Kurunzi
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 9,285
- 9,920
Nimemsikiliza dogo JM Wakati akichangia majadala wa mpango wa maendeleo wa miaka 5 nimemkubali sana pamoja ya kuwa yupo kwenye chama chenye mitazamo na utashi wake lakini nimependezwa sana na uelewa na misimamo yake, ameonya serikali inoyoongozwa na chama chake kwa kufanya mambo kwa mazoea. "ukifanya kwa mazoea yale yale utapata matokeo yale yale yale" kuhusu elimu alisema nivema tukaangalia output au software zaidi kuliko hardware yaani serikali kuweka nguvu kubwa juu ya juzi waliopata wanafunzi badala ya wingi wa wanafunzi na majengo ya shule.