Jamani tujikumbushe vitabu vya o'level vya fasihi

Mr Penal Code

JF-Expert Member
Jul 9, 2012
823
213
hebu tujikumbushe vitabu vya fasihi ambavyo tumesoma o'level na Mhusika Gan ulikuwa unampenda zaidi.
 
Ngoswe penzi kitovu cha uzembe mhusika niliyekuwa nampenda ni Ngoswe na binti mazoea.
 
Elimu mitaani kulikuwa na riwaya ya Harakati za Pimbi, stelingi alikuwa ni Dr. Love Pimbi

usiwasahau na kina Obi...Linda....Zumo na Mayuku.....
pia riwaya kama...usiku wa balaa....Dar es Salaam usiku....Njama....Tutarudi na roho zetu....Kiruka njia.....Rosa Mistika.....
Niendelee......?
 
Rosa Mystica cha Ezekiel Kezilahabi.
Kilikuwepo home, niko darasa la 1 au la 2, nikakutwa na mama nakisoma, akaninyang'anya, akakificha, akasema hd nikikuwa ndo nitakisoma.
Nilipokuwa sec, ndo nikakisoma, nikatambua why nilinyang'anywa kipind kile.
 
Kwenye Sani, kuna riwaya ya Maji Mazito ya hayati Said Mbwana Makaja Bawji,
pia kulikuwa na mtu anaitwa RAMOZA(Rashid Mohamed Zahor) anapika riwaya kwenye gazeti la kiongozi.
 
Rosa Mystica cha Ezekiel Kezilahabi.
Kilikuwepo home, niko darasa la 1 au la 2, nikakutwa na mama nakisoma, akaninyang'anya, akakificha, akasema hd nikikuwa ndo nitakisoma.
Nilipokuwa sec, ndo nikakisoma, nikatambua why nilinyang'anywa kipind kile.

Kuna hii: 'Dunia uwanja wa fujo' ya huyo Mkerewe, Ephraim Kezilahabi, mama yako angekukuta na hii, ungekula bakora nyingi!
 
Back
Top Bottom