IST inakula sana mafuta, sijui tatizo

IST inakula sana mafuta, sijui tatizo

Ok nimemlisha tango basi tufafanulie maana ya OVERDRIVE na side effect yake ikiwa 'ON' na 'OFF', then tuendelee.
Sasa fafanua ni wakati gani inatakiwa iwe ON na wakati gani inatakiwa kuwa OFF. Hapa ni kuelimishana tu unaweza kuwa na gari au simu hata kwa miaka 10 lakini ukawa hujui namna ya kutumia vitu vilivyomo. Elimu haina mwisho toa ilimu mkuu!
 
Hapa ni kulishana matango pori tu,sasa overdrive iwe ON tena? Unajua kazi ya over drive na nini kinafanyika kwenye gear box mara inapokua turned on?

Sorry hiyo ya mwanzo nilikuwa namjibu CHARGER nikakosea nikaquote wewe. Huyo jamaa alitakiwa kufafanua tu ni wakati gani OVERDRIVE iwe ON na wakati gani iwe OFF
 
Sasa fafanua ni wakati gani inatakiwa iwe ON na wakati gani inatakiwa kuwa OFF. Hapa ni kuelimishana tu unaweza kuwa na gari au simu hata kwa miaka 10 lakini ukawa hujui namna ya kutumia vitu vilivyomo. Elimu haina mwisho toa ilimu mkuu!

Mi nimetoa ushauri kwa Ushirombo naambiwa namlisha tango, so its better ndugu yetu charger aliyesema namlisha tango basi yeye akatoa elemu maana yeye ndiyo anafahamu vizuri. Mtu hana imani na Mimi kwa nini niendelee kuwalisha matango??
 
Last edited by a moderator:
Nadhani nikubaliane na ushauri wa Kisiri. Ni kweli hata mimi nina IST. Inakula zaidi mafuta ukilinganisha engine capacity yake. Huenda tatizo likawa mojawapo ya mambo aliyosema Kisiri. I'll do that.
 
Nadhani nikubaliane na ushauri wa Kisiri. Ni kweli hata mimi nina IST. Inakula zaidi mafuta ukilinganisha engine capacity yake. Huenda tatizo likawa mojawapo ya mambo aliyosema Kisiri. I'll do that.

Kijana hebu check pia mi nimeanza na oxygen sensor,niliikuta imechafuka sana,sasa nimesafisha ngoja nione outcome,nitakuja na majibu,
 
LEGE

Mkuu unge edit bs yani umegoogle ukayamwaga jinsi yalvyo
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ushirombo, kashughulikie yafuatayo:-

1. Angalia tenki la mafuta kama lina unyevunyevu. Kama linao basi linavujisha mafuta.

2. Angalia mfuniko wa tenki? Unafunga vizuri? Ni vizuri ubadilishe au badilisha seal zake

3. Kagulia pipes za mafuta kutoka kwenye tenki na kurudi kwenye tenki pamoja na fuel rail. Hakikisha hazina unyevunyevu wa kuvujisha mafuta

4. Angalia 'Charcoal Canister' kama inafanya vizuri

5. Cheki pipe ya kutoka kwenye 'Charcoal Canister' to intake manifold kama imechomekwa vizuri

6. Nozzles kama zina muda mrefu zibadilishe. Kusafisha haisaidii na zenyewe huwa zinachoka

7. Hakikisha spark plugs zako zote zinachoma

8. Badilisha Oxygen sensors

9. Safisha throttle body yote kwa sababu carbon deposits huwa inajaa ndani yake hivyo kuziba hewa kuingia kwenye combustion chambers

10. Hakikisha Overdrive button ipo 'ON'

11. Hakikisha Crankase ventilation System inafanya kazi vizuri (PCV pipes na PCV valve hazijaziba)

Ukishayafanya hayo rudi utupe maendeleo Mkuu.

Safi sana kaka, naona watu wanacoment ujinga!
 
Hopeless, kaa kimya kama huna cha kusema,we unafikiri sina au gari imebadili fuel consumption rate? Hata akiwa tajiri vp lazima gari aitunze na aitengeneza kila inapoonekana kuharibika,so unataka niitupe au niendelee kuwa nayo hvyo hvyo? Nyie ndo mnao haribu jukwaa,unapoona hujisikii kuchangia au hujui kaa kimya,kwani utachapwa usipoonesha ujinga wako humu? Mnaudhi sana

Wanaudhi sana kwa kweli
 
Wakuu naombeni ufafanuzi kuhusu kuiweka ON au OFF hiyo Overdrive button, maana mawazo yangu yalikuwa kwamba kwa jinsi kiingereza kilivyokaa, overdrive ikiwa OFF ndio inakula mafuta kidogo!

Kwa kifupi gia za magari zimegawanyika mara tatu. Kuna Underdrive Gears, Direct Drive Gears na Overdrive Gear(s). Underdrive Gears ni gia ambazo zinafanya input shaft ya kwenda kwenye Gearbox (ambayo ni Output shaft ya Engine) inapozunguka mzunguko mmoja inapelekea output shaft (Propeller shaft / Drive shaft) izunguke for less than one turn. Mara nyingi kwa Gari ambazo zina Gear nne, Gia namba moja, mbili na Gia ya Reverse ni Underdrive Gears.

Direct Drive Gears ni gia ambazo zinafanya Input shaft ya kwenda kwenye Gearbox inapozunguka mzunguko mmoja inapelekea output shaft na yenyewe kuzunguka mara moja. Kwa gari zenye Gia nne, Gia namba tatu ni Direct Drive Gear.


Sasa, Overdrive Gears ni gia ambazo zinafanya Input shaft ya kwenda kwenye Gearbox inapozunguka mzunguko mmoja inapelekea output shaft (Propeller / Drive Shaft) izunguke zaidi ya mzunguko mmoja. Kwa gari zenye Gia nne, Gia namba nne ni Overdrive Gear.

Relationship ya mizunguko kati ya Input shaft na Output shaft ndiyo kwa kitaalamu inaitwa 'Gear ratio'. So, Underdrive Gear ratio inakuwa higher than 1 (Mfano 1:0.5), Direct Drive Gear ratio always inakuwa ni 1 (i.e. 1:1) na Overdrive Gear ratio inakuwa less than 1 (Mfano 1:1.6).

Aidha, Kwa gari zenye Gia tano, sita, nane na kuendelea inategemea na jinsi manufacturer ame-design gear ipi iwe Underdrive, Direct Drive na Overdrive Gear. So unaweza kukuta gia zaidi ya moja mfano gia namba tano na sita ndiyo Overdrive Gears kwenye Gearbox yenye gia sita, nk. It depends on the design.

Sifa ya Underdrive Gears ni gia zenye nguvu lakini hazina speed. Sifa za Overdrive Gears ni gia ambazo hazina nguvu lakini zinazalisha speed kubwa. Sifa ya Direct Drive Gear ina sifa ambazo zina range between the two above. Yaani zina nguvu ingawa si kama Underdrive Gears lakini ni zaidi ya Overdrive Gear na zina Speed ingawa si kama Overdrive Gears lakini ni zaidi ya Underdrive Gear

Matumizi ya Overdrive Button
Unapowasha Overdrive button "ON" maana yake umeiruhusu gearbox ku-engage hadi kwenye Overdrive Gear gari iki-meet certain conditions (Mfano spidi ikifikia level flani). Uzuri wa Overdrive Gear ni kwamba ina-save mafuta kwa sababu input shaft (Output shaft ya Engine) itakapozunguka mzunguko mmoja itapelekea matairi ya gari(through Propeller / Drive shaft) kuzunguka zaidi ya mzunguko mmoja (Assuming Axle Ratio ni 1:1) na hivyo kukufikisha unapokwenda kwa kutumia mafuta machache yatakayotumika kuzungusha engine mara mmoja tu tofauti na Underdrive Gears ambazo ili matairi yazunguke mzunguko mmoja ni lazima engine izunguke zaidi ya mzunguko mmoja (na hivyo mafuta kuchomwa mengi).

