ITV na CHADEMA

ITV na CHADEMA

Taarifa ya ITV kupuzia aliyekufa na kumpa kipaumbele aliyenusurika
Imetangazwa sababu ya huyo aliyenusurika
Unafikiri hiyo ndiyo ajali pekee kwa tz siku hiyo ?
Lakini ulichoandika viroba vikukutoka soma tena na uandae Uzi mwingine
 
hebu angalia hii, halafu uache UNAA.

Kupitia video hii unaweza ona kuwa ile ya mwanzo ni breaking news na hii video imeonyesha kila kitu mpk sugu anavyoumia kwa gari yake kusababisha kifo,imejitosheleza cjui Uhuru tv wamelipoti vipi huko
 
Hakuna sababu ya kuwalaumu ITV.. Nafikiri sugu kwa wadhifa alionao ndio ameibeba habari!

Ni ujinga tu unaweza kumfanya mjinga awalaumu ITV eti wana uchadema kisa wamewasilisha kunusurika kwa "mbunge" kabla ya kifo!
Ni kweli sugu ndio amebeba habari.....
Swali hapa ni kaibeba positively au negatively?
Kwamba mtoto kasababisha ajali Lakini kwa bahati Nzuri Mh. Sugu 'KASALIMIKA'
Au Mh.Sugu amehusika ktk ajali iliyopekea kifo cha KIJANA?
Habari hapo Sio SUGU kusalimika ktk ajali Bali habari hasa ni SUGU au gari la SUGU kuua ktk ajali
 
Sugu alikuwa abiria kwenye hii ajali ingawa yeye ndie mmiliki wa gari.

Dereva wake alijaribu kusimama kwenye zebra ili yule mtoto yule avuke barabara pale kwenye zebra lakini ndio ivyo tena breki zikafeli ajali ikatokea.

Hilo linaweza kumtokea mtu yeyote na ukumbuke gari ni kama mashine sometimes mashine inafeli kwasababu mbalimbali.
Na hiyo mashine iliyofeli breki iliweza kusimama vizuri tu baada ya kukimbizwa na boda boda, na ikaweza kurudi eneo la ajali na kusimama vizuri tu....breki za ajabu sana hizi wallahi.
 
f7435447ffa9bab2372f63cb4130d11a.jpg
Hili sio swala la mahaba ya chama.
Ni uandishi mbovu wa habari.
ITV wanaichunia chadema hadi wanalia humu jukwaani.
Mwandishi aliweka focus ya ajali kwa mbunge...ambalo ni kosa la kiuandishi..
Nadhani alitaka kusema "mbunge anusurika kifo katika ajali...."

Mbunge hakunusurika ajali, amepata ajali lakini kanusurika kifo.

Na ni makosa kusisitiza walionusurika na kupotezea waliopoteza maisha..
 
Mleta uzi una matatizo je unakumbuka idadi ya waliokufa kutokana na misafara ya maccm
 
leta ushahidi kuwa sugu alikuwa abiria.sugu alikuwa peke yake ndio maana alikimbia,akaenda kumwita Driver
Wakati mwingine sio lazima uanike ujinga wako!Siku zote tunajua madereva wakisababisha ajali kwa uzembe huwa wanakimbia hasa kifo kinapotokea!Sasa ni dereva gani huyo bwege anayeweza kukubali kuitwa kuja kupewa kesi ya mauaji?
Mara baada ya ajali,watu walijaa pale!Ina maana hao watu hawakuona dereva ni nani?Eti mpaka mtu aitwe ndio aje afike eneo la tukio ndio aingie kwenye gari iliyopata ajali halafu ndio atoke kwamba ni dereva!
 
Taarifa ya ITV kupuzia aliyekufa na kumpa kipaumbele aliyenusurika
Umejuaje kama kuna mtu amekufa?Au ulisikia sehemu tofauti na ITV?
Nways hata ingekuwa hivyo wala usishangae,kama PM kutwa anahangaika na Faru John wakati kuna watu wamefukiwa bila kutambulika lakini pia Binadamu amepotea lakini wala hakuna anayeshughulika nao!
 
D
Hata kama alikuwa haendeshi yeye lakini kwanini dereva hajawekwa ndani kama wanavyofanyiwa madereva wengine? Kuna jambo kati ya Cdm, Polisi na ITV.
Duuuuh,una uhakika gani kama hajashikiliwa
 
Ukisema amenusurika kifo..unamaanisha kwamba Sugu anathamani kubwa kuliko huyo mtoto aliyekufa...habari kubwa hapa ni kifo cha mtoto na siyo kunusurika kwa sugu
Huo ni upotoshaji,hebu angalia hiyo clip!
 
Wakati mwingine sio lazima uanike ujinga wako!Siku zote tunajua madereva wakisababisha ajali kwa uzembe huwa wanakimbia hasa kifo kinapotokea!Sasa ni dereva gani huyo bwege anayeweza kukubali kuitwa kuja kupewa kesi ya mauaji?
Mara baada ya ajali,watu walijaa pale!Ina maana hao watu hawakuona dereva ni nani?Eti mpaka mtu aitwe ndio aje afike eneo la tukio ndio aingie kwenye gari iliyopata ajali halafu ndio atoke kwamba ni dereva!
Kwa hiyo dereva alikimbia akiwa na muheshimiwa? Maana gari ilikimbizwa na boda boda,muheshimiwa alimuachaje dereva avunje sheria?
 


Wewe kilaza sana...Sugu hakuwa dereva was hiyo gari, yeye alikuwa abiria katika gari yake. Katika safari hiyo gari yake hiyo iligonga ikaua wakati yeye akiwa abiria na yeye akanisurika.

Kwa maana hiyo basi Sugu hakuua
 
Kwa hiyo dereva alikimbia akiwa na muheshimiwa? Maana gari ilikimbizwa na boda boda,muheshimiwa alimuachaje dereva avunje sheria?
Utajua mwenyewe,dereva anashikiliwa na jeshi la polisi!Kama una chuki binafsi,jinyonge!
 
Watu wengi wanagongwa na magari na kufanya na wengi tu wanagonga watu na kufanya pia.

Lakini hili la Mbeya limevuma sana na kuwa habari kubwa kwasababu ndani ya Gari alikuwepo Mh Joseph Mbilinyi ( Sugu ) Mbunge wa Jiji la Mbeya.

Kwa hiyo hata coverage ya vyombo vya habari itamtaja sana Mh 'Sugu' kuliko hata huyo mtoto tena yatima aliyefariki.

Ndiyo ilivyo duniani kote.
 
Back
Top Bottom