo za kale kwa mamlaka ya kiimani ili kuanzisha mwanzo mpya wenye baraka na ulinzi wa Mungu.
 
Hizi story za ndoa kuvunjika sana, naziona humu Jf. Mbona huku mtaani watu wanaishi vyema na familia zao na ndoa zao ? Sio kama watu wanavyokuza mitandaoni
Mitandao ni kokoro.

Kule baharini kokoro kazi yake kubeba kila kitu kisafi na kichafu.
 
Inawezekana kabisa, maana ukiangalia kwenye mitandao unaweza hisia nchi nzima ndoa zimevunjika 😅
Zingatia neno Kokoro.
Kwa mfano mimi binafsi mtandaoni ndani ya saa moja naweza nikaandika kwemye nyuzi tofuati tofauti kwamba nipo single, kwingne nimeoa, kwingime nina mchumba. Ili mradi tu kuwavuruga wanaosoma na kufuatilia fuatilia watu.
 
Na kama mtu una roho ndogo huwezi ingia kwenye ndoa kwa story za mitandaoni,kumbe live watu wanaburudika zao
Kuna chi nasikia ulaya, imepiga maruku matumizi ya mitandao kabla ya umri flani. Maana watoto ambao hawajapevuka akili kutwa wakiwa wanasoma mambo mabaya mabaya kuhusu ndoa wanajengewa kitu mbaya sana ambayo kama leo baadhi tayari imewaangia kwenye akili wanaogopa ndoa kupita kiasi
 
Matokeo ya mkutano wa Beijing ... now 30th anniversary of the landmark 1995.

Na kwa sasa mtoto wa kiume ameachwaa ...... expect next 20 - 30 years matokeooo

Kila mwenye mtoto ataanza kumpa maneno ya hisiaa ili akikua aamue mrengo aupendaooo

Watoto wa kiume hawaimariki kuweza kuwapokea wasichana na wala watoto wa kike hawaimarishwi kuishi mahusiano mema

* Usijilazimishe ingia kwa ndoa fuata hisia zako
 
Kuna chi nasikia ulaya, imepiga maruku matumizi ya mitandao kabla ya umri flani. Maana watoto ambao hawajapevuka akili kutwa wakiwa wanasoma mambo mabaya mabaya kuhusu ndoa wanajengewa kitu mbaya sana ambayo kama leo baadhi tayari imewaangia kwenye akili wanaogopa ndoa kupita kiasi
Ni hatari sana kwa akili changa aisee!
 
Hizi story za ndoa kuvunjika sana, naziona humu Jf. Mbona huku mtaani watu wanaishi vyema na familia zao na ndoa zao ? Sio kama watu wanavyokuza mitandaoni
Ndoa za JamiiForums lazima zivunjike maana sio halisi, pili wanawake wamekuwa wajuaji (Feminists), ni nadra sana kuona mwanamke ambaye ni mwanasheria, wakili au jaji ana ndoa, pia mwanamke ambaye ni daktari ana ndoa na mwanaume ambaye sio daktari au msomi.

Ndoa zinazodumu ni za vijijini ambapo kijana anaoa binti (16-21) ambaye ni bikra amelelewa kwenye maadili. Na hao hawapo JamiiForums.
 
  • Thanks
Reactions: Oho

Similar Discussions

Back
Top Bottom