Jamani nifanye vipi nisimchukie?

Jamani nifanye vipi nisimchukie?

Nifanye nini na mimi niwe huru sina raha kabisa.. Naona kama bora nisioe tu maana sijui hata huyo mwingine atakuja kwa style gani??
Wala mkuu...huna haja ya kuongea hivyo. She is not worth it at all ...she is not worth your pains ....embu njoo PM kwanza
 
She never was yours to begin with, stop beating yourself up over nothing. The best revenge is to be happy with someone else!
 
Kwa mtu mwenye akili timamu, kwa hili ni rahisi kuachana nae ila kwasababu huna akili ndio maana unapata shida na unashindwa kumsamehe. Maandiko yanasema "azinie na mwanamke hana akili kabisa, afanya jambo litakalomuangamiza. " huko ndiko unakoelekea. Iko hv. Nafsi yako ndiyo iliyojeruhika na imesbabisha maumivu ndani yake. Na nafsi iliyoumizwa inataka kulipa kisasi. Hivyo kabla haujafika hapo tumia hatua ya imani. Isemeshe nfsi yako kwa kuiyenganisha na nafsi ya huyo binti kwakutamka majina yenu. Km ni mkristo tumia damu y Yesu. Ila km sio tumia njia unayoona inafaa kwa mujibu wa imani yako, pia itangaziae uponyaji itapona na utamuona wa kawaida. Hakuna haja yakuwachukia wanawake ni moja kt ya watu wazuri sana, kwa baadhi yako. Usije ukakata tamaaa
Nimekuelewa sana mkuu ngoja nimshirikishe mungu katika hili maana moyo unauma sana
 
Habari za majukumu familia yangu na JF?
Natumaini ni wazima wa afya njema huku mkiendelea na majukumu yenu ya kila siku.

Back to the point
Mwenzenu nlikuwa na mpenzi wangu ambae nilimpenda sana nasema tena nilimpenda sana na nilijua yeye ndo atakuja kuwa mke wangu maana nilimtambulisha mpaka kwa baadhi ya ndugu zangu na yeye pia alinitambulisha kwa baadhi ya ndugu zake.

Mimi nlikuwa nimemtangulia kielimu maana wakati yeye anaenda kuanza chuo (diploma) mimi nlikuwa mwaka wa tatu (degree ) hivyo basi tofauti hizi za kielimu zilitufanya tusiwe karibu kwa muda mwingi maana wakati mimi nipo chuo yeye alikuwa nyumbani.

Tatizo lilianza taratibu baada ya binti kuanza vitabia vya dharau na kuwa busy sana na simu hususani wakati wa usiku. Sikuweza kugundua haraka kinachoendelea ila nilianza tu kuhisi kuna kitu flani sasa hivi kipo kwa huyu binti. Tuliendelea kuwasiliana tu kwa simu japo mawasiliano hayakuwa mazuri sana kama hapo awali.

Baada ya binti kuwa amechaguliwa kujiunga na chuo ilili bidi nisafiri niende kumtembelea hapo chuoni kwao maana ilikuwa ni muda mrefu sana tangu nimuache home akisubiri post za kujiunga na chuo (vyuo vyetu vilikuwa vipi mikoa tofauti)

Nilikaa nae kama siku tatu then nikarudi zangu chuo. Huwezi amini hata wiki moja haijaisha tangu nirudi chuo akanitumia message kuwa kapata mimba hizo siku tatu nilizo kaa nae. Kwa kweli nilishangaa mimba gani ya kugundulika ndani ya wiki moja tu! Nikamwambia asihofu azae tu mtoto atakaa nyumbani then yeye aendelee tu na masomo akakubali ila akasema akae kwanza huko chuoni wakati anafanya utaratibu wa kuwaambia kwao nikasema fresh.

Huwezi amini yule binti kakaa kama wiki moja mbele akasema aliugua kichwa so akaenda kununua dawa alivokunywa tu mimba ikatoka na alilia sana siku hiyo akanipa jukumu la kuanza kumbembeleza kupitia simu. Siku moja nipo class binti akanipigia simu nikamwambia nipo class akanitumia message "tuko nje tuongee jambo serious" kutoka binti ananiambia kuna jamaa anamsumbua na yeye hamtaki eti rafiki zake na yule jamaa wanasema watamdhuru kama hata mkubali rafiki yao akasema ana hofu sana na wale watu so akanipa namba za huyo jamaa alie mkataa.

