kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,940
- 7,847
Eti wanakuwekea games bila ya ridhaa yako kwa shs 500 kama hupendi ndio wewe utume neno UNSUB kwenye namba 15362. Cha ajabu licha ya usumbufu ukituma huo ujumbe message haiendi. Hii ni mara ya pili kwangu kipindi cha wiki mbili. Sasa jamani huu ukoloni na ufisadi wa simu za mkononi tufanyeje wandugu? Simu yako,..licha ya kusumbuliwa kwa simu yako kugeuzwa ubao wa matangazo bila kulipwa chochote pia unanyang'anywa hela yako. Huu kama sio ujambazi ni nini? TCRA tafadhali fanyeni kazi yenu wananchi sasa tumechoka na hii kero.