So Overdrive inapoiweka 'OFF' maana yake unaizuia gearbox ku-engage into higher gears ambazo kimsingi zina-save mafuta. Aidha, inapoiweka 'OFF' huku gari unaikimbiza kwa kunyaga sana accelerator pedal unachosha Engine.

Unaruhusiwa kuweka 'OVERDRIVE OFF' katika mazingira ambayo unapanda mlima wenye kilomita nyingi. Mfano unapopanda Mlima Kitonga ni muhimu kuweka 'OVERDRIVE OFF' lakini usikanyage accelerator pedal saana hadi mwisho (doing so unaweza pasua head gasket). Kwa kufanya hivyo utakuwa imeiambia Gearbox kwa mazingira uliyomo Overdrive Gears are irrelevant so just engage on Underdrive Gears only. Ushuhuda wa hili upo hata kwenye Gari za Manual. Hata ukianzia na gia yako namba nne kutoka chini ya Kitongo ukapanda nayo kwa speed mwisho wa siku ukifika katikati itakubidi tu urudi kwenye gear namba mbili au moja ambazo ndizo gia nzuri za kupandia Milima. Kwa sababu underdrive gears zina nguvu ya kupandisha gari Mlima kuliko na Overdrive Gears.

CC: CYBERTEQ, Ushirombo, charger TCleverly, mandingo6262, etc
 
Last edited by a moderator:
Kwa kifupi gia za gari zimegawanyika mara tatu. Kuna Underdrive Gears, Direct Drive Gears na Overdrive Gear(s). Underdrive Gears ni gia ambazo zinafanya input shaft ya kwenda kwenye Gearbox (ambayo ni Output shaft ya Engine) inapozunguka mzunguko mmoja inapelekea output shaft (Propeller shaft / Drive shaft) izunguke for less than one turn. Mara nyingi kwa Gari ambazo zina Gear nne, Gia namba moja, mbili na Gia ya Reverse ni Underdrive Gears.

Direct Drive Gears ni gia ambazo zinafanya Input shaft ya kwenda kwenye Gearbox inapozunguka mzunguko mmoja inapelekea output shaft na yenyewe kuzunguka mara moja. Kwa gari zenye Gia nne, Gia namba tatu ni Direct Drive Gear.


Sasa, Overdrive Gear ni gia ambazo zinafanya Input shaft ya kwenda kwenye Gearbox inapozunguka mzunguko mmoja inapelekea output shaft (Propeller / Drive Shaft) izunguke zaidi ya mzunguko mmoja. Kwa gazi zenye Gia nne, Gia namba nne ni Overdrive Gear.

Relationship ya mizunguko kati ya Input shaft na Output shaft ndiyo kwa kitaalamu inaitwa 'Gear ratio'. So, Underdrive Gear ratio inakuwa higher than 1 (Mfano 1:0.5), Direct Drive Gear ratio always inakuwa ni 1 (i.e. 1:1) na Overdrive Gear ratio inakuwa less than 1 (Mfano 1:1.06).

Aidha, Kwa gari zenye Gia tano, sita, nane na kuendelea inategemea na jinsi manufacturer ame-design gear ipi iwe Underdrive, Direct Drive na Overdrive Gear. So unaweza kukuta gia zaidi ya moja mfano gia namba tano na sita ndiyo Overdrive Gears kwenye Gearbox yenye gia sita, nk. It depends on the design.

