Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,778
WAZIRI Mkuu na Makamu wa Rais mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba (69), amepelekwa Afrika Kusini kwa matibabu baada ya afya yake kuzorota; Tanzania Daima imebaini.
Habari za uhakika ambazo gazeti hili limezipata kutoka vyanzo vilivyo karibu na familia ya Jaji Warioba zinaeleza kuwa mwanasiasa huyo anayeheshimika, alisafirishwa kwenda Afrika Kusini jana alfajiri.
Kwa mujibu wa habari hizo ambazo hata hivyo hazikueleza kiongozi huyo mstaafu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa gani, zilizothibitishwa na mwanafamilia mmoja, zilisema kuwa hali yake haikuwa ya kukatisha tamaa.
Pamoja na kukiri kupelekwa Afrika Kusini kwa mwanasiasa huyo, mwanafamilia huyo alilielezea tukio la mzee wake kusafirishwa kuwa ni la kuchunguzwa afya zaidi kuliko matibabu.
"Ni kweli baba anaumwa, leo (jana asubuhi) amepelekwa Afrika Kusini kwa ajili ya ‘check up' (matibabu) ili kubaini chanzo cha ugonjwa unaomsumbua," alisema mtoto huyo.
Alisema baba yake alikuwa imara hadi Jumamosi iliyopita, ambako alihudhuria mazishi ya aliyekuwa Balozi wa Kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Daudi Mwakawago.
"Jumamosi alikwenda kwenye mazishi ya Balozi Mwakawago akiwa mzima… lakini tangu juzi (Jumatatu) alionekena kudhoofika na mpaka sasa hatujajua nini kinachomsumbua zaidi," alisema mtoto huyo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Alli Idd, alipoulizwa kuhusiana na suala hilo, alijibu: "Niko Arusha kikazi, nawaomba muwasiliane na Ikulu, inaweza kuwa kwenye nafasi nzuri ya kutoa ufafanuzi."
Juhudi za gazeti hili kuwasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Salvatory Rweyemamu, ziligonga mwamba baada ya simu yake ya mkononi kuita bila kupokewa kwa muda wote jana.
Kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu Novemba 5, 1985 na Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, mwanasiasa huyo aliyezaliwa Septemba 3, 1940 amepata kushika nyadhifa mbalimbali kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Sheria.
Alikuwa Waziri Mkuu hadi Novemba 9, 1990 wakati Mwinyi alipovunja baraza la mawaziri na nafasi yake ikachukuliwa na John Samuel Malecela na yeye akateuliwa kuwa Waziri wa Nchi Tawala wa Mikoa na Serikali za Mitaa. Januari 17, 1996 wakati wa Serikali ya Rais wa Awamu ya Tatu, Jaji Warioba aliteuliwa na rais wa wakati huo, Benjamin Mkapa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kuchunguza Mianya ya Rushwa, ambayo ripoti yake ilimjengea umaarufu na heshima kubwa katika jamii.
Habari za uhakika ambazo gazeti hili limezipata kutoka vyanzo vilivyo karibu na familia ya Jaji Warioba zinaeleza kuwa mwanasiasa huyo anayeheshimika, alisafirishwa kwenda Afrika Kusini jana alfajiri.
Kwa mujibu wa habari hizo ambazo hata hivyo hazikueleza kiongozi huyo mstaafu alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa gani, zilizothibitishwa na mwanafamilia mmoja, zilisema kuwa hali yake haikuwa ya kukatisha tamaa.
Pamoja na kukiri kupelekwa Afrika Kusini kwa mwanasiasa huyo, mwanafamilia huyo alilielezea tukio la mzee wake kusafirishwa kuwa ni la kuchunguzwa afya zaidi kuliko matibabu.
"Ni kweli baba anaumwa, leo (jana asubuhi) amepelekwa Afrika Kusini kwa ajili ya ‘check up' (matibabu) ili kubaini chanzo cha ugonjwa unaomsumbua," alisema mtoto huyo.
Alisema baba yake alikuwa imara hadi Jumamosi iliyopita, ambako alihudhuria mazishi ya aliyekuwa Balozi wa Kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Daudi Mwakawago.
"Jumamosi alikwenda kwenye mazishi ya Balozi Mwakawago akiwa mzima… lakini tangu juzi (Jumatatu) alionekena kudhoofika na mpaka sasa hatujajua nini kinachomsumbua zaidi," alisema mtoto huyo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Alli Idd, alipoulizwa kuhusiana na suala hilo, alijibu: "Niko Arusha kikazi, nawaomba muwasiliane na Ikulu, inaweza kuwa kwenye nafasi nzuri ya kutoa ufafanuzi."
Juhudi za gazeti hili kuwasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Salvatory Rweyemamu, ziligonga mwamba baada ya simu yake ya mkononi kuita bila kupokewa kwa muda wote jana.
Kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu Novemba 5, 1985 na Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi, mwanasiasa huyo aliyezaliwa Septemba 3, 1940 amepata kushika nyadhifa mbalimbali kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Sheria.
Alikuwa Waziri Mkuu hadi Novemba 9, 1990 wakati Mwinyi alipovunja baraza la mawaziri na nafasi yake ikachukuliwa na John Samuel Malecela na yeye akateuliwa kuwa Waziri wa Nchi Tawala wa Mikoa na Serikali za Mitaa. Januari 17, 1996 wakati wa Serikali ya Rais wa Awamu ya Tatu, Jaji Warioba aliteuliwa na rais wa wakati huo, Benjamin Mkapa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Rais ya Kuchunguza Mianya ya Rushwa, ambayo ripoti yake ilimjengea umaarufu na heshima kubwa katika jamii.