Jamani naomba ushauri wako.

Fimbo ya Musa

Member
Jul 21, 2012
94
13
Wanajamvi naomba mnishauri: nimekaa kijiji(home) kwa muda wa mwaka sasa baada ya kumaliza degree yangu ya Accountancy na kutafuta kazi pasipo mafanikio yoyote! Nimeamua kuja Dar kwa lengo la kutafuta kazi. NAOMBENI MNISHAURI NIANZIE WAPI JAMANI kwani wengi wenu ni wazoefu wa jiji hili na mnajua maujanja ya kupata kazi. Asante
 
badili jina au kwenye jina lako ongeza majina kama kikwete, lowassa, mramba, chenge, mwinyi utapata kazi haraka.
 
Muda wa kusubiria mpaka nafasi zitangazwe gazetini zimeshapitwa na wakati!Nenda physically kwenye ofisi uulizie kazi ndugu!
 
Ninachomaanisha ni kwamba kama huna ndugu hasa wenye majina makubwa imekula kwako mwanangu Fimbo ya Musa. Sikuwangii wala kukutania zaidi yakujisika vibaya jinsi vijana wetu wanavyosota bila kazi wakati majambazi wakubwa wakiwapa watoto na jamaa zao tena wasio na elimu ya kutosha.
 
muda wa kusubiria mpaka nafasi zitangazwe gazetini zimeshapitwa na wakati!nenda physically kwenye ofisi uulizie kazi ndugu!

asante sana itegama twi, nakuomba atleast unielekeze office hata chache kwa uzoefu wako ambazo naweza kuziona. Funguka mkuu.
 
ninachomaanisha ni kwamba kama huna ndugu hasa wenye majina makubwa imekula kwako mwanangu fimbo ya musa. Sikuwangii wala kukutania zaidi yakujisika vibaya jinsi vijana wetu wanavyosota bila kazi wakati majambazi wakubwa wakiwapa watoto na jamaa zao tena wasio na elimu ya kutosha.

ok,nimekuelewa father of all, ila naomba uendembele zaidi ya hapo kwa uzoefu wako inijuze chakufanya mkuu
 
asante sana itegama twi, nakuomba atleast unielekeze office hata chache kwa uzoefu wako ambazo naweza kuziona. Funguka mkuu.


Huwezi kuwa serious basi kama hujui hata sehemu ambayo unafit kufanyakazi kwa taaluma uliyonayo! I mean you have to visit all possible areas ambazo unaqualify kuwa mfanyakazi (Hasa ofisi za private),nipo serious kuna jamaa yangu alishawahi kupata kazi kama mzaha tu alikwenda kwenye ofisi fulani kutest zali. Mimi kwa fani yako ya Accountancy siwezi kusema exactly uende wapi maana bahati mbaya taaluma yangu ni tofauti kabisa na yako so sehemu za kutafutia kazi unazijua wewe Mkuu!!
 
huwezi kuwa serious basi kama hujui hata sehemu ambayo unafit kufanyakazi kwa taaluma uliyonayo! I mean you have to visit all possible areas ambazo unaqualify kuwa mfanyakazi (hasa ofisi za private),nipo serious kuna jamaa yangu alishawahi kupata kazi kama mzaha tu alikwenda kwenye ofisi fulani kutest zali. Mimi kwa fani yako ya accountancy siwezi kusema exactly uende wapi maana bahati mbaya taaluma yangu ni tofauti kabisa na yako so sehemu za kutafutia kazi unazijua wewe mkuu!!

nashukuru sana itegamatwi. Ila ukisikia kuna office yoyote kuna opportunity naomba unip.m. Vp kwenye office za usafirishaji/uchukuzi naweza kupata huko?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom