Jambo leo: Mtwara wakubali gesi itoke.

Jambo leo: Mtwara wakubali gesi itoke.

Gazeti la jambo leo limeandika "Mtwara wakubali gesi itoke" wanasema ni baada ya jeshi la wananchi wa Tanzania kwenda kurejesha amani, salamu ya wana mtwara imebadilika kutoka "Gesi haitoki" hadii kuwa "Gesi inatoka".

CC THE BIG SHOW

Kuna njia nyingi za kuchochea vurugu. Moja ni kuwaunga mkono wanaofanya vurugu kwa kuwaambia kuwa wanachokifanya ni sahihi. Njia hii hutumiwa na wajasiri ambao huamini wanachokisema. Na njia ya pili ambayo hutumiwa na wanafiki na waoga ni kuwaambia kuwa mmekubaliana na na wapinzani wenu wakati ukijua kuwa hawajakubaliana. Hawa jambo leo wanachochea vurugu kwa nja ya pili.
 
Gazeti la jambo leo limeandika "Mtwara wakubali gesi itoke" wanasema ni baada ya jeshi la wananchi wa Tanzania kwenda kurejesha amani, salamu ya wana mtwara imebadilika kutoka "Gesi haitoki" hadii kuwa "Gesi inatoka".

CC THE BIG SHOW

mkuu the big show upo?sema neno jambo leo wachitike
 
Last edited by a moderator:
Nishaacha kusoma magazeti sasa miaka sita, nitarudi kuyasoma baada ya 2015.
 
Gazeti la jambo leo limeandika "Mtwara wakubali gesi itoke" wanasema ni baada ya jeshi la wananchi wa Tanzania kwenda kurejesha amani, salamu ya wana mtwara imebadilika kutoka "Gesi haitoki" hadii kuwa "Gesi inatoka".

CC THE BIG SHOW

Kama kuna uchochezi ambao hautakiwi kufumbiwa macho huu ni mmoja wapo,kauli kama hizi ndizo zinapelekea waandishi wa namna kama hii wanachomewa nyumba zao moto pindi vurugu zinapotokea.Mwenzako Muongo kayasababisha haya yaliyotokea kwa sentesi moja tu ya mstari wake wa hotuba yake pale aliposema "Mpango wa serikali kujenga bomba la gesi upo pale pale na hautaweza kukwamishwa na kundi lolote la watu".
 
Bila shaka limeamua kufanya propaganda kwa kuujifanya limehoji wanamtwara na wakakubaliana kuwa sasa gesi inatoka na wamekubali kubadili kauli kuwa "gesi haitoki" hadi kuwa "gesi inatoka".

Kuna udhaifu mkubwa sana kwenye sheria zetu! Sheria zina semaje kuhusu vyombo vya habari kuandika propaganda na uwongo kwenye masuala nyeti?!

Mkuu Mohamedi Mtoi, jambo lolote linalohusisha watu wengi huwa na mushkeli. Jambo Leo linaripoti kuwa WAMEKUBALI, hizi tutaita propaganda, lkn litakaloripoti WAMEKATAA tutasema limesema kweli. Jambo la kujiuliza ni kwamba hawa wote wawili wanamhoji nani?

Wakati tunaona watu na mabango mitaani na nyumba zikichomwa moto, kuna ambao wamesalia majumbani mwao wakikerwa kweli kweli na hayo maandamano. Ila kwa kuwa hawa wameamua kufanya fujo, basi wanaonekana kuwasemea wenzao.

Hata mimi nina jamaa zangu Mtwara, wao maoni yao ni kwamba, fujo hizi zinaletwa na watu wasio na kazi na ni kwa yale walioambiwa na wanaowachochea.

Kuna bwana mdogo mmoja aliwahi kuniambia hivi wakati wa zile fujo za kwanza: HATA MTWARA NAYO INATAKIWA KUENDELEA KAMA BAGAMOYO NA KATAVI. Ukiyatafakari haya utaona ni upuuzi wa kuambiwa, ila kwa mimi niliyefika Mtwara, Katavi na Bagamoyo namuonea tu huruma kwa kuwa na mshawasho wa kujitafutia madhila kwa jambo la kijinga kabisa kwani Mtwara ni mji mkubwa kuliko Katavi na Bagamoyo.

Hapa utaona ni kwamba kalishwa tu maneno kwa kuwa Katavi anatoka PM na Bagamoyo President. Sasa je, tunapaswa kuamini kuwa kila aishie Mtwara anaamini haya? Na Mtwara haiishii Mikindani, mpaka Newala ni Mtwara, je huko nako wanasemaje?
 
Last edited by a moderator:
Gazeti la jambo leo limeandika "Mtwara wakubali gesi itoke" wanasema ni baada ya jeshi la wananchi wa Tanzania kwenda kurejesha amani, salamu ya wana mtwara imebadilika kutoka "Gesi haitoki" hadii kuwa "Gesi inatoka".

CC THE BIG SHOW


Hakuna kitu kama hicho,machafuko mengine yametokea usiku wa jana huko msimbati,
unasomaje gaezi la habari leo na kusikiliza Tbccm?
Soma nipashe upate habari yote...
Ngoma hii wataisoma mwaka huu...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mohamedi Mtoi, jambo lolote linalohusisha watu wengi huwa na mushkeli. Jambo Leo linaripoti kuwa WAMEKUBALI, hizi tutaita propaganda, lkn litakaloripoti WAMEKATAA tutasema limesema kweli. Jambo la kujiuliza ni kwamba hawa wote wawili wanamhoji nani?

Wakati tunaona watu na mabango mitaani na nyumba zikichomwa moto, kuna ambao wamesalia majumbani mwao wakikerwa kweli kweli na hayo maandamano. Ila kwa kuwa hawa wameamua kufanya fujo, basi wanaonekana kuwasemea wenzao.

Hata mimi nina jamaa zangu Mtwara, wao maoni yao ni kwamba, fujo hizi zinaletwa na watu wasio na kazi na ni kwa yale walioambiwa na wanaowachochea.

Kuna bwana mdogo mmoja aliwahi kuniambia hivi wakati wa zile fujo za kwanza: HATA MTWARA NAYO INATAKIWA KUENDELEA KAMA BAGAMOYO NA KATAVI. Ukiyatafakari haya utaona ni upuuzi wa kuambiwa, ila kwa mimi niliyefika Mtwara, Katavi na Bagamoyo namuonea tu huruma kwa kuwa na mshawasho wa kujitafutia madhila kwa jambo la kijinga kabisa kwani Mtwara ni mji mkubwa kuliko Katavi na Bagamoyo.

Hapa utaona ni kwamba kalishwa tu maneno kwa kuwa Katavi anatoka PM na Bagamoyo President. Sasa je, tunapaswa kuamini kuwa kila aishie Mtwara anaamini haya? Na Mtwara haiishii Mikindani, mpaka Newala ni Mtwara, je huko nako wanasemaje?

All this ni uchaguzi 2015. Si kweli kwamba Gas ni lazima isafirishwe kuja Dar ili iwe na manufaa kiuchumi,lakini ni kweli kwamba kama Gas itasafirishwa kutoka mtwara kuja Dar kuna civil work yenye MSHIKO wa NGUVU,maana hela ya kujengea miundombinu ya kusafirishia gasi hadi Dar ni ndefu sana ambayo itawasaidia baadhi ya Watu kwenye uchaguzi wa 2015, hivyo basi wakazi wa Mtwara ama wakaubali Gasi isafirishwe then baada ya 2015 iangaliwe namna ambavyo wanaweza ku reverse uamuzi huo huku wakiwa wamepata hela zitokanazo na mradi huo, hii ni version mpya ya EPA na wala si swala la Gasi kusafirishwa ama lah... Mtwara wanajisumbua sana watakufa wengi lakini miundombinu ya kusafirishia gasi itajengwa hata kama Gasi haitasafirishwa.
Mtwara kuweni wapole tu, hamuwezi kubadili matokeo ya mechi hii,yamekwisha kupangwa,kinachosubiriwa ni filimbi ya kumaliza mchezo.
 
