Jamani nimefiwa!

pole sana kwa huo msiba. Let him rest in Peace..Mungu alitoa na ametwaa, jina lake lihimidiwe!!! Amen
 
jamani mwenzenu siku ya leo nimepata msiba mkubwa wa kupotelewa na bestman wangu mpendwa. Ameilea ndoa yangu kwa muda wa mwaka mmoja na miezi miwili tu. Nisipotembelea JF kesho mjue kuwa nipo kwenye majonzi majonzi mazito:A S cry:.

Mungu ailaze Roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina

Pole sana kwa msiba huo; mwenyezi mungu aipumzishe pema roho ya marehemu kwa amani. Sote tuko kwenye njia hiyo hiyo.
 
Nawashukuru sana wanaJF wote kwa kutufariji katika kipindi hiki cha majonzi. kwa kweli bestman wangu alikuwa ni bestman wa kila mtu. Kwenye msiba kulijaa watu balaa. Magari ndo usiseme ingawa yeye mwenyewe alikiwa hana hata gari. Alikuwa anajua namna ya kuishi na jamii yake inayomzunguka. Tumempumzisha jana huko Vwawa-Mbozi mkoani Mbeya. Mungu amlaze mahli pema peponi. Amina
 
Back
Top Bottom