Hmaster
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 346
- 86
Ama kweli za mwizi arobaini, nikiwa naendelea na kazi zangu humu ofisini kuna rafiki yangu mmoja amekuja ofisini kwangu macho yamemtoka, sijamuuliza tayari akanipa simu yake na kunionyesha sms ambayo kwa wakati huo ilikuwa bado ipo juu ya screen. Aliposcroll hadi chini nikaona ni jina na namba ya mke wake. Ujumbe ambao uliforwadiwa na mywife wake uliandikwa hivi: "SIKUTEGEMEA KAMA UNA MAPENZI MATAMU NAMNA ILE, YAANI JANA NIMELALA MWEPESI NA HATA KWENYE NDOTO ZANGU WEWE NDO ULITAWALA, NAAHIDI SITOKUACHA DEAR!". Sababu ya kuja kwangu mbio ni kunieleza kosa alilofanya na kuniomba ushauri ili akakabiliane na mkewe nyumbani. Nimebaki nacheka ingawa jamaa anataka kulia na nikamuahidi tukapate lunch pamoja ili tuchakachue ishu. Nimshauli vipi jamaa huyu ili wainusuru ndoa yao?