Jamii Media yafungua Kesi ya Kikatiba kupinga Vifungu vya Sheria ya Makosa ya Mtandao

Heko jamii forum kwa msimamo huu ambao unaonyesha upevu na kuchukua majumu ipasavyo katika jambo hili
 
Tatizo la nchi yetu huwa haipendi kitu kinachoitwa MADE IN TANZANIA, Jamii Forum ni kama vile Facebook kwa wamerekani ambapo wana fursa ya ku-access huduma mbalimbali (mbona hawajawaandikia facebook), hivyo tukipende chetu ambacho kinatoa vitu kwa level ya kikwetukwetu tena tofauti na facebook kama habari inakuwa inauhakika uzi huwa unapotezwa tofauti na facebook. Wakileta zengwe madhara yatakuwa zaidi maana watu watahamia facebook na kuandika majina ya uongo na wakiwa wana habari tata hata uzushi wanaingia internet cafe.
 
KWA MTINDO HUU WA KUANDAMA WHISLE BLOWERS SIDHANI KAMA KUNA RAIA ATAKUWA TAYARI KUSHIRIKIANA NA POLISI KUZUIA UHALIFU. YAANI MTU UNATOA TAARIFA YA KIFISADI BADALA KUPONGEZWA, UNAKANDAMIZWA!
Yaani acha tu unaweza usitoke kabisa kituo cha polisi ndio maana labda watu wanaogopa atakujitokeza kuwatumbua wauza unga na majambazi yanayojulikana mtaani kwao; leo tena ujifanye unaenda kusema mambo ya ufisadi serikarini kwa utaratibu huu ujitakii mema. Sasa tena ata huku kwenye faragha nako awatakii watu waseme hii ndio polisi yenyewe isiyotaka tips hawa kweli wana nia ya kupambana na wanayosema.
 
lengo lao kubwa wanataka habari azisitufikie sisi huku watz ambao ni wa muhimu kupata habari mbalimbali za uharifu wao sijui serikali ina nn na wananchi wake hawataki wananchi wake tujue kinachoendelea kwenye nchi yetu hawa watu wa ajabu sana
 
ile kesi ya msingi kuhusu cybercrime iliyofunguliwa kipind kile imeishia wap?
 
Serikali ya awamu hii sijui kwa nini inataka kubana uhuru wa habari, Sijui wanahofia nini!, Watanzania tulikuwa tumepiga hatua kubwa sana kwenye uhuru wa habari sasa tunarudi nyuma kwa kasi ya ajabu
 
Magufuli akitaka kuongoza nchi hii vizuri basi aviruhusu vyombo vya habari vifanye kazi yake na mitandao ya kijamii. Kwa kuvikandamiza watu wataficha taarifa nyeti ambazo zingeisaidia serikali.
 
Tusimame kwa pamoja kuitetea JF bila kujali itikadi zetu.
Natamani kila member atie neno kwenye uzi huu.
HATA NA MM NATUA NENO
Jamani tuisaidie Jamii Media hata kwa ile michango ya kawaisa imefia wapi?@Mushi Maxence Melo kampuni la Appe huko Marekani limeigomea Serikali na FBI yake kuweka bayana siri za mteja aliyelipua majengo, na sasa Makampuni yote ya simu yanaiunga mkono Apple
MY TAKE
kuanza kutengana au kumuachia Max na Mushy ndio mwanzao wa kila Member kukamatwa hata km hatahusika na Jukwaa la Siasa
tuache Itikadi Hapa Serikali ilichemsha na hasa Bunge kwa kumsikiliza Nape na Makamba
Uhuru wa habari haupo tena
635918600698647000-AP-rich-drew-tim-cook-quote.jpg

Apple CEO Tim Cook, pictured in April 2015, says his company will resist a federal magistrate's order to hack its own users in connection with the investigation of the San Bernardino, Calif., shootings. (Photo: Richard Drew, AP)

635918611338539204-manu-fernandez-ap-zuckerberg.jpg

Facebook CEO Mark Zuckerberg sides with Apple during the Mobile World Congress wireless show in Barcelona (Photo: Manu Fernandez, AP)
Apple vs. the FBI: Who said what — and which side are they on?
 
Kampuni ya Jamii Media ambayo ndiye wamiliki na waendeshaji wa mitandao ya JamiiForums na FikraPevu wamewasilisha mashtaka Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kupinga ushuruti waliopewa na Polisi kutoa taarifa binafsi za wanachama wake.

Ushuruti unakuja kutokana Sheria ya Uhalifu Mitandaoni (Cyber crime law).

Taarifa ya kilichojiri zitawajia punde.

Naona hakuna update ya Kesi hii?
 
Bongo hii kila kitu kinaenda na kupita kama upepo! Anyway yeyote mwenye taarifa hii !
cc. Invisible
Kesi kama hizi zinakuwa na nguvu kwenye nchi zinazofuata sheria , nchi zinazosigina katiba ni kazi bure tu , kesi ya msingi haijafika hata nusu , mkuu wa jf kakamatwa !
 
J
Kwa Heshima ya kipekee nawapongeza Jamii Media kwa kuamua kulinda Uhuru na faragha ya watumiaji wa Mitandao na pia kwa kupigania haki ya kikatiba ya watanzania na kupingana na masharti kandamizi yasiyo ya kistaarabu katika karne hii ya sayansi na Teknolojia

Nimekua mwanachama wa JamiiForums Tangu Tarehe 18 July,2007 nikiwa Mwaka wa Pili Chuo kikuu na hapo kabla nilikuwa Mwanachama ambaye sikuwa nimesajiliwa

Tumekuwa na WanaJF wengi hapa wenye fani na taaluma mbalimbali.Pia viongozi wa Vyama,Serikalini,Mashirika na hata viongozi wa Dini.Wengine kwa majina yao halisi na wengine ya kificho (Baadhi yao Tunatambuana).

Katika Uanachama wangu JF nimewahi kupata misukosuko mingi na Jeshi la Polisi kutokana na michango yangu humu likiwemo tukio la Kuitwa Polisi asubuhi ya Tarehe 20 December 2013 siku ya Ijumaa na kuhojiwa kisa nilianzisha mjadala dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani kipindi Hicho Emmanuel Nchimbi.

Polisi waliniambiwa kuna jalada ambalo liletwa na Dr.Nchimbi.Nikiambatana na Wakili Msomi Peter Kibatala Nilihojiwa kwa masaa kadhaa hadi kufukua thread na kuomba Password zangu za JF na Barua Pepe .Niliwakatalia kwa kuwa hawakua na haki hiyo

Hata hivyo Jioni yake kufika saa 3 Usiku aliyepeleka Jalada Hakuwa Waziri tena(Rejea Operesheni Tokomeza Bungeni).Ilikuwa Coincidence au Mipango ya Mungu?

Ni katika mazingira hayo niliona tishio la haki ya uhuru wa faragha na jinsi ambavyo vyombo vya dola pasipo uhalali wowote wanaweza kuhujumu haki za Raia na pia kukandamiza kabisa uhuru wa habari,haki ya kupewa Taarifa na pia kukandamiza haki za msingi kabisa za binadamu na kutishia misingi ya ukuaji wa utawala bora ambayo inashikiliwa na nguzo kuu mbili za uwazi na uwajibikaji

Ni jambo la ajabu kuwa serikali iliyoahidi kurekebisha sheria ya mitandao inaendelea kutumia dola kukandamiza vyombo vya habari

Kwa uamuzi huu wa JamiiMedia,Nitaungana katika mapambano haya kuilinda sio Jamii Forums Pekee bali haki za watanzania

JF ni nyumbani,Ni Chuo .Tubuni njia ya kuisapoti JF kwa kishindo katika kipindi hiki
Jamani Ben!
 
Back
Top Bottom