Serikali haipangi bei ya kuuza korosho; Chicago Mercantile Exchange ndio bei za bidhaa za nafaka zinapopangwa kutegemea wazalishaji na walaji; unapiga kelele kujifanya unatetea wamakonde kumbe ni unafiki wenu hata korosho zenyewe hununui kuboresha soko la ndani ; kaa ukijua gesi itatoka tu bila wasiwasi wowote; vipi ajira Tanzania Daima imejipa?
Chama
Gongo la mboto DSM
Mkuu.
Naomba nianze na angalizo maana kwenye ule mjadala wa Prof J ulijivua ufahamu na kuporomosha matusi. Ukitaka mjadala na mimi ujifunze kujadili kwa kutumia lugha za staha na kistaarabu, tunasomwa na wadogo zetu na wakubwa wetu walio tuzidi umri humu.
1. Umesema "Chicago Mercantile Exchange ndio mahali ambapo bei za nafaka zina pangwa kutegemea wazalishaji na walaji " kauli hii na jibu hili lina mwanya mpana sana kwa sababu sio kweli kwamba bei zote zina pangwa CME kama ulivyo sema na si kweli kwamba hao CME ndio wamepanga na kusema wakulima wa korosho wakopwe na wasilipwe fedha zao kwa wakati.
2. Umesema "napiga kelele kuwatetea wamakonde kumbe ni unafiki na hata korosho zenyewe sinunui". Ninacho kifanya hapa sio kupiga kelele bali natumia haki yangu ya msingi kikatiba kama jinsi ilivvyo ainishwa kwenye ibara ya 18 haki ya uhuru wa mawazo (a) "... Uhuru wa kuwa na maoni na kueleza fikra" usianze kuwa kiranja wa kuelekeza kipi nijadili na kipi nisikijadili.
Lakini pia najadili mambo ya Mtwara kwa kuwa mimi ni Mtanzania na yanayotokea Mtwara yananigusa kijamii, ibara ya 8 (1), (a) inasema ..."Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote na serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi" kwa ibara hii, kama. Serikali ingetambua nafasi ya wananchi wa Mtwara busara za kawaida zina nituma kuamini kuwa hakukupaswa kuwa na vurugu kama serikali ingewashirikisha wana Mtwara ipasavyo. Nayaongea kwa kuwa serikali imeshindwa kutimiza takwa la kikatiba, hili lina onwa na mtu yoyote sio lazima awe mkazi wa Mtwara, sio lazima anunue au asinunue korosho.
Lakini pia ibara hiyohiyo ya 8 Ibara ndogo kifungu (b) na (c) inasema ... " Lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi, na serikali itawajibika kwa wananchi". Kimantiki, kifungu (b) na (c) kinawapa nguvu wananchi kuhakikisha ustawi wa nchi yao na kimsingi nchi inaanza kwenye eneo la kijiografia mahali ulipo, kama hivyo ndivyo wanamtwara wana haki ya kufaidi na madini kamaa jinsi watu walioko kwenye mbuga za wanyama wanavyo faidi raslimali hizo.
Mwisho
Umeongelea ajira Tanzaniadaima. Asante kwa kuonyesha upendo kwangu lakini nasikitika kuwa siko hapa kutafuta ajira, ajira niliyo kuwa nayo inanitosha, tafiti ninazo fanya kule kwenu Kwale wilaya ya mkinga zinanitosha na zimeanza kuonyesha matunda maana fukwe za bahari sasa hazitumiki tena kama vyoo.
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.