Fall Army Worm
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 19,331
- 14,259
Kabisa Chifu,Ruge ni Mwamba.Na wote tunyanyue vibuyu na vipeyu vyetu vya rubisi juu huku tukisema ..."viva Ruge...vivaaaa and hooray to the hero of the "neshion"...!
Kabisa Chifu,Ruge ni Mwamba.Na wote tunyanyue vibuyu na vipeyu vyetu vya rubisi juu huku tukisema ..."viva Ruge...vivaaaa and hooray to the hero of the "neshion"...!
Mtanzania ametanguliza mahaba kabla ya ufahamu....Ajabu kuna watu humu ht kusoma hii habari wakaelewa hawajaisoma wamekurupuka ku comment mara Mwendazake kaitia hasara inchi, mara apewe bandari mara anaidai serikali...JF imekua na watu wa hovyo sana now days, ht km ni Uhuru wa mawazo huu hapana aisee...
and this is a reflection ya jinsi information warlfare ilivyo ngumu..mtu anaweza kufanya character assasination na mijitu ya hovyo yakarukia habari ki ushabiki shabiki bila ku verify habari husika
Baada ya kusota rumande kwa zaidi ya miaka minne kabla hajaachiwa hivi karibuni, hatimaye mfanyabiashara maarufu nchini, James Rugemalira ameanza harakati za kuzishtaki kampuni na taasisi za fedha anazozituhumu kuhusika katika wizi wa fedha za Serikali zilizomsababishia kesi ya uhujumu uchumi.
Katika kutimiza azma yake hiyo, Rugemalira amewasilisha maombi ya kibali cha kufungua na kuendesha mashtaka hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu dhidi ya kampuni na taasisi hizo kama mwendesha mashtaka binafsi.
Mfanyabiashara huyo aliyekaa ndani kwa miaka minne na miezi mitatu, ameachukua hatua hiyo ukiwa ni mwezi mmoja na nusu tangu alipotoka mahabusu baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kumfutia mashtaka yaliyokuwa yakimkabili yeye na wenzake watatu, Septemba 16.
Katika mchakato huo Rugemalira ambaye ni mmliki wa kampuni ya VIP Engineering and Marketing Limited, amefungua maombi hayo dhidi ya watuhumiwa 11 zikiwamo taasisi za fedha na watu binafasi ambao anawatuhumu kuisababishia Serikali hasara ya Sh 61 trilioni.
View attachment 1996474
Maombi hayo tayari yamepangwa kusikilizwa mahakamani hapo Novemba 10 mwaka huu, na pande zote yaani waombaji (Rugemalira na kampuni yake ya VIP Engineering) na wajibu maombi wote wametakiwa kufika siku hiyo kwa ajili ya kuyasikiliza maombi hayo.
Wajibu maombi hao ambao Rugemalira anawatuhumu ni Benki ya Standard Chartered (Hong Kong), Benki ya Standard Chartered Tanzania, Benki ya Standard Chartered (Malaysia) Berhad, Wartsila Netherlands B.V na Wartsila Tanzania Limited.
Wengine ni Sanjay Rughani ambaye kwa sasa ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Samir Subbrwai ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered (Hong Kong), Abrar Anwai ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered (Malyasia) Berhad.
Vilevile wamo Bill Winters, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered na Hakan Agnevall ambaye ni Rais na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wartsila Corporation.
Katika hati ya kiapo kinachounga mkono maombi hayo, Rugemalira anayejitambulisha kama mshauri binafsi wa kimataifa wa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) na mwanahisa mkuu wa VIP Engineering and Marketin Limited, anaanza kwa kutoa historia ya sakata hilo.
Anadai mwaka 2005 baada ya IPTL kufunga shauri lililokuwa limeanza tangu Februari 25 mwaka 2002, Benki ya Standard Chartered (SCB) kupitia kampuni tanzu yake, Benki ya Standard Chartered (Hong Kong) na Danaharta (SBCHK) walikusudia kuandaa mkataba wa makubaliano na, uuzaji na ununuzi wa IPTL.
Hata hivyo, Rugemalira anaituhumu Kampuni ya Mechmar ambayo ilikuwa mbia mkuu wa IPTL kula njama na SCB kukwepa kulipa dola 4.2 milioni za Marekani ambazo ni asilimia nne ya ushuru wa forodha katika mkopo wa IPTL wa dola 105 milioni wa Juni 28 mwaka 1997.
Rugemalira anadai katika kiapo chake kuwa kukwepa malipo hayo ni kosa la jinai chini ya Kifungu cha 73(2)(a) cha Sheria ya Ushuru wa Forodha iliyorekebishwa mwaka 2019.
Pamoja na makosa mengine aliyoyaainisha, Rugemalira anadai maombi hayo yanakusudia kurejesha Sh61 trilioni ambazo Standard Chartered Bank Group na washirika wake walifanya ulaghai kuchepusha fedha hizo kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na VIP Engineering isivyo halali.
