Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) kimesisitiza kuwa endapo kitapata ridhaa ya kuingia madarakani, kipaumbele chake kitakuwa kuwawajibisha wote walioiba mali za umma.
Kauli hiyo imetolewa Oktoba 3, 2024 katika Wilaya ya Ilemela, wakati wa mwendelezo wa kampeni za mtaa kwa mtaa zinazofanywa na Mwenyekiti wa ADC Taifa, Shabani Itutu ambaye pia ni mgombea ubonge wa Ilemela mkoani Mwanza.
Itutu, ameeleza kuwa tatizo la ufisadi ndilo limekuwa chanzo kikuu cha changamoto nyingi zinazowakabili wananchi ikiwemo upungufu wa madawa hospitalini.
Kwa mujibu wa maelezo yake, zaidi ya Sh30 trilioni zimepotea kutokana na matumizi mabaya na ubadhirifu ulioainishwa kwenye ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) tangu mwaka 2021.
Hata hivyo, licha ya wahusika kutajwa hadharani, Itutu amedai hakuna hatua za kisheria zilizochukuliwa dhidi yao.
Kauli hiyo imetolewa Oktoba 3, 2024 katika Wilaya ya Ilemela, wakati wa mwendelezo wa kampeni za mtaa kwa mtaa zinazofanywa na Mwenyekiti wa ADC Taifa, Shabani Itutu ambaye pia ni mgombea ubonge wa Ilemela mkoani Mwanza.
Itutu, ameeleza kuwa tatizo la ufisadi ndilo limekuwa chanzo kikuu cha changamoto nyingi zinazowakabili wananchi ikiwemo upungufu wa madawa hospitalini.
Kwa mujibu wa maelezo yake, zaidi ya Sh30 trilioni zimepotea kutokana na matumizi mabaya na ubadhirifu ulioainishwa kwenye ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) tangu mwaka 2021.
Hata hivyo, licha ya wahusika kutajwa hadharani, Itutu amedai hakuna hatua za kisheria zilizochukuliwa dhidi yao.