Jamani wanaume wasomi mna nini?

Jamani wanaume wasomi mna nini?

Dah
I feel sorry for the lady.....arudi shule tu.hapo bado watu watamshauri avumilie. ..
Mie sipendi dharau
 
PHD ndo nn?nan alomwambia kwenye mapenzi kuna hayo masuala,nina wasiwasi na uwezo wake wa kufikiri hapo anachanganya maisha ya ndoa na elimu,kama ameamua kuoa tena alijua kiwango cha elimu cha aliyemuoa huo ni ulimbukeni akasome sociology huko!
 
huyo tu mshenzi hata asingesoma kuna waliosoma maprofesa na hawako hvyooo
tabia ni km ngozi haibadiliki kwa msomi na asiye msomi
ila pole yake huyo dada cha msingi asimame ktk maombi
kingine ajiangalie sana may be anajisahau sana ktk mambo yake
 
Sio kweli,kaka zangu wakubwa wawili wana phd na ndugu zangu wengine kadhaa wana master na wake zao ni form four lakini wanaishi nao vizuri. Hiyo case study yako isikupelekee kutoa hukumu kwa wanaume wasomi wote. Hiyo ni tabia ya hao uliokutana nao sio wanaume wote wasomi wako hivyo.
 
Hebu kwanza twende trtibu, kwo huyo jamaa ni wapi, ni kule tunaendaga kwa kuvuka maji baridi?!! maana msikae mnasingizia watu wenye elimu za juu kwa sample ya wajinga wawili! btw, hivi kwa nini wanawake wengi wenye elimu kubwa wameolewa na kuachika?..na wengine wameachika kimyakimya bado wanatumia majina ya waume zao?!
 
Yaani we acha hapa nilipo me mwenyewe natamani nikimbie nifeee....

Wahivi wapooooo



kuna wakina dada wanabahati mbaya wanakutana na wanaume ambao 'selfish' hiyo ni shida mnao...yaani mtu mimi, mimi, hela zangu, mimi nimesoma, magari yangu, mimi utaniambia nini nimesoma..ukidate na mtu wa mmimi, mimi, mimi,mimi kimbia ufe...
 
Aise pole ya huyo dada. Huyo jamaa atakuwa yeye intellectual yake ndio iko low kupita maelezo. Tena nahisi ni mhaya. Ptuu!!
 
yaani kama namuona vile...Hii mbaya sana...wanaume wa hivi wapo wengi, wabinafsi, wanajiona wao ndio wao...Hiyo Elimu yako itakupeleka wapi bila kuwa na upendo kwa mkeo? Jifikirie utaondoka duniani elimu yako haitakusaidia kukuzuia uendelee kuishi....

Unakuta mwanamke kila unachokifanya unaonekana hakifai, ukiongea unaonekana huna point hata kama ni jambo linalohitaji busara lakifamilia...

F--k-- yuuuu...nahasira sana na hawa MANG'AA





Mwidiwee.. Namahorooo wana jf....
Bado Niko najiuliza maswali juu ya wanaume wasomi hasa hasa kuanzia level ya masters, PhD hadi kule kwenye ukuta ulioandikwa elimu tena basi kwanini wengi wao wanakuwa wanatabia ya kupenda kuwadharau wake zao hasa ukikuta wamewapita kiwango cha elimu mfano mke ana kidiploma kake Ka ualimu au kadigrii kake Ka course ya kuchechemea.. Naongea hivi kwa experience cz nimekutana na kesi kama Tatu zenye kufanana lakini hii ya nne too much..
Haya yamemkuta shosty wangu moja hivi mwenye kidigrii chake cha sociology na GPA ya kuchechemea na mchuchu wake mwenye phd ya mambo ya planning.. Sikutaka kuchukua details nyingi cz elimu yake hainisaidii wala kuniletea hela ya ugali
Back to the topic, shosty kipindi kabla hajaolewa mapenzi yamechanua kama maua ya saa nne alikuwa anajisifia kweli na mchuchu wake Mara ooh wanaume waliosoma sana waelewa sana, Mara ooh mi kadegree holder kenzangu nikapeleke wapi, maneno kibao kudharau waume za wenzie na kujifanya Wa kwake ndio bora sana kama tunavyojua masikini akipata masaburi hulia mbwata..sie tena wenye vicertificate holder vyetu tukawa tuna zip our mouth shut tunajipa moyo maisha hayapimwi kwa wingi Wa makaratasi ya vyeti..
Bas bwana Shoga yule mwaka juzi kaolewa kwa shangwe na vigelele na sisi mashabiki kama kawa tupo mbele kumpa kampani, ndoa sasa ina miaka mitatu ndo anaona chungu ya ndoa mkaka kawa na dharau kila analoliongea mkewe sharty liwe prove intelectually with high thinking capacity, akikosea kidogo matusi najuta kukuoa kilaza mkubwa wewe degree yenyewe umeipata kwa bahati, mara mi siwezi kukaa na kujadili maisha na watu ambao sio ma critical thinker, mara asa utanishauri nini wewe na akili yako ndogo na maneno mengine ya maudhi.. Sasa juz ndo ilikuwa komesha shoga kaingiza loss katika biashara ya familia ambayo mkaguzi ni mr.. Alioona junijulai alitukanwa mpaka aliiona ardhi ngumu kuikanyaga kupooza machungu kabaki anatupigia cim mashoga zake kutupa mkasa na maneno ya najuuta kibao nikamwambia shoga vumilia ndo ndoa ilivyo vumilianeni kila mtu ana kasoro zake..
Back to my question: kwani mahusiano yanahitaji akili ya kukariri vitabu?? kama mnaona vitabu ni mali si mngekaa single mkaendelea kukariri.. Najua wengi mko humu wenye hizo tabia Acheni dharau ishini na familia zetu kwa amani, kama mkeo ana weakness mu encourage aweze vile unavyotaka kumnyanyasa kisaikolojia sio vizuri.. Unasababishia makovu moyoni ambayo inawezekana hata we huyajui...
 
