Mtoa uzi ni mvivu wa kuchunguza,na anashangaa tu kwa sababu inaoneshwa hapa kwetu,Jaribu kuangalia tv stations za nje utaona tamthilia za THE BOLD AND THE BEAUTIDUL,bado inaoneshwa muda mrefu tu,kuna Passions,Scandal na zingine zisizoisha na ni muda mrefu tu umepita bado hazijaisha,au umezoea Kaole
naingalia hii kila siku na kuna ingine inaitwa rythm city, soap za south africa nzuri sana....zinagusa angle zote za maisha kazi,biashara,shule,crime,high life,low life yaani ni maisha halisi ya kila siku.....za kifilipino siwezi hata kuangalia dakika kumi kwasababu ni mapenzi mapenzi na mapenzi.
hahahahaha hivi ilianza mwaka gani
Kama ya leo ni nzuri sana natamani kesho ifike nione nini kitaendelea kwa katlego na calvin
nampenda Lerato anayoumwa cancer nataman hadi kulia........ ni makeke fulan sa hivi kapoa huyooo
Hivi jamani kuna kitu sijakielewa hapa kuhusu hii isdingo the need, kwanini huwa haishi?? Ina maana itv wamekosa kipindi kingine cha kuelimisha jamii zaidi ya hiki cha isdingo?? Au kuna percent wanapata kutoka kwa hao isdingo wenyewe???? Isdingo yenyewe haina mashabiki hata kidigo, maisha gani ya ki miner yasiyo na mwisho?? Itv
muache kutuzingua banaaa!!!
Mkuu maisha huwa yanakuwa na mwisho? Watu ndio wana mwisho lakini maisha huwa yanaendelea na ndio maana kwenye Isidingo watu wanabadilika. Soap Opera nyingi huchukua muda mrefu sana kuonyeshawa kwa sababu zinasimulia maisha ya jumla ya mahali fulani na sio kisa fulani specifically. Days of Our Lives ambayo hapa kwetu iliwahi kuonyeshwa na Channel 10 kama sikosei, ilianza kuonyeshwa mwaka 1965 na mpaka leo bado inaonyeshwa.
Mimi mwenyewe niliifuatilia nikachoka lakini siwezi kulalamika kwa nini wanaendelea kuonyesha, inaonekana kuna watu wengi bado wanaipenda.
Tamthilia ya tangu mwaka 1995 mpaka sasa zaidi ya miaka 20.kweli kama naangalia ITV ukifika mda wa isidingo huwa nahamia channel nyingine.tumeichokaaaa
naipenda isidingooo
Hivi jamani kuna kitu sijakielewa hapa kuhusu hii isdingo the need, kwanini huwa haishi?? Ina maana itv wamekosa kipindi kingine cha kuelimisha jamii zaidi ya hiki cha isdingo?? Au kuna percent wanapata kutoka kwa hao isdingo wenyewe???? Isdingo yenyewe haina mashabiki hata kidigo, maisha gani ya ki miner yasiyo na mwisho?? Itv
muache kutuzingua banaaa!!!
Mtoa uzi ni mvivu wa kuchunguza,na anashangaa tu kwa sababu inaoneshwa hapa kwetu,Jaribu kuangalia tv stations za nje utaona tamthilia za THE BOLD AND THE BEAUTIDUL,bado inaoneshwa muda mrefu tu,kuna Passions,Scandal na zingine zisizoisha na ni muda mrefu tu umepita bado hazijaisha,au umezoea Kaole
Wale wanaoangalia etv kuna nyingine nayo inaitwa the "Young and the Restless" nayo haiishi
Watoto wanapenda vitamthilia vya kifilipino aangalie mwezi mmoja miwili,huku wanaigiza maisha yasiyo ya uhalisia...ni mapenzi tu..
hii ni ishara ya uvivu wa kufikiri, ndiyo maana uapenda vitu rahisi rahisi - isidingo haina mfano wake hata wenye shida ya lugha wanaikubali
nimezaliwa nimeikuta