jamani nyie wanaume

jamani nyie wanaume

G3T

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2013
Posts
816
Reaction score
400
Habari wana MMU,mimi ni msichana mwenye kazi yangu ya kuniingizia kipato kidogo, na elimu ya kawaida.Kikubwa ambacho kinaniuma sana mpaka naandika huku nalia,Nina BF wangu ambaye aliamishwa kikazi mkoa mwingine na baaadae akanitafutia kazi huko aliko na kuanza kuishi nae(kwa kweli sikuwa napenda kuishi nae bila ndoa).Miaka mitatu sasa imepita,ila jamaa sijawahi kumsikia hata siku moja kudokezea jambo la kwenda kujitambulisha kwetu.Chakushangaza sasa nikimwambia kuhusu swala la kwenda kwetu daaaah!anachonijibu sidhani kama ntakuja kukuoa wewe na ukae ukijua kwamba ukiamua ondoka au ubaki nikufuje tu,ila swala la mimi kwenda kwenu sahau.

nashindwa kuendele jamani,
 
Mydear unashindwaje kuelewa na ashakueka wazi kua hana time na yuko kwa ajili ya kukufuja tu,,...achana nae tupa kuleeeeeeeee,,.....LIFE goes on
 
Heeeeeeeee sasa unasubiri nini? bora yeye kasema ukweli mbele yako kuna mwingine anakupiga danadana tu kuwa nitaenda nitaenda miaka inaenda. Bidada hata nashindwa nikwambieje maana jibu unalo ngoja waje wengine tuone.
 
^^
Hivi jamani leo nimepata utata,,hii post ya pili sasa,,UBOYFRIEND unaisha lini?
Miaka 3 unaishi nae bado unamwita boyfriend?
If that the case,,inaweza kuwa sababu ya yeye kutofunga ndoa na wewe!
3yrs tunaishi wote,,bado uniite boyfriend? Maanake akija mwingine akatangaza ndoa basi huyo ni mume?
^^
 
Ukiona manyoya????...

wala si manyoya; umeambiwa black and white halafu unauliza ufanyaje. No wonder ameamua kukuacha kama unashindwa kufanya maamuzi kwa kitu straight kama hiki then hata familia huwezi endesha.
Kifupi kwa kukaa na wewe hiyo miaka 3 amegundua mapungufu yako ya kuzidi ambayo ni pamoja na akili za kushikiwa. Endelea ku'fujwa' kama alivyokuambia.
 
Mama utukome wanaume kabisaaaaaa. Tatizo hapa siyo wanaume bali ni huyo BF wako na hasa wewe ambaye umeamua kwa hiari yako kumpelekea huduma zote za mke bila kwanza kuingia naye mkataba wa ndoa.Mbaya zaidi yeye keshakwambia kuwa anakufuja tu na hana mpango wa kukuoa halafu bado unaendelea kumuinulia sketi na kumpanulia .......... afuje anavyotaka. Wacha niishie hapa nisije nikaongea mambo mazito mbele ya watoto kinyume na maadili yetu ya kule ninakotoka.
 
Dah Kaunga ulivyoandika utafikiri unanijibu mie tena...ebu muelekeze huyo bidada hapo juu...mi nilimsaidia tu kwamba akiona manyoya ajue keshaliwa
 
Last edited by a moderator:
On the first place kosa ulilofanya ni kukubali kuishi na kidume under one roof for good 3yrs bila ndoa

Mazoea ni kitu kibaya sana inshort amekutumia amekuzoea na mwisho amekukifu,sikushauri hata kidogo eti uendelee kukaa nae kuweka mambo sawa

Fungasha virago vyako kimbia na ukaanze upya from scratch na usilirudie tena hilo kosa, pengine kukaa nae distance kwa mda anaweza kumiss the good side of u akakurudia na pindi akifanya hivyo ndio mda wa kumpa direction ya nyumbani kwenu kabla ya yote....asiporudi organize urslf with time atakuja mwingine ila uwe na msimamo,,,,DON'T BE "YES" WOMEN ALL THE TIME
 
Acha kuwa king'ang'a hutakiwi hapo bibie....
jamaa kishakuambia ukweli, wala halihitaji ushauri hili,
 
fungasha kilicho chako nenda mwana kwenda kwenu
 
Sasa unasubiri nini? Una taarifa zote, ni wewe tu kufanya maamuzi.

Ila kama uko content na kuishi naye hivyo mlivyo usilie, maana kakuambia lake la moyoni.
 
kwa mujibu wa sheria mkiishi pamoja kwa muda wa miezi 3 nyie ni mume na mke,ila ndoa hailazimishi ukilazimisha utateseka.na sio wanaume ndio tulivyo co wote ila usilazimishe tulia utapata atakae kuja kujitambulisha.
 
Habari wana MMU,mimi ni msichana mwenye kazi yangu ya kuniingizia kipato kidogo, na elimu ya kawaida.Kikubwa ambacho kinaniuma sana mpaka naandika huku nalia,Nina BF wangu ambaye aliamishwa kikazi mkoa mwingine na baaadae akanitafutia kazi huko aliko na kuanza kuishi nae(kwa kweli sikuwa napenda kuishi nae bila ndoa).Miaka mitatu sasa imepita,ila jamaa sijawahi kumsikia hata siku moja kudokezea jambo la kwenda kujitambulisha kwetu.Chakushangaza sasa nikimwambia kuhusu swala la kwenda kwetu daaaah!anachonijibu sidhani kama ntakuja kukuoa wewe na ukae ukijua kwamba ukiamua ondoka au ubaki nikufuje tu,ila swala la mimi kwenda kwenu sahau.

nashindwa kuendele jamani,

Achana nae. Maisha lazima yaendelee. Kwanini unalazimisha ndo? Ndo hailazimishwi. Huyo ukimlazimisha kukuoa atakunyanyasa sana na ndoa utaiona chungu!
 
Una bahati sana umeelezwa ukweli cha maana fanya maamuzi ya kuondoka hapo ukatafute ustaarabu mwingine..!
 
Dah Kaunga ulivyoandika utafikiri unanijibu mie tena...ebu muelekeze huyo bidada hapo juu...mi nilimsaidia tu kwamba akiona manyoya ajue keshaliwa

Aisee nisamehe, hasira got better of me hadi nikaflow tu bila kufikiria kuwa nimekuqoute wewe.
 
my dia..inauma lakini kaa ukijua kua hauna chako hapo..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom