John safar tour
Member
- Dec 8, 2021
- 25
- 55
ITANIGHARIMU KIASI GANI KUTALII KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI?
Napenda kuchukua nafasi hii kutoa ufafanuzi kwa wale wanaotamani kwenda kutalii lakini hawajui itawagharimu shilingi ngapi.
Gharama ya kutalii mara nyingi inabadirika kutegemeana na sababu mbalimbali kama vile...
Kampuni utakayotaka kutumia, upatikanaji wa gari(kama ni gari binafsi au ya kukodi), chakula, na malazi endapo utapenda kulala hifadhini.
Kwa ufupi tu makadirio ya upesi kwa kundi la watu 2 hadi 5 itagharimu kuanzia laki 5 kuendelea kwa safari ya siku moja (Day Trip). Na kwa kundi la watu 6 hadi 12 itagharimu kuanzia laki 6 na kuendelea. Kama safari itahusisha kulala hifadhini gharama zinaweza ongezeka kutegemea na endapo utachagua kulala lodge, campsite au hostel.
Endapo pia utatumia gari binafsi gharama zinaweza kupungua Hadi kufikia shilingi laki 2-3 kwa kundi la watu 2 hadi 5.
Kumbuka: Gharama zinahusisha kiingilio Cha HIFADHI, chakula, muongoza watalii na tozo ya gari.
KAMA UNA SWALI LOLOTE TAFADHARI ULIZA NA NITAKUJIBU HAPAHAPA!
Kwa wakazi wa mikoa ya kaskazini, pwani na kati kama vile Arusha, Kilimanjaro, Dodoma, Tanga, Pwani n.k wanaweza kwenda Hadi Arusha au Moshi na kuzungumza na kampuni za watalii zinazopatikana maeneo hayo.
Kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa inapendeza zaidi kuanzia safari yao katika mji wa Mugumu kupitia geti la Tabora-B au Ikoma na kumalizia katika geti la Ndabaka.
Binafsi napatikana katika mji wa Mugumu, Wilayani Serengeti.
Asante!
Napenda kuchukua nafasi hii kutoa ufafanuzi kwa wale wanaotamani kwenda kutalii lakini hawajui itawagharimu shilingi ngapi.
Gharama ya kutalii mara nyingi inabadirika kutegemeana na sababu mbalimbali kama vile...
Kampuni utakayotaka kutumia, upatikanaji wa gari(kama ni gari binafsi au ya kukodi), chakula, na malazi endapo utapenda kulala hifadhini.
Kwa ufupi tu makadirio ya upesi kwa kundi la watu 2 hadi 5 itagharimu kuanzia laki 5 kuendelea kwa safari ya siku moja (Day Trip). Na kwa kundi la watu 6 hadi 12 itagharimu kuanzia laki 6 na kuendelea. Kama safari itahusisha kulala hifadhini gharama zinaweza ongezeka kutegemea na endapo utachagua kulala lodge, campsite au hostel.
Endapo pia utatumia gari binafsi gharama zinaweza kupungua Hadi kufikia shilingi laki 2-3 kwa kundi la watu 2 hadi 5.
Kumbuka: Gharama zinahusisha kiingilio Cha HIFADHI, chakula, muongoza watalii na tozo ya gari.
KAMA UNA SWALI LOLOTE TAFADHARI ULIZA NA NITAKUJIBU HAPAHAPA!
Kwa wakazi wa mikoa ya kaskazini, pwani na kati kama vile Arusha, Kilimanjaro, Dodoma, Tanga, Pwani n.k wanaweza kwenda Hadi Arusha au Moshi na kuzungumza na kampuni za watalii zinazopatikana maeneo hayo.
Kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa inapendeza zaidi kuanzia safari yao katika mji wa Mugumu kupitia geti la Tabora-B au Ikoma na kumalizia katika geti la Ndabaka.
Binafsi napatikana katika mji wa Mugumu, Wilayani Serengeti.
Asante!