mkuu the big show upo?sema neno jambo leo wachitike

Watanzania wengi kwa sasa si watu wenye kukubali propaganda mfu kama hizo,
alisema pinda kwamba kayamaliza,
je leo kiko wapi?
Time will tell them,eti mtwara wamekubali gesi itoke?nani wamemuhoji??
 
“Mpango wa kusafirishwa kwa gesi
asilia hatuna mpango nao kwa wakazi
wote wa Mtwara kwa kifupi akina mama
wa mtwara hatutaki itoke,” alisema
Fatuma Abdallah.
 
kama serikali tumekwisha buni mipango sahihi ya kukabiliana na fujo zinazoendana na rasilimali. tumeamua maeneo yote yenye rasilimali kuitangaza miakoa mipya hapa tutakuwa na mkoa wa songosongo, mkoa wa mchuchuma, mkoa wa nyarugusu mkoa wa mererani na mingine. hii mikoa itakuwa na watu wachache ambao watapewa kipaumbele katika shughuli zinazofanyika katika mikoa hii na tutawaboreshea huduma za jamii na sehemu kubwa ya mapato itakuwa ikiwahudumia watanzania wote.Ndugu spika wa JF naomba kuwasilisha. naomba kila msomaji alipo anapomaliza anasimama kuunga hoja mkono
 
Hao jambo leo wameamua kuwadanganya wakubwa wao. kimsingi wenyeji wa Mtwara jambo hili limewaunganisha pamoja kuliko DINI,KABILA AU VYAMA VYA SIASA.Wanaweza kutulia kwa muda lakini sidhani kama watakubali gesi itoke bila hatima ya maisha yao in connection na gasi yatakuwaje.taratibu siku hizi unaona jinsi hata wageni kutoka mikoa mingine ambavyo hawaaminiwi sana kushirikishwa kwenye mazungumzo yao nyeti kuhusu gesi.SASA HAO JAMBOLEO WANAANDIKA UONGO KWA FAIDA YA NANI?
 
Bila shaka limeamua kufanya propaganda kwa kuujifanya limehoji wanamtwara na wakakubaliana kuwa sasa gesi inatoka na wamekubali kubadili kauli kuwa "gesi haitoki" hadi kuwa "gesi inatoka".

Kuna udhaifu mkubwa sana kwenye sheria zetu! Sheria zina semaje kuhusu vyombo vya habari kuandika propaganda na uwongo kwenye masuala nyeti?!

Mambo haya ya propaganda zisizo makini yanatia hasira sana si kwa watanzania wa Mtwara tu hata kwa watanzania wa maeneo mengine.

Yaani kupigwa mabomu, kuvunjiwa mali zao,kuibiwa malizao...na baadhi ya vyombo vya usalama kwa siku hizi mbili tatu ndizo zimewaelimisha watanzania wa Mtwara faida za kusafirisha gesi kwenda Bagamoyo...kweli..!!!?
 
Mbona CCM hawazungungumzii sera na sheria itakayoongoza uvunaji wa gesi. wanakazana gas itoke mtwara, waende mtwara wakae na wananchi waandae sera shirikishi then waende waandae muswada wapeleke bungeni.

mbona hiyo mikataba imewekwa siri kwanini hawaiweki wazi?? kama ni kwa maslahi ta taifa ??
 
Gazeti la Jambo leo ni chombo cha propaganda za CCM na serikali.
Bora gazeti la Uhuru kuliko jambo leo.
Hata vitumbua halifai kufungia.
Linafaa kutumika chooni tu.

Mhariri mkuu wa Jamba leo amesoma Tumaini University Iringa, njaa tupu yule dogo.
 
Back
Top Bottom