Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,266
Huyu Daktari alipata madhara makubwa kule Mabwepande na baada ya kunusurika kifo, aliaahidi kuwa atasema kila kitu kuhusu watesi wake.
Kutokana na mateso aliyoyapata daktari huyu, gazeti moja maarufu lilifungiwa kwa kutoa habari za mhuka mkuu wa kadhia hii ambaye lilidai yuko Magogoni.
Sasa huyu daktari amepotea wala haongei tena. Je yuko wapi na je anaendelea na kazi yake ya udaktari au bado anajipanga kutoa taarifa kamili?
Kuna daktari mwenzake mmoja naye alipata madhara makubwa ya kupukutika ngozi na kunyonyoka nywele ambapo alikwenda kuponea India.
Rafiki yake mkubwa aitwae Six akapita sehemu mbali mbali ikiwa ni pamoja na kanisani na kutangaza kuwa rafiki yake amepewa sumu. Dr mwenyewe aliporudi baada ya kunusurika kifo aliaahidi kuwa ataweka mambo hadharani. Wakati anaendelea kutangaza kuwa ataweka mambo hadharani, tukasikia ghafla kapewa uwaziri.
Kuanzia hapo akasitisha matangazo ya kuwa ataeleza kilicho mpata na hivyo kumfanya rafiki yake Six kuonekana ni mnafiki na mwongo mkubwa. Sasa hicho kimya chake kinaeleweka kwani keshapewa fidia.
Sasa rafiki yangu "Dr. Mabwepande" kapewa nini hadi awe kimya namna hii na kusahau ahadi zake?!
Kutokana na mateso aliyoyapata daktari huyu, gazeti moja maarufu lilifungiwa kwa kutoa habari za mhuka mkuu wa kadhia hii ambaye lilidai yuko Magogoni.
Sasa huyu daktari amepotea wala haongei tena. Je yuko wapi na je anaendelea na kazi yake ya udaktari au bado anajipanga kutoa taarifa kamili?
Kuna daktari mwenzake mmoja naye alipata madhara makubwa ya kupukutika ngozi na kunyonyoka nywele ambapo alikwenda kuponea India.
Rafiki yake mkubwa aitwae Six akapita sehemu mbali mbali ikiwa ni pamoja na kanisani na kutangaza kuwa rafiki yake amepewa sumu. Dr mwenyewe aliporudi baada ya kunusurika kifo aliaahidi kuwa ataweka mambo hadharani. Wakati anaendelea kutangaza kuwa ataweka mambo hadharani, tukasikia ghafla kapewa uwaziri.
Kuanzia hapo akasitisha matangazo ya kuwa ataeleza kilicho mpata na hivyo kumfanya rafiki yake Six kuonekana ni mnafiki na mwongo mkubwa. Sasa hicho kimya chake kinaeleweka kwani keshapewa fidia.
Sasa rafiki yangu "Dr. Mabwepande" kapewa nini hadi awe kimya namna hii na kusahau ahadi zake?!