mito
JF-Expert Member
- Jun 20, 2011
- 10,811
- 11,031
Wakuu nimekumbuka enzi hizo nikiwa mdogo mdogo kulikuwa na muvi moja ya kikomando tulikuwa tunaipenda sana (mimi na vijana wenzagu enzi hizo). Stelingi wake tulikuwa tunamwita 'Komando chambo' (ila siyo jina lake halisi). Tulimwita hivyo kwa sababu ktk baadhi ya episodes zake alikuwa anakula chambo (aina fulani hivi ya minyoo - earthworms I think). Sasa kwa sababu ya hii tabia yake ndo tukawa tunamwita Komando chambo.
Naitafuta ili niweze kujikumbusha lakini nashindwa kuipata kwa sababu sijui jina lake halisi wala title yake. Ambaye ana kumbukumbu na hii muvi naomba anifahamishe jina lake niitafute kwa udi na uvumba!!
Naitafuta ili niweze kujikumbusha lakini nashindwa kuipata kwa sababu sijui jina lake halisi wala title yake. Ambaye ana kumbukumbu na hii muvi naomba anifahamishe jina lake niitafute kwa udi na uvumba!!