Rugemalira na mwenzake Harbinder Singh Seth, walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Kisutu Juni 19, mwaka 2017 wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi iliyokuwa na mashtaka 12 kabla ya kuongezwa aliyekuwa mwanasheria wa IPTL, Joseph Makandege.
Kesi hiyo ilitokana na kashfa ya uchotaji wa mabilioni ya pesa katika akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa imefunguliwa Benki Kuu kutokana na mgogoro wa malipo ya gharama za uwekezaji kati ya IPTL na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) lililopinga malipo hayo kuwa yalikuwa makubwa.
Akaunti hiyo ilifunguliwa kwa pamoja na pande hizo mbili kwa ajili ya kuhifadhi fedha za malipo hayo kusubiri utatuzi wa m
Tetetete Bashite kwenye ubora wakoKwani wewe ujui kiswahili ni lugha mbovu sana bado sasa Rais ndiyo kitu gani kwenye sarufi za kiswahili tatizo tunatabia ya kujiona wasomi kwa kushikamana na makosa ....lugha sahihi ni RAISI SIYO RAIS
Mfano maeno KAZI RAHISI huwezi kusema KAZI RAHIS kiswahili hakina mtindo huo, sema wasomi feki tulio nao ndiyo wamesababisha neno Raisi liwe kosa wakati ndiyo neno sahihi
Zoezi lilianza 2002 huko,JK akusaidie nini?Y usimfufue Ben ndiyo akusaidie!.Huyu Mzee anajua mambo mengi sana ambayo serikali haiyajui ama imeyafumbia macho makusudi..
Kwa hii kesi ndio utajua hii nchi inaliwa kwa namna gani
Kikwete kuna maswali inabidi atusaidie kujibu hapa.
Kikwete akikujibu unitag pleazeHuyu Mzee anajua mambo mengi sana ambayo serikali haiyajui ama imeyafumbia macho makusudi..
Kwa hii kesi ndio utajua hii nchi inaliwa kwa namna gani
Kikwete kuna maswali inabidi atusaidie kujibu hapa.
Kalia dole la kati soma uelewe sio kilakitu unamuangushia jumba bovu magufuli.Mwendazake ni mleta hasara tu kwa nchi.
- Alikamata meli ya kigeni,mwisho wa kesi nchi ikalipa wageni,
- Akahonga nyumba za serikali kwa washikaji na concubines,serikali ikala hasara,
- Ujenzi wa "mabharabhara" na ununuzi wa "vivukio" ukafanywa kimagumashi,serikali ikalipa na kula hasara,
- Kawasotesha "watu" bila hata hatia,wanaidai serikali.Italipa na kuleta hasara/mahasara.Yuleee,akajitorokea aibu!
Hapa nilimaanisha endapo ukwapuaji huu unahusisha baadhi ya vigogo wa serikali, kuna uwezekano mkubwa hii kesi ikapotezewa. Yetu macho.Kwenye 61 Trillion ni serikali gani ambayo haitokuwa interested?
Eeh hilo nalo neno! Kama kuna 10% zilishapitaga hapo kesi hamnaHapa nilimaanisha endapo ukwapuaji huu unahusisha baadhi ya vigogo wa serikali, kuna uwezekano mkubwa hii kesi ikapotezewa. Yetu macho.
endelea kukariri mama mdogoUnadhani rugemalila ana njaa Kama wewe umelizika na kamshahara kako ka laki 9 na ka IST unajiona maisha umemaliza
Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
Kumtoa JK kwenye hili suala ni kama kujaribu kuuficha moshi.Zoezi lilianza 2002 huko,JK akusaidie nini?Y usimfufue Ben ndiyo akusaidie!.
Je, jiwe ni binadamu? Hana utu na mtumia mabavu, JK alimweka makusudi kwa sababu sisi kulialia, anasema anawaletea mkali ikawa balaa, mwenyewe JK anachekaaa, na kusema anaongoza vizuri sana!Jiwe kwa Nini hakumsikiliza
Mwendazake ni mleta hasara tu kwa nchi.
- Alikamata meli ya kigeni,mwisho wa kesi nchi ikalipa wageni,
- Akahonga nyumba za serikali kwa washikaji na concubines,serikali ikala hasara,
- Ujenzi wa "mabharabhara" na ununuzi wa "vivukio" ukafanywa kimagumashi,serikali ikalipa na kula hasara,
- Kawasotesha "watu" bila hata hatia,wanaidai serikali.Italipa na kuleta hasara/mahasara.Yuleee,akajitorokea aibu!
Ukimaliza kumlilia mjomba wako,nistue nikupe rubisi unywe.Homa ya Magufuli haitaisha sasa hivi.
Kesi za huyo mzee got none to do with Magu ila Kikwete...
Meza vidonge mkuu ..
Niambie wewe usiyekuwa bashite kiswahili kina fasihi ngapi ? nataka nikuonyeshe upumbavu wako sasa hiviTetetete Bashite kwenye ubora wako
He is still alive in your head.Ukimaliza kumlilia mjomba wako,nistue nikupe rubisi unywe.