Jamii inaheshimu kazi yako, siyo sura

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,527
14,399
1. Pundamilia anavutia lakini anaishi na wanyama porini, Punda wa kawaida havutii lakini anaishi majumbani na watu.

2. Huyu Punda wa kawaida uwezo wake wa kubeba mizigo (kuchapa kazi) ndo umempa heshima ya kuishi na watu mujini.

3. Kwa mfano huu tunajifunza kwamba katika jamii ya leo kinachokupa heshima ni kazi unayofanya, siyo uzuri ulionao ndiyo maana watu watakuuliza unafanya kazi gani ili waone heshima ya kukupa.

4. Kazi ni kipimo cha utu. Hutaki kazi kaishi porini na Pundamilia. Unataka heshima fanya jambo la heshima.

5. Binadamu hajawahi kuheshimu mtu, anaheshi alicho nacho mtu!

6. Usipojituma kufanya kazi sura yako ya malaika, shingo ya upanga, macho yako ya golori, kiuno cha Ray C, miguu ya bia, rangi ya Mtume na muondoko wa twiga vitakupa pesa ya kula na kwenda saluni tu; ukitaka pesa ya maana kachape kazi.

7. Kufanya kazi ni kushiriki uumbaji wa Mungu katika ulimwengu unaoishi. Hata kwa nyie vijana wangu msipiganie uhandsome, piganieni kuchapa kazi.

8. Ukichapa kazi utapata maisha, ukipata maisha utakuwa handsome automatically alisema Diamond wa Tanzania.
 
Nchi za laana zinatumikisha punda sio kwamba punda wanapenda ni laana za Jami
Na ukitaka kujua punda mwenyewe hapendi michongo ya kutwishana mizigo mizito alafu unamwambia aende,hebu jaribu kumbebesha na mwanae.

Atakumaindi sana,na anaghaili kutembea mpaka utue madumu yako ya maji kwenye mkokoteni wa mwanae. Na Nina uhakika ile moment anakugomea ni kama anakutukana uache mambo ya kishamba ya kutwishana mizigo mizito. Watoto wa Leo wanakuambia,"kuwa wewe kuweza"?
 
Na ukitaka kujua punda mwenyewe hapendi michongo ya kutwishana mizigo mizito alafu unamwambia aende,hebu jaribu kumbebesha na mwaneo.

Anakumaindi kishenzi,na anaghaili kutembea mpaka utue madumu yako ya maji kwenye mkokoteni wa mwanae. Na Nina uhakika ile moment anakugomea ni kama anakutukana uache mambo ya kishamba ya kutwishana mizigo mizito. Watoto wa Leo wanakuambia,"kuwa wewe kuweza"?



Point Sana hii , mawazo ya laana ya mtoa mada akili ndogo
 
1. Pundamilia anavutia lakini anaishi na wanyama porini, Punda wa kawaida havutii lakini anaishi majumbani na watu.
2. Huyu Punda wa kawaida uwezo wake wa kubeba mizigo (kuchapa kazi) ndo umempa heshima ya kuishi na watu mujini.
3. Kwa mfano huu tunajifunza kwamba katika jamii ya leo kinachokupa heshima ni kazi unayofanya, siyo uzuri ulionao ndiyo maana watu watakuuliza unafanya kazi gani ili waone heshima ya kukupa.
4. Kazi ni kipimo cha utu. Hutaki kazi kaishi porini na Pundamilia. Unataka heshima fanya jambo la heshima.
5. Binadamu hajawahi kuheshimu mtu, anaheshi alicho nacho mtu!
6. Usipojituma kufanya kazi sura yako ya malaika, shingo ya upanga, macho yako ya golori, kiuno cha Ray C, miguu ya bia, rangi ya Mtume na muondoko wa twiga vitakupa pesa ya kula na kwenda saluni tu; ukitaka pesa ya maana kachape kazi.
7. Kufanya kazi ni kushiriki uumbaji wa Mungu katika ulimwengu unaoishi. Hata kwa nyie vijana wangu msipiganie uhandsome, piganieni kuchapa kazi.
8. Ukichapa kazi utapata maisha, ukipata maisha utakuwa handsome automatically alisema Diamond wa Tanzania.
Hasa kwa mwanaume
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom