Jaji Lubuva: Nape angeijua Serikali asingekurupuka

Jaji Lubuva: Nape angeijua Serikali asingekurupuka

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,645
Reaction score
164,792
Siku moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye,kutaka vigogo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) kung'oka,Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji mstaafu,Damian Lubuva,amesema amekurupuka kutoa kauli hiyo,kwakuwa hajui ukweli kutoka serikalini.

"Kama Nape angeweza kuwauliza wakubwa zake,serikali na Tume ya uchaguzi nina uhakika hayo aliyoyasema asingeyasema, lakini kwakuwa hajui ukweli ndio maana amekurupuka tu na mimi siwezi kujibizana nae,"alisema.

Chanzo:Tanzania Daima

My take:
Nape unajitia sana aibu!
 
Heri ya Pasaka WanaJf

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Lubuva ameshangaa sana Kauli ya katibu Mwenezi wa CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye aliyoitoa ya kwamba WAJIUZULU NAFASI ZAO kwa kuahhirisha tarehe ya kura ya maoni.
Akiongea kwa masikitiko Lubuva amesema
"Nape ni wa ajabu kwa nini asingeuliza wakubwa zake serikalini ambao ni Viongozi wake wa Chama ili kujua aliyekwamisha ni mimi au wao serikalini hizi ni sifa za Kitoto"
Nape na Kinana ina maana hayo mnayoyaongea huko majukwaani hamshauriani na Mwenyekiti wenu kabla ili mambo mnayoyafanya na kuongea yawe na nguvu zaidi?
Wananchi tutaamini vipi kwamba hayo mnayoyafanya na kuahidi yanaishia hewani tu?
Mwisho chama na Serikali huwa wanafanya kazi pamoja vp wewe hutaki kuuliza hata wateule wa Mwenyekiti wako unashutumu tu kutafuta sifa za muda tu jirekebisheni.
 
Ingetakiwa Nape amtukane huyo Mwenyekiti wa Nec matusi makubwa makubwa ili akasirike halafu kwenye kutangaza matokeo mwezi wa 11 asiibebe ccm kwa hasira.
 
Hata kama kuna tatizo kwenye tume ya taifa ya uchaguzi, Nape hakupaswa kuwakoromea kwenye vyombo vya habari bali angemshauri mwenyekiti wake (Kikwete) kuhusu mapendekezo yake binafsi.

Huu ni mwendelezo wa utendaji mbovu wa chama cha mapinduzi na serikali yake. Kila mtu anaropoka kila kinachokuja kinywani...tena kwa kuita waandishi wa habari.
 
Nape huwa ni chizi na anapenda kujipendekeza kwa jk jambo lipo wazi kbsa kuwa jk ndo katufikisha hapa tulipo halafu anamsumbua Mzee wa watu. Sijui kala maharage ya wapi huyuu
 
Huyo mzee hajajua nape anafanya ivo ili kukisafisha chama na serikali?
 
Hawa wote mafiganyanza.....JK Nyerere

Lubuva anatumika nakuburuzwa -ccm

Nape anatumika nakuburuzwa -ccm

Hawa woote wachafu na wakati wote maamuzi yao nikuibeba ccm.
 
Mzee hajui kateuliwa kulinda maslahi ya Chama na siyo kufuata professionalism yake,
akaulize wenzake kina Tido walifuata profesprofessionalism wakatajwa kuwa ni mojawapo wa watu waliosaidia kupunguza kura za Chama.
Mzee waachie wenyewe wamalizie maana matokeo ya kura ya maoni ya katiba yakija kinyume na matarajio/mmatakwa yao, utakuwa sababu
 
  • Thanks
Reactions: 999
Inaonekana mfumo wa uongozi wa ccm uko very disorganised
 
Wakati mwingine huwa ninakuwa na wasi wasi na uwezo wa kufikiri wa mkuu wetu wa nchi.Na sina wasi wasi na washauri wake , tatizo ni yeye mwenyewe.He never put a thought in anything he plans to do.Ni bora liende.
Heri ya Pasaka WanaJfMwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Lubuva ameshangaa sana Kauli ya katibu Mwenezi wa CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye aliyoitoa ya kwamba WAJIUZULU NAFASI ZAO kwa kuahhirisha tarehe ya kura ya maoni.Akiongea kwa masikitiko Lubuva amesema"Nape ni wa ajabu kwa nini asingeuliza wakubwa zake serikalini ambao ni Viongozi wake wa Chama ili kujua aliyekwamisha ni mimi au wao serikalini hizi ni sifa za Kitoto"Nape na Kinana ina maana hayo mnayoyaongea huko majukwaani hamshauriani na Mwenyekiti wenu kabla ili mambo mnayoyafanya na kuongea yawe na nguvu zaidi?Wananchi tutaamini vipi kwamba hayo mnayoyafanya na kuahidi yanaishia hewani tu?Mwisho chama na Serikali huwa wanafanya kazi pamoja vp wewe hutaki kuuliza hata wateule wa Mwenyekiti wako unashutumu tu kutafuta sifa za muda tu jirekebisheni.

Mkuu mwambieni Jaji Lubuva hana haja kujisumbua kufikiri sana.Yupo katikati ya watu wasiojua wanaenda wapi.
 
Siku moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye,kutaka vigogo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) kung'oka,Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji mstaafu,Damian Lubuva,amesema amekurupuka kutoa kauli hiyo,kwakuwa hajui ukweli kutoka serikalini.

"Kama Nape angeweza kuwauliza wakubwa zake,serikali na Tume ya uchaguzi nina uhakika hayo aliyoyasema asingeyasema, lakini kwakuwa hajui ukweli ndio maana amekurupuka tu na mimi siwezi kujibizana nae,"alisema.

Chanzo:Tanzania Daima

My take:
Nape unajitia sana aibu!
NAPE yuko sahihi, LUBUVA achia ngazi huna tija na taifa ni udanganyifu tu, Ukweli umekuwa siri kwani hiyo tume ya kusafirisha madawa ya kulevya??? Tume ya Uchaguzi eti kuna mambo kiongozi mkubwa kama nape hayajui, ni tume au chumba cha kulala cha mtu??? NEC yote iondoke haraka
 
Mkuu mwambieni Jaji Lubuva hana haja kujisumbua kufikiri sana.Yupo katikati ya watu wasiojua wanaenda wapi.
Wakati mwingine nalazima kukubaliana na wale wanachama wa CCM wanaomlalamikia Nape kwamba anaongea mawazo yake badala ya maelekezo na maamuzi ya Chama!
 
Back
Top Bottom