Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
Madaktari wamewatahadhirisha watu wanaobakwa kwamba wakishatendwa hivyo wasioge au kubadili nguo kwa sababu kufanya hivyo kunapoteza ushahidi muhimu wa kumtia hatiani kisheria mbakaji.
Imeelezwa kuwa mtu akibakwa, anapaswa kwenda Polisi haraka kupata fomu namba tatu (PF3) na awahishwe hospitali ya wilaya ambako atapewa matibabu ikiwa ni pamoja na dawa ya kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU).
Dawa ya kuzuia maambukizi ya VVU inayojulikana kama PEP, inaweza kufanya kazi endapo tu mwathirika atapewa ndani ya saa 72 baada ya kubakwa kama kabla ya kubakwa hakuwa na maambukizi.
wasichana na wanawake wengi wanaofika hospitalini baada ya kubakwa na kunajisiwa, huwa wamepoteza ushahidi kwa kuoga na kubadili nguo walizovaa wakati wakibakwa. Wanawake wengi hufika hospitalini wamechelewa na hivyo kuwa katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya VVU.
Kesi nyingi za ubakaji zimekuwa zikikosa ushahidi wa madaktari, kwa sababu aliyebakwa anatakiwa kupelekwa hospitalini akiwa na nguo zake na ‘uchafu', kwa sababu ushahidi wa Polisi na daktari kuwa tendo la ubakaji limefanyika ni nguo alizobakwa nazo mwathirika.
Imeelezwa kuwa mtu akibakwa, anapaswa kwenda Polisi haraka kupata fomu namba tatu (PF3) na awahishwe hospitali ya wilaya ambako atapewa matibabu ikiwa ni pamoja na dawa ya kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU).
Dawa ya kuzuia maambukizi ya VVU inayojulikana kama PEP, inaweza kufanya kazi endapo tu mwathirika atapewa ndani ya saa 72 baada ya kubakwa kama kabla ya kubakwa hakuwa na maambukizi.
wasichana na wanawake wengi wanaofika hospitalini baada ya kubakwa na kunajisiwa, huwa wamepoteza ushahidi kwa kuoga na kubadili nguo walizovaa wakati wakibakwa. Wanawake wengi hufika hospitalini wamechelewa na hivyo kuwa katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya VVU.
Kesi nyingi za ubakaji zimekuwa zikikosa ushahidi wa madaktari, kwa sababu aliyebakwa anatakiwa kupelekwa hospitalini akiwa na nguo zake na ‘uchafu', kwa sababu ushahidi wa Polisi na daktari kuwa tendo la ubakaji limefanyika ni nguo alizobakwa nazo mwathirika.