Jamani hawa wanakera

Jamani hawa wanakera

ligendayika

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2012
Posts
1,183
Reaction score
199
Ukipita katika mitaa mingi ya miji utakuta vijana wameweka computer barazani mwa nyumba, wanaingiza nyimbo kwenye simu na kadhalika. Sasa najiuliza hivi ni lazima kufungulia muziki sauti ya juu kabisa? Kama sivyo mnatukera hivi hamjui kuwa ni sound polution naomba wana JF tujadili hili.
 
Wengi wao ni vilaza hawajui zaidi ya kukopi na kupesti muziki. Inakera lakini ndo ajira zenyewe. Ujasiriamaliza!
 
kwakweli inakera sipati huusiano wa kuwepo nyimbo na sauti kubwa.
 
Wengi wao ni vilaza hawajui zaidi ya kukopi na kupesti muziki. Inakera lakini ndo ajira zenyewe. Ujasiriamaliza!
sawa ni ajira lakini sauti kubwa ni kikwazo kwa wengine,,,,,,nadhani wanapaswa kuweka sauti ndogo ya kumtosheleza yeye na mteja wake.
 
Kama watafungulia kwa sauti ya chini hawatapata wateja au sauti ndo inaleta wateja. Mi nadhani sauti haina uhusiano na wateja
 
matangazo hayo ... hizo Kati ya 60% walee ...
 
Mara nyingi wanakuwa wengi sehemu moja, hivyo kila mmoja anajitaid kuongeza sauti ili asikike. Ila kiujumla inakera...!!
 
Hawa jamaa wananikera sana jamani,mchana kutwa ni kelele kiasi kwamba ukifika home jioni unasikia masikio yanatoa mwangwi wa sauti.ila kuna kitu naomba kuuliza wana JF,Hapa ninapofanyia shughuli zangu kuna kijana anafanya hizo kazi za kuingiza miziki kwenye simu.tangu aanze kazi hii kuna miezi 2.sasa huyu kijana namuna anabadilika siku hadi siku(kuchanganyikiwa)sijajua ni bangi au kuna uhusiano wa kutumia computer na kupiga mziki wa juu zaidi ya masaa 14 kila siku.naomba mwenye kujua hii kitu anisaidie ili nami niweze kumsaidia huyu dogo kabla hajawa "kichaa"kamili.
 
Back
Top Bottom