Jambo leo: Mtwara wakubali gesi itoke.

Jambo leo: Mtwara wakubali gesi itoke.

Propaganda hizo,mm nadhani ikawa hali ni hiyo wanajipanga na plan B,ya kuhujumu bomba

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Katika pitia pita ya magazeti asubuhi hii imedaiwa kuwa wana Mtwara wamekubali kuwa gesi itoke mkoa humo kwa kuwa walikua hawajui faida za gesi watakazo pata kwa ujumla.

Napenda kujua habari hizi ni kweli kwa Wanamtwara??

Kama ni kweli hongereni sana kwa vikao mlivyokaa na kuamua hayo
 
Gazeti la Jambo leo ni chombo cha propaganda za CCM na serikali.
Bora gazeti la Uhuru kuliko jambo leo.
Hata vitumbua halifai kufungia.
Linafaa kutumika chooni tu.
 
Si walujifanya kubana haoooo wameachiiiaaa chezea Dola wewe nimesikitika wale Wabunge wapenda sifa za kukamatwa hatukuwaona wakikamatwa
 
Gazeti la jambo leo limeandika "Mtwara wakubali gesi itoke" wanasema ni baada ya jeshi la wananchi wa Tanzania kwenda kurejesha amani, salamu ya wana mtwara imebadilika kutoka "Gesi haitoki" hadii kuwa "Gesi inatoka".

hata mwanzoni tuliaminishwa hivyo kuwa kila kitu kipo sawa.
 
Gazeti la Jambo leo ni chombo cha propaganda za CCM na serikali.
Bora gazeti la Uhuru kuliko jambo leo.
Hata vitumbua halifai kufungia.
Linafaa kutumika chooni tu.

Bila shaka limeamua kufanya propaganda kwa kuujifanya limehoji wanamtwara na wakakubaliana kuwa sasa gesi inatoka na wamekubali kubadili kauli kuwa "gesi haitoki" hadi kuwa "gesi inatoka".

Kuna udhaifu mkubwa sana kwenye sheria zetu! Sheria zina semaje kuhusu vyombo vya habari kuandika propaganda na uwongo kwenye masuala nyeti?!
 
nguvu ndiyo njia pekee kama watu wamechoka kuheshimiwa,jeshi na polisi endeleeni kuwanyoosha wahuni.
 
Bila shaka limeamua kufanya propaganda kwa kuujifanya limehoji wanamtwara na wakakubaliana kuwa sasa gesi inatoka na wamekubali kubadili kauli kuwa "gesi haitoki" hadi kuwa "gesi inatoka".

Kuna udhaifu mkubwa sana kwenye sheria zetu! Sheria zina semaje kuhusu vyombo vya habari kuandika propaganda na uwongo kwenye masuala nyeti?!

hata mimi huwa zinanichanganya nikiangalia hata wanavyoandika tanzania daima ni uongo na uchochezi sijui kwa nini hawashitakiwi.
 
busara ikitumika mambo huwa mepesi lakini wakiweka bangi mbele wanamtwara watajuta daima dola si mchezo.
 
kama ingekua ni kusoma magazeti tu, basi pasingekua na vurugu zilizotokea
 
Back
Top Bottom