Jamani mapenzi na chama wapi na wapi?

Jamani mapenzi na chama wapi na wapi?

Hii imemtokea rafiki yangu kipenzi, Jana aliniomba nimsindikize Lenana Hotel jioni akisema kuwa kuna binti kampenda sana sasa anataka amweleze intention yake ya kumuoa, mimi nikamsindikiza, kufika Lenana Hotel baada ya dakika kama 20 binti akafika, ukimwangalia kwa haraka haraka atakuwa na umri wa miaka 21-25 hivi, basi, tukasalimiana pale, mazungumzo ya kuchumbiana yakaanza, kilichonistua zaidi ni hili, katika kuulizana maswali ya hapa na pale mfano, unafanya kazi gani, umri wako, kwenu mpo wangapi, wazazi wako wapo, unasali dhehebu gani, nk. ndipo yule binti akauliza wewe ni chama gani? duuu!! ikabidi nimuwahi kwa kumuuliza swali, chama una maana gani? akasema, Chama cha siasa, Bahati nzuri yule rafiki yangu akasema hana chama ila ni mshabiki wa vyama tu! binti akasema yeye alitaka kufahamu tu!!

Sasa nauliza, hivi siku hizi mkichumbiana ni lazima hili swali umuulize mwenzio? na nafasi ya hili swali katika mahusiano ni ipi?
Mwambie bibie tumemsoma....na gwanda tutamtumia!
 
Sijaona kosa lako kukaa nao kalibu, kwani kipindi hiki watu wanachumbia na kutongozana mbele ya wazazi sembuse we,lafiki tu. Achana na washamba wanao tongezeana kwenye majumba mabovu.

Nimekupa tano kamanda, sasa watu wanataka kura ya siri wengine wazi, wale wanaotaka ya wazi kwa nini wasikubali uwazi katika hili pia la kuchumbiana? rafiki au ndugu yako wa karibu awepo ili na yeye afanye tathimini yake.
 
siku nyingine wape uhuru wenzio..waache peke yao
 
Kuwa na mahusiano na gamba wanasema kwa kitaalam "be in a relationship at your own risk" utapata michepuko kibao, wote ni chakula cha wazee wa Lumumba, akili mgando, wezi,matapeli, hawajui maisha...ptuuuuuuuuuuu.!
 
usikariri maisha! kuna maswali mengi ya

kuuliza ! ulidhani atamuuliza anapenda rangi gani!
 
Mimi ni CCM damu lakini babydoll is Chadema, but we cool. Nikienda kwa shemeji zangu Marangu ni debate mtindo mmoja.
 
Back
Top Bottom