Kuliko usumbufu tunaoupata napendekeza vibao viwekwe Kama nchi za wenzetu across the road na kwenye mwisho WA katazo ili iwe rahisi Mtu kuona . Kwani sasa hivi ni full kabambikizanaNdio michezo yao hao jamaa; siku hizi wanalazimisha utoe hela kwa nguvu. Sheria ibadilishwe TANROADS iwajibike pale ambapo max speed ni kiwango fulani basi vibao viwekwe mfululizo umbali usiozidi mita 100 kila kibao ili kutoa msisitizo.
Kuna kakijiji fulani hapo unakaribia kuimaliza Pwani kuingia Tanga; kibao cha 50 na cha kuifuta 50 viko umbali wa zaidi ya km. 5; yaani hapo matrafiki wanapapenda kuliko eneo lolote Tanzania. Kakibanda kao ka nyasi (upande wa kulia kama unaenda Segera) kametegeshwa mahali ambapo huwezi kuona kibao cha upande wowote na ni lazima uingie mkenge tu. Huu ujanja ujanja wa kitoto ufike mwisho kama ni hela sio kwa utaratibu huo.
Imenitokea leo hapo mombo kwa mbele kma unakuja dar yani kaniambia nimepita mombo na 62 speed,nimepita mvua inanyesha kubwa halafu nlikua chini ya 50Wakuu, juzi nilisafiri kwa gari binafsi toka Moshi kuja Dar es salaam. Nilikuwa mwangalifu sana na speed limit hasa zile za 50.
Nilipofika Mombo nikasimamishwa na Trafiki wakasema kuna eneo lenye speed limit ya hamsini eti nilipita kwa speed 62/saa. Nikawaeleza kuwa sijavuka spidi hiyo kwenye kibao chochote tangu nitoke Moshi.
Eti wakanionyesha picha gari yangu waliyotumiwa na mmoja wao (nadhani atakuwa alijificha porini na speed camera) nikawambia hio sio conclusive evidence kuwa nilikuwa katika eneo la kwenda spidi 50 kwa vile hakuna ushahidi kuwa nilikuwa ndani ya eneo lenye spidi limit.
Hakuna picha ya kibao chochote kinachoonyesha gari langu lilikuwa katika eneo hilo. Walichoniambia hao trafiki eti kama nina shaka basi wanipeleke Mahakamani. Nikawaambia twendeni na mthibitishe kuwa kweli nilikuwa katika range ya 50km/hr na mkishindwa mtanilipa fidia za usumbufu.
Baada ya malumbano wakanirudishia Driving licence yangu wakaniambia we jamaa mbishi sana.
Nilichojifunza ni kuwa hawa trafiki wanapiga picha popote tu wanarushiana ili watengeneze malipo. Kwa kweli kuna maonezi makubwa sana barabarani. Wana JF wenzangu nimeona niwashirikishe katika hili tusikie na tusikie experience za wengine waliokumbwa na masaibu haya
Ipi hyo mkuuMimi ninayo ile app ya kujua cameta ziko wapi. Cha kushangaza unaweza kuwa unaendesha gari polini kabisa na hakuna kibao cha 50 lkn utasikia simu ina toa alarm na kukujulisha kuwa kuna camera. Huo ni uthibitisho kuwa hela inatafutwa kwa lazima. Huu utaratibu wa kurusha picha ni mbovu hakuna mfano
Ipi hyo mkuu
Jina asee maana haya mambo mazrmazr sio ya kuwa nayo mwenyewe
Wakuu, juzi nilisafiri kwa gari binafsi toka Moshi kuja Dar es salaam. Nilikuwa mwangalifu sana na speed limit hasa zile za 50.
Nilipofika Mombo nikasimamishwa na Trafiki wakasema kuna eneo lenye speed limit ya hamsini eti nilipita kwa speed 62/saa. Nikawaeleza kuwa sijavuka spidi hiyo kwenye kibao chochote tangu nitoke Moshi.
Eti wakanionyesha picha gari yangu waliyotumiwa na mmoja wao (nadhani atakuwa alijificha porini na speed camera) nikawambia hio sio conclusive evidence kuwa nilikuwa katika eneo la kwenda spidi 50 kwa vile hakuna ushahidi kuwa nilikuwa ndani ya eneo lenye spidi limit.
Hakuna picha ya kibao chochote kinachoonyesha gari langu lilikuwa katika eneo hilo. Walichoniambia hao trafiki eti kama nina shaka basi wanipeleke Mahakamani. Nikawaambia twendeni na mthibitishe kuwa kweli nilikuwa katika range ya 50km/hr na mkishindwa mtanilipa fidia za usumbufu.
Baada ya malumbano wakanirudishia Driving licence yangu wakaniambia we jamaa mbishi sana.
Nilichojifunza ni kuwa hawa trafiki wanapiga picha popote tu wanarushiana ili watengeneze malipo. Kwa kweli kuna maonezi makubwa sana barabarani. Wana JF wenzangu nimeona niwashirikishe katika hili tusikie na tusikie experience za wengine waliokumbwa na masaibu haya