Jamani waungwana niokoeni

Jamani waungwana niokoeni

Bhozo

Member
Joined
Feb 23, 2013
Posts
8
Reaction score
0
JF naikubali, ni kisima cha elimu, uzoefu na maarifa ya kila aina, isitoshe kuna waungwana kibao. Mwenzenu nimekwama, naombeni waungwana mnisaidie. Biashara zangu zimesimama kwa kukosa mtaji. Nimejaribu kutafuta mkopo benk zote ninazoenda sikidhi masharti yao. Nimejaribu kuuza kiwanja changu hadi sasa sijapata mteja yeyote, kazini utaratibu umebadilika mikataba inasainiwa mwezi May ndo tuanze kulipwa mishahara. Yamenikuta mwenzenu dunia naiona imesimama!

Naombeni msaada wenu waungwana wa mkopo sh. mil. mbili hata kama ni kwa riba niendeleze biashara zangu nitarudisha ndani ya mwaka 1 kidogo kidogo. Au yeyote anayeweza kununua kiwanja changu anakaribishwa sana ili nimalize tatizo hili linalonikabili. Shukrani sana kwa waungwana wote.
 
Details za Kiwanja please!!

Kiwanja kipo Chanika mwisho, ni kikubwa robo eka, umeme upo, bei mil. 13 inapungua na unaweza lipa kidogo kidogo kutegemeana na uwezo wako, lengo ni kusupport biashara zangu wakati nikiisubiri May.
 
pole sana.naelewa na maisha haya sometimes ukikwana,unaiona dunia haikutendei haki.kwa nini usingejaribu biashara za mtaji mdogo,ikakusaidia kujikwamua matatizo madogo madogo.
 
JF naikubali, ni kisima cha elimu, uzoefu na maarifa ya kila aina, isitoshe kuna waungwana kibao. Mwenzenu nimekwama, naombeni waungwana mnisaidie. Biashara zangu zimesimama kwa kukosa mtaji. Nimejaribu kutafuta mkopo benk zote ninazoenda sikidhi masharti yao. Nimejaribu kuuza kiwanja changu hadi sasa sijapata mteja yeyote, kazini utaratibu umebadilika mikataba inasainiwa mwezi May ndo tuanze kulipwa mishahara. Yamenikuta mwenzenu dunia naiona imesimama!
Naombeni msaada wenu waungwana wa mkopo sh. mil. mbili hata kama ni kwa riba niendeleze biashara zangu nitarudisha ndani ya mwaka 1 kidogo kidogo. Au yeyote anayeweza kununua kiwanja changu anakaribishwa sana ili nimalize tatizo hili linalonikabili. Shukrani sana kwa waungwana wote.

Mkuu kwanza pole, pili usipende kuandika kwa kulialia namna hii, unapoonesha dhahili kwamba umefikwa na maji ya shingo unawapa advantage ya kukuchinjia baharini hao unaotaka "wakusaidie"! Kikubwa wewe ni kwamba una biashara zako zitaje ziko wapi na zinaendeleaje ili uvutie mtu kuwekeza kwenye hizo biashara akiwa na hakika kuwa pesa yake itarudi, ukiona mkopeshaji anafurahia kuuza dhamana aliyoweka mteja ujue huyo ni mwizi. Hayo unayopitia ni mapito tu mkuu, komaa. BTW, hiyo kampuni isiyolipa mishahara mpaka wasaini mikataba kwa miezi minne ni kampuni gani?!!! Kuna watu ambao ukiwaona sasa ukaambiwa wamepitia mazito kuliko hivyo vijichangamoto vyako huwezi amini, usilie sana bana, wewe unaaford mpaka kulipia bundle ya kuingia JF!
 
pole sana.naelewa na maisha haya sometimes ukikwana,unaiona dunia haikutendei haki.kwa nini usingejaribu biashara za mtaji mdogo,ikakusaidia kujikwamua matatizo madogo madogo.

Asante sana. Biashara nilizonazo pia ni za mtaji mdogo na huwa ninaziendesha kwa kutegemea support kubwa toka kwenye ajira yangu. Mabadiliko makubwa kazini ndo yameharibu.
 
Mkuu kwanza pole, pili usipende kuandika kwa kulialia namna hii, unapoonesha dhahili kwamba umefikwa na maji ya shingo unawapa advantage ya kukuchinjia baharini hao unaotaka "wakusaidie"! Kikubwa wewe ni kwamba una biashara zako zitaje ziko wapi na zinaendeleaje ili uvutie mtu kuwekeza kwenye hizo biashara akiwa na hakika kuwa pesa yake itarudi, ukiona mkopeshaji anafurahia kuuza dhamana aliyoweka mteja ujue huyo ni mwizi. Hayo unayopitia ni mapito tu mkuu, komaa. BTW, hiyo kampuni isiyolipa mishahara mpaka wasaini mikataba kwa miezi minne ni kampuni gani?!!! Kuna watu ambao ukiwaona sasa ukaambiwa wamepitia mazito kuliko hivyo vijichangamoto vyako huwezi amini, usilie sana bana, wewe unaaford mpaka kulipia bundle ya kuingia JF!

Nashukuru sana kwa ushauri. Nafanya kazi kwenye taasisi ambayo inategemea zaidi funding toka kwa wahisani nje ambapo kila mwanzoni mwa mwaka process ya utumaji budget huwa ndefu ingawa huwa tunalipwa malimbikizo. Thanks kwa kunitia moyo.
 
Back
Top Bottom