Basi mi kwa hasira za demu wangu kutishiwa maisha nilimpiga mkwara jamaa nikamwambia ntamuua yeye kabla hajamdhuru demu wangu kiukweli yule jamaa hakunitukana kitu alinambia yule ni demu wake pia ila walikuwa na mgogoro kwanini demu atoe mimba yake.

Na jamaa akanambia kuwa demu alisafiri kwenda kwake na waka kaa wiki mbili pamoja (huyu jamaa anakaa mkoa wa nyumbani kwetu) daaah aisee nilichanganyikiwa ikabidi nimpigie simu rafiki ake mmoja pale chuo nimuulize kama Jessica aliondoka chuoni.

Rafiki yake akanambia ni kweli aliondoka kwa wiki mbili. Roho iliniuma sana kwa mtu niliempenda kujazwa mimba na jamaa mwingine na mbaya zaidi kunisingizia kuwa ni yangu. Ilibidi jamaa nimuonbe msamaa kwa lugha chafu niliyotumia kwake.

Then nikakomaa na binti kumhoji vizuri na baadae akakubali kuwa mimba haikuwa yangu roho iliniuma sana ndo nikaamini watu wengi sana wanaishi na watoto wasio wao kwa kusingiziwa tu. Nikakausha kama wiki mbili baadae nikaanza kuona profile picha yake ya whatsupp anamuweka yule jamaa na mpaka sasa nahisi wako pamoja.

Tatizo langu ni kwamba nimejaribu sana kumsamee huyu kiumbe ili aende zake kwa amani lakini nashindwa. Najikuta natumia muda mwingi kumuwazia vibaya tu. Hata mimi sitaki kuhifadhi chuki juu yake lakini najikuta tu namchukia automatic. Msanii Fd Q anasema "chuki umchoma zaidi anae iifadhi"
Jamani sitaki kuhifadhi chuki naombeni ushauri jinsi ya kumsamee huyu binti ili hata nikimuona niwe na amani tu.

Maana nimeshaanza kuona wanawake ni viumbe hatari sana katika maisha yangu. Mpaka huwa nawaza hata huyo mwingine ntakae kuja kumpata siku akinambia ana mimba yangu sijui nitamwambiaje.. Tukapime DNA au? Maana kusingiziwa mimba nje nje tu.

Ushauri wenu jinsi ya kuondoa hii roho ya kinyongo inanitesa sana
Wala usifanye kinyongo nae jaribu kujiweka busy na mambo mengine, bora umemgundua mapema kua ni msalit kuliko angeyafanya haya katika ndoa ambayo ungekua na watoto kibao wakusingiziwa, pia kila kitu katika maisha kinatokea kwa sababu Fulani jaribu kukaa utulie kama utaanzisha mausiano mapya jaribu kumchunguza MTU ujiridhishe nafikir wako wanawake wanaojitambua na kujielewa na wako ambao hawajatulia sasa kaz kwako, kinyongo hakisaidii sana zaid yakukumiza ww namna yakuondikana na hicho kinyongo ni kufuta namba zake zote na kutowasiliana kabisa na ata akituma msg au kupiga hakuna kurespond lakin IPO cku atakukumbuka mana mkataa pema pabaya panamwita na pia huyo bint hakua anakudhamin ata kidogo huwez kumpa namba boyfriend wako et huyu ananitaka na cmtaki na kanitishia wakat anajua huyo ni mpenz wake, mfano jamaa ulivyomtukana labda mngekua karibu akakuzuru kisa huyo bint, ingekuwaje, bint kuendekeza tamaa unaweza kost maisha ya MTU
 
Pole sana... Uchungu wake hausimikili wala hauna ushauri...

Cha kufanya toka na rafiki yake wa karibu...
 
I know that you are so angry with her, you wish she dies even today but that is not the case mkuu, accept the realty that she did something untold. Acknowledge your anger at her and get comfortable with this then your anger shall perish by itself.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom