Jamani nina pepo la kukataliwa

Jamani nina pepo la kukataliwa

kijana mkimya

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2015
Posts
277
Reaction score
121
Hii hali inanihuzunisha sana. mwaka wa tatu sasa nataka kuoa lakini inashindikana.

Kama sijapata kikwazo toka kwa wazai basi nitapata kwa binti.

Mara nne nilikuwa nimemaliza process zote za kufanya harusi lakini siku ya harusi mabinti wanakuwa wanakimbia.

Harusi inaahirishwa na hapo ndo unakuwa mwisho. mara nyingine wazazi wa binti wanakuwa hawakupendezwa na mimi.

Mara nyingine wazazi wanakubali ila binti anakuwa hanipendi.

Sasa wakuu sasa nimetokea kumpenda mdogo wa rafiki yangu, nimemueleza hisia zangu lakini hajanijibu chochote yapata wiki sasa.

Inafikia kipindi nakata tamaa nahisi ni yaleyale ya kukataliwa.

Mimi ni kijana wa dini ninamaisha yangu japo sio tajiri lakini nina maisha ambayo watu wengi wanayatamani.

Wakuu nifanye nini? Sasa nimepoteza Imani kabisa.
 
Kwa miaka hakuna mtu mwenye nuksi,hawa dada zetu wanataka pesa na wazazi wao!ukigawa hela mkuu Hadi utawakataa,hata ukiwa unakula ugoro wanakula denda na wewe hata harufu haisikii chezea hela wewe!!!!shikamoo hela
 
Kwa miaka hakuna mtu mwenye nuksi,hawa dada zetu wanataka pesa na wazazi wao!ukigawa hela mkuu Hadi utawakataa,hata ukiwa unakula ugoro wanakula denda na wewe hata harufu haisikii chezea hela wewe!!!!shikamoo hela

mkuu mara nne nimetoa mahari yote lakini siku ya harusi wanakimbia. ingekuwa suala la pesa si wangekataa toka mwanzo?
 
Unajipenda,mtanashati,unaenda na wakati na fashion au umekaa kizee,una swagg kweli wewe,unajua kuongea kupanga maneno matamu halafu sio unamtongoza unahisi kakubari tupa ndoano Kwa wengi sio mmoja ukishindwa vyote mwaga pesa tumia helaaaaaa jombaaa uwaone
 
mkuu mara nne nimetoa mahari yote lakini siku ya harusi wanakimbia. ingekuwa suala la pesa si wangekataa toka mwanzo?

Mbali na mahari ulishawahi kumpa mama mkwe hata laki mbili ya mboga,na huyo shemu wetu ulishawahi kumpa laki tano ya kwenda kununulia nguo na saluni?hebu fanya hivyo
 
Unajipenda,mtanashati,unaenda na wakati na fashion au umekaa kizee,una swagg kweli wewe,unajua kuongea kupanga maneno matamu halafu sio unamtongoza unahisi kakubari tupa ndoano Kwa wengi sio mmoja ukishindwa vyote mwaga pesa tumia helaaaaaa jombaaa uwaone

mkuu najipenda, mtanashati na ninakwenda na wakati ila sio kwa kuvaa katakei. isitoshe ni kijana ninaejiheshimu. lakini sijajua nakosea wapi.
 
hii hali inanihuzunisha sana. mwaka wa tatu sasa nataka kuoa lakini inashindikana. kama sijapata kikwazo toka kwa wazai basi nitapata kwa binti. mara nne nilikuwa nimemaliza process zote za kufanya harusi lakini siku ya harusi mabinti wanakuwa wanakimbia, harusi inaahirishwa na hapo ndo unakuwa mwisho. mara nyingine wazazi wa binti wanakuwa hawakupendezwa na mimi. mara nyingine wazazi wanakubali ila binti anakuwa hanipendi. sasa wakuu sasa nimetokea kumpenda mdogo wa rafiki yangu, nimemueleza hisia zangu lakini hajanijibu chochote yapata wiki sasa. inafikia kipindi nakata tamaa nahisi ni yaleyale ya kukataliwa. mi ni kijana wa dini ninamaisha yangu japo sio tajiri lakini nina maisha ambayo watu wengi wanayatamani. wakuu nifanye nini? sasa nimepoteza Imani kabisa.

Dedication ya wimbo:Njoo ufanyiwe maombi by Bon Mwaitege inakuhusu kwa hali yako.
Shetani hapendi furaha yako, kutatua shida yako nenda maombezi kama hutaenda basi anza kujiombea mwenyewe.
 
MUNGU akutie nguvu mr, kuea na imani ya kuwa yote yawezekana kwa Mwenyezi Mungu alie tuumba.
 
Ama kweli LIFE isn't fair, kila mtu na kilio chake. Wengine akina sisi tunamlilia Mungu anichagulie mke mmoja tu sahihi kati ya msululu uliopo, maana nakuwa dilema nichague yupi na niache yupi. Teh teh.

But wengine wanalilia kupendwa hata na mmoja. Daaah dunia hii bhana.

Mleta uzi, relax and wait for your perfect match. Endelea kumtumainia Mwenyezi Mungu!
 
Mbali na mahari ulishawahi kumpa mama mkwe hata laki mbili ya mboga,na huyo shemu wetu ulishawahi kumpa laki tano ya kwenda kununulia nguo na saluni?hebu fanya hivyo

mkuu inawezeka sijawahi kutoa pesa kiasi hiko ila pesa natoa. mi nimfanya biashara nikisafiri narudi na zawadi kila nikisafiri. nawapa wote mama mkwe na mchumba
 
Dedication ya wimbo:Njoo ufanyiwe maombi by Bon Mwaitege inakuhusu kwa hali yako.
Shetani hapendi furaha yako, kutatua shida yako nenda maombezi kama hutaenda basi anza kujiombea mwenyewe.

Dada, hilo jina lako kila napoliona huwa nalifikiria sana mkuu. Teh
 
Usikate tamaa utakuwa kama unamsusia mugu. Zidisha ibada yupo uliyepangiwa
 
naona watu wananishauri aombi tu. shukran kwa ushauri wenu. jamani nimefanya sana maombi. nimekata tamaaa!
 
naona watu wananishauri aombi tu. shukran kwa ushauri wenu. jamani nimefanya sana maombi. nimekata tamaaa!
 
naona watu wananishauri aombi tu. shukran kwa ushauri wenu. jamani nimefanya sana maombi. nimekata tamaaa!

Kama unakata tamaa kwenye maombi?????basi nenda kwa waganga si unataka tukupe ushauri wa kijinga kama huu
 
Back
Top Bottom