yaani kama namuona vile...Hii mbaya sana...wanaume wa hivi wapo wengi, wabinafsi, wanajiona wao ndio wao...Hiyo Elimu yako itakupeleka wapi bila kuwa na upendo kwa mkeo? Jifikirie utaondoka duniani elimu yako haitakusaidia kukuzuia uendelee kuishi....

Unakuta mwanamke kila unachokifanya unaonekana hakifai, ukiongea unaonekana huna point hata kama ni jambo linalohitaji busara lakifamilia...

F--k-- yuuuu...nahasira sana na hawa MANG'AA

Pole sana.sasa wewe unamudu vipi hiyo hali.ushauri wako kwa huyu msociologist
 
junior . Cux mwanamke hapigwi wewe jamani
sa kama amekosea asiambiwe, umeleta hasara kwenye biashara unataka nikubembeleze tena.... hiyo kitu haipo, tusipokuwa wakali mtatupanda kichwani, lazima upige biti ata kidogo!!! Ilitakiwa ampe na vibao hata viwili kabisa sio maneno matupu
 
Last edited by a moderator:
Ndo inavokuwaga msomi akae na msomi mwenzie vinginevy umeliwa! Kuna my ex mmoja ilikuwa nikienda kwao mama yake anamuongelesha ki FRENCH! Makubwaaaaaaa! Basi nangaaaje sharubu! Mpaka nikajifunza cha kiombea maji! Japo kuongea siwezi ila wakinisema naelewa! Loooooooh! Sasa ukute mumeo anawasiliana na mchepuko wake ki English au French wewe umekaa hapo hapo! Hawasemi I love you! Ili ustuke? Thubutuuuuu! Wanasema i adore you! Hahaaaa!
 
Hapo kuna mashaka na hiyo hasara isikute kahonga, ndiyo tatizo la wadada miaka 22 anaolewa na mbaba 39/43 wakat yeye damu inachemka!
 
Jamaa kakosea sana ila alikosea zaidi na zaidi katika kuoa. Kimisingi huyo bwana anapata tabu sana kuishi na mtu ambaye intellectually yuko chini sana kulinganisha na yeye. Kwa mfano katika hali ya kawaida tu unaweza kuacha kujadiliana na mtu kwa kugundua kwamba uwezo wake wa kuchambua mambo ni mdogo au saa nyingine unaweza kuvumilia na kujaribu kujiweka katika level ya huyo mtu. Sasa fikiria kama unapaswa kufanya hivyo kila siku na mtu huyo huyo!!! Ni wazi baada ya kujitahidi kwa miaka 3 kuna mahali itafika lazima ushindwe.

Hii mara nyingi inatokea kwa sababu mwanzo mwanaume anaweza kugubikwa na mapenzi moto moto na pia wanakuwa hawapati muda wa kukaa pamoja kwa muda mrefu. Zaidi mume anaweza kutegemea mke atakua kiakili na kimaarifa lakini kwa bahati mbaya inaweza isiwe hivyo kwa kuwa watu tunatofautiana uwezo. Kuna wengine hata ufanye vipi hawawezi kufika kiwango anachotamani mume. Sasa ukute mume anataka kujadili kuhusu uchumi wa Uingereza, Marekani, Tanzania na Brazil hapo anakuja na habari za GDP, PPP, per capita, FDI na habari za sekta za dhahabu, wese na wenzao, ukigeuka kidogo anataka kuzungumzia import/export tax, custom duties na visa issues. Hujakaa sawa anataka kuongelea U.S foreign policy in the middle east. Kabla hujajikuna vizuri anakuletea habari za investment and planning ukichanganya na expanding and dreaming big. Sasa kama ndoto zako ni kuishi kwenye nyumba ya vyumba vitatu na gari ya kutembelea lazima mambo yatakuzidi kimo sana. Na ukichanganya na tabia ya watz wengi tulivyo wavivu wa kujifunza mambo mapya ndio kabisa lazima uchemshe. Ndo hapo sasa mume anakuona kilaza bab kubwa. Lazima nyumba uione chungu.

Ila hata hivyo mimi huwa naona watu wanalazimisha mambo. Kuna siku niliwahi kusema maisha yanaweza kuwa magumu sana kama badala ya kutafuta mke unatafuta business partner. Inapofikia mahali huyo mke akashindwa kuwa business partner inakuwa shida kubwa sana.

Inabidi ifike mahali watu kama huyo jamaa inabidi wajue kuwa mke ni mke tu. Kuna majukumu yake kama mke kama anayaweza hayo basi inatosha. Ikitokea akaweza kusimamia na mambo mengine nje ya yale ya msingi na wajibu basi ni vizuri lakini kama hawezi basi si budi kumlazimisha asichokiweza.

Utakuwa hujaeleimika kama utataka kuongea mambo ya bond cleaving na mtu wa historia au utake kumuambia mambo ya meli kuelea mtu wa anthropology by the way hujaoa mke ili uzungumze naye ma GDP na vitu kama hivyo!!!!

Tukiamua kuoa basi tukubali hizo tofauti zetu, hivi we ukiwa na PhD mkeo mpishi kila uchao akuletee stori za recipes mpya utaona sawa!!!

Tuzungumze yenye kuhusu familia zetu na hao tuliowaoa italeta amani na upendo na penzi shirikishi!!!
 
kuna kitu hamjajua ni bora uoe mwanamke asiyesoma kabisaaaaaaaaaaa!!!!! kuliko aliyefika digrii huwa wana maudhi sana kidigrii chake anataka ukanyenyekeee hata mimi nakunyanyasa sasa wewe una degree halafu unaongea utumbo peleka kuleeeee!!!!!!!!!
 
Mwidiwee.. Namahorooo wana jf....
Bado Niko najiuliza maswali juu ya wanaume wasomi hasa hasa kuanzia level ya masters, PhD hadi kule kwenye ukuta ulioandikwa elimu tena basi kwanini wengi wao wanakuwa wanatabia ya kupenda kuwadharau wake zao hasa ukikuta wamewapita kiwango cha elimu mfano mke ana kidiploma kake Ka ualimu au kadigrii kake Ka course ya kuchechemea.. Naongea hivi kwa experience cz nimekutana na kesi kama Tatu zenye kufanana lakini hii ya nne too much..
Haya yamemkuta shosty wangu moja hivi mwenye kidigrii chake cha sociology na GPA ya kuchechemea na mchuchu wake mwenye phd ya mambo ya planning.. Sikutaka kuchukua details nyingi cz elimu yake hainisaidii wala kuniletea hela ya ugali
Back to the topic, shosty kipindi kabla hajaolewa mapenzi yamechanua kama maua ya saa nne alikuwa anajisifia kweli na mchuchu wake Mara ooh wanaume waliosoma sana waelewa sana, Mara ooh mi kadegree holder kenzangu nikapeleke wapi, maneno kibao kudharau waume za wenzie na kujifanya Wa kwake ndio bora sana kama tunavyojua masikini akipata masaburi hulia mbwata..sie tena wenye vicertificate holder vyetu tukawa tuna zip our mouth shut tunajipa moyo maisha hayapimwi kwa wingi Wa makaratasi ya vyeti..
Bas bwana Shoga yule mwaka juzi kaolewa kwa shangwe na vigelele na sisi mashabiki kama kawa tupo mbele kumpa kampani, ndoa sasa ina miaka mitatu ndo anaona chungu ya ndoa mkaka kawa na dharau kila analoliongea mkewe sharty liwe prove intelectually with high thinking capacity, akikosea kidogo matusi najuta kukuoa kilaza mkubwa wewe degree yenyewe umeipata kwa bahati, mara mi siwezi kukaa na kujadili maisha na watu ambao sio ma critical thinker, mara asa utanishauri nini wewe na akili yako ndogo na maneno mengine ya maudhi.. Sasa juz ndo ilikuwa komesha shoga kaingiza loss katika biashara ya familia ambayo mkaguzi ni mr.. Alioona junijulai alitukanwa mpaka aliiona ardhi ngumu kuikanyaga kupooza machungu kabaki anatupigia cim mashoga zake kutupa mkasa na maneno ya najuuta kibao nikamwambia shoga vumilia ndo ndoa ilivyo vumilianeni kila mtu ana kasoro zake..
Back to my question: kwani mahusiano yanahitaji akili ya kukariri vitabu?? kama mnaona vitabu ni mali si mngekaa single mkaendelea kukariri.. Najua wengi mko humu wenye hizo tabia Acheni dharau ishini na familia zetu kwa amani, kama mkeo ana weakness mu encourage aweze vile unavyotaka kumnyanyasa kisaikolojia sio vizuri.. Unasababishia makovu moyoni ambayo inawezekana hata we huyajui...


Huyo jamaa sijui kama sio akina Ruta, na sio usomi unaomfanya awe na dharau ni tabia yake na upumbavu wake, wasomi wangapi hawana dharau za aina hiyo, wasomi sasahivi wanaongoza kucheza na watoto wao jioni, mwanaume anaeongelea elimu kutwa kucha sio mwanaume ila mwalimu wa shule
 
Back
Top Bottom