Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Dr. Hussein Ali Mwinyi leo ameongoza mazishi ya Jaji Haji Omar Haji huko mkoa wa Mjini Magharib Unguja Zanzibar.
Marehemu Jaji Haji Omar Haji pia aliwahi kuwa Mtendaji wa Mkuu Mahakama ya Africa Mashariki ( EACJ administrator) kati ya mwaka 2018 mpaka 2021 kabla ya kuteuliwa na Mh. Rais Hussein Mwinyi kuwa jaji Zanzibar.
Marehemu Jaji Haji Omar Haji aliteuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar mnamo Februari 01, 2021 na kuapishwa mnamo Februari 08, 2021.
Marehemu alizaliwa 4 June 1967 katika kisiwa cha Mafia mkoani Pwani kabla ya kuhamia Zanzibar 1985 kwa masomo ktk skuli ya sekondari Lumumba, kisha kuendelea na masomo ya juu katika Chuo cha Mzumbe Morogoro kusomea sheria. Baadaye alisomea shahada ya sheria kati vyuo vikuu vya Zanzibar na Afrika ya Kusini. Marehemu ameacha kizuka na watoto wanne.
Source : Zbc Zanzibar
Jaji Omar Haji
Mazishi yalihudhuria halaiki kubwa ya watu pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali, mahakama na vyama vya siasa. Marehemu alifariki ghafla baada ya kuumwa kwa muda mfupi.Marehemu Jaji Haji Omar Haji pia aliwahi kuwa Mtendaji wa Mkuu Mahakama ya Africa Mashariki ( EACJ administrator) kati ya mwaka 2018 mpaka 2021 kabla ya kuteuliwa na Mh. Rais Hussein Mwinyi kuwa jaji Zanzibar.
Marehemu Jaji Haji Omar Haji aliteuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar mnamo Februari 01, 2021 na kuapishwa mnamo Februari 08, 2021.
Marehemu alizaliwa 4 June 1967 katika kisiwa cha Mafia mkoani Pwani kabla ya kuhamia Zanzibar 1985 kwa masomo ktk skuli ya sekondari Lumumba, kisha kuendelea na masomo ya juu katika Chuo cha Mzumbe Morogoro kusomea sheria. Baadaye alisomea shahada ya sheria kati vyuo vikuu vya Zanzibar na Afrika ya Kusini. Marehemu ameacha kizuka na watoto wanne.
Source : Zbc Zanzibar