Wamefanya uamuzi mzuri. Pongezi kwa wananchi wa Mtwara.
Tunajenga nyumba moja kwanini tugombee fito?
Ila tu tusije rudi huku
Chanzo chetu mkoani Mtwara kilisema; Watu wa Mtwara tumekuwa tukikutana tangu Waziri Mkuu aondoke wiki iliyopita, kwa kweli hatujaridhika kabisa, na tunashangaa mambo aliyokwenda kuzungumza kule Dodoma.
Sisi tulikaa naye, na alipomaliza kazi yake kabla ya kuondoka alitupata ahadi moja tu, ahadi yenyewe alisema anayachukua yote na kuyapeleka kwa Rais ili yapatiwe ufumbuzi.
Lakini kesho yake tunashangaa kusikia kwenye vyombo vya habari kuwa Waziri Mkuu amefanikiwa kuuzima mgogoro wa gesi Mtwara, hili si kweli hata kidogo na Serikali wanafahamu.
Lakini pamoja na yote hayo, tuliposikia Bunge linaunda kamati kuja Mtwara kuchunguza mgogoro huu, hapo tukawa na matumaini kwamba wawakilishi wanakuja, ili tuwaeleze ni nini hasa tunakitaka.
Lakini baadae tena tunasikia hiyo kamati haiji tena Mtwara kwa sababu mgogoro umekwisha. Baada ya kusikia hivyo basi tukajua kuna kitu kilishakusudiwa tangu awali, kwa hiyo kitabaki kama kilivyo.
Kwa hiyo sisi tutaendelea kudai haki yetu mpaka pale tutakaporidhika kwamba haki yetu itabaki hapa Mtwara na kutunufaisha kwanza, na katika hili hatutaki siasa wala maneno matamu.
Wakati hali ikiwa hivyo, taarifa zaidi zinasema kuwa, idadi ya polisi mitaani na hata wale wa usalama barabarani imepungua kwa kiasi kikubwa kutokana na hali ya usalama kuwa tete.
Mtu yoyote akija Mtwara atajionea mwenyewe, idadi ya polisi barabarani imepungua sana, hata watu wanaokwenda polisi kwa ajili ya kuripoti matukio madogo kama ya wapenzi kupigana kwa sasa hawasikilizwi.
Polisi wanajaribu sana kuepuka kutengeneza mazingira yanayoweza kusababisha vurugu, hii ndio hali halisi ya Mtwara na maeneo ya jirani, alisema mtoa habari wetu.
Akizungumzia hali hiyo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara (RPC), Maria Nzuki, alisema Jeshi la Polisi mkoani humo mpaka jana lilikuwa halina taarifa zozote kuhusiana na maandalizi ya maandamano hayo.
RPC Nzuki alisema; Sisi hatuna taarifa za maandamo hayo ya tarehe 10, lakini kwa sababu tumeulizwa, basi kama polisi tutazifanyia kazi mara moja taarifa hizo.
Kuhusu askari polisi kutoonekana barabarani, si kweli, askari wapo, isipokuwa kwenye vituo vidogo hawapo kwa sababu vilichomwa moto. Tunasubiri hali ya usalama itakapotengemaa, basi watarejea.
Baada ya kutokea kwa machafuko makubwa mjini Mtwara Desemba 27, 2012, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alikwenda mjini humo, ambapo pamoja na mambo mengine alizungumza na viongozi wa makundi mbalimbali ya kijamii, kisiasa na Serikali.
Baada ya ziara yake hiyo, aliporejea mjini Dodoma alizungumza na vyombo vya habari na kusema moja ya mambo yaliyoamsha hisia za wakazi wa Mkoa wa Mtwara hadi kushinikiza kwa vurugu wakitaka gesi isitoke mkoani humo, ni taarifa kuwa nishati hiyo ingepelekwa wilayani Bagamoyo, nyumbani kwao Rais Jakaya Kikwete.
Pinda alisema mbali na imani hiyo, alibaini kuwapo mpasuko ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mtwara, na harakati za kisiasa ni sababu nyingine iliyochochea mgogoro huo.
Sasa hili nililitolea ufafanuzi kwa kukanusha kuwa si kweli kwamba gesi inakwenda Bagamoyo. Lakini pia baada ya kukaa nao nilibaini kuwa hata viongozi wenyewe wa CCM hawako pamoja.
Pamoja na hayo nikachukua maelezo kuhusu matatizo yao mengine na nikawaahidi kwamba nitayafikisha katika mamlaka husika, ili waweze kuona namna ya kufanya.
Madai kwamba gesi hiyo inapelekwa Bagamoyo yalikuwa moja ya ujumbe mkuu uliokuwa umeandikwa kwenye baadhi ya mabango wakati wa maandamano hayo ambayo yalidaiwa kuratibiwa na baadhi ya vyama vya siasa.
Pinda alisema viongozi wa kisiasa mkoani Mtwara wakiwamo wabunge, wameonekana kuwa na mpasuko unaosababisha uchochezi kwa makundi ya watu.