Sifa ya Underdrive Gears ni gia zenye nguvu lakini hazina speed. Sifa za Overdrive Gears ni gia ambazo hazina nguvu lakini zinazalisha speed kubwa. Sifa ya Direct Drive Gear ina sifa ambazo zina range between the two above. Yaani zina nguvu ingawa si kama Underdrive Gears lakini ni zaidi ya Overdrive Gear na zina Speed ingawa si kama Overdrive Gears lakini ni zaidi ya Underdrive Gear

Matumizi ya Overdrive Button
Unapowasha Overdrive button "ON" maana yake umeiruhusu gearbox ku-engage hadi kwenye Overdrive Gear gari iki-meet certain conditions (Mfano spidi ikifikia level flani). Uzuri wa Overdrive Gear ni kwamba ina-save mafuta kwa sababu input shaft (Output shaft ya Engine) itakapozunguka mzunguko mmoja itapelekea matairi ya gari(through Propeller / Drive shaft) kuzunguka zaidi ya mzunguko mmoja (Assuming Axle Ratio ni 1:1) na hivyo kukufikisha unapokwenda kwa kutumia mafuta machache yatakayotumika kuzungusha engine mara mmoja tu tofauti na Underdrive Gears ambazo ili matairi yazunguke mzunguko mmoja ni lazima engine izunguke zaidi ya mzunguko mmoja (na hivyo mafuta kuchomwa mengi).

So Overdrive inapoiweka 'OFF' maana yake unaizuia gearbox ku-engage into higher gears ambazo kimsingi zina-save mafuta. Aidha, inapoiweka 'OFF' huku gari unaikimbiza kwa kunyaga sana accelerator pedal unachosha Engine.

Unaruhusiwa kuweka 'OVERDRIVE OFF' katika mazingira ambayo unapanda mlima wenye kilomita nyingi. Mfano unapopanda Mlima Kitonga ni muhimu kuweka 'OVERDRIVE OFF' lakini usikanyage accelerator pedal saana hadi mwisho (doing so unaweza pasua head gasket). Kwa kufanya hivyo utakuwa imeiambia Gearbox kwa mazingira uliyomo Overdrive Gears are irrelevant so just engage on Underdrive Gears only. Ushuhuda wa hili upo hata kwenye Gari za Manual. Hata ukianzia na gia yako namba nne kutoka chini ya Kitingo ukapanda nayo kwa speed mwisho wa siku ukifika katikati itakubidi tu urudi kwenye gear namba mbili au mmoja ambazo ndizo gia nzuri za kupandia Milima. Kwa sababu underdrive gears na zina nguvu tofauti ya kupandisha gari Mlima kuliko na Overdrive Gears.

CC: CYBERTEQ, Ushirombo, charger TCleverly, mandingo6262, etc

Duuu ingawa c mtaalamu wa magari, kwa maelezo haya umeniongezea kitu Mkuu. Mimi nilikuwa naweka overdrive on pale ninapoovateki tu ili niovertake faster. Big up brother kwa kutupa elimu.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana. IST inapotumia mafuta kama Land Cruiser 4.7 V8 basi kuna tatizo kubwa. Dawa hapa ni kuifanyia diagnosis ambayo itakuwezesha kugundua tatizo ni nini kuliko kufanya matengenezo au marekebisho ya kubahatisha.
 
kama alivyosema mkuu hapo juu lakini hapo cha mhim cha kuanza nancho ni namaba 8 oxygen sensor na namba 9 hapo kwenye namaba 9 kuna sensor inaitwa idle sensor hiyo ukitaka kujua kama inafanya kazi vizuri gari ukiwasha asubuhi huwa inakuwa sailensa juu jinsi inavyopata moto taratibu inashuka mpaka kwenye normal. hiyo ndio huwa inakula sana mafuta kama ikiwa chafu?? kama upo dar na hauto jari nitafute nikufanyie hiyo kazi na ukitaka tukupimie nitakupimia mashine ninayo. phone 0717228064.

tatizo wabongo ni wabishi sana na wengi tumeathirika na used kuna spea zingine hazitakiwi used mfano oxygen sensor ww huwezi jua imetumika kiasi gani ww unanunua unaweka ilimladi tu taa ta check engine izime

Kamanda mie nina IST ya 1290 cc ila inayapiga 10 km/l ukiwa na kiyoyozi. Ni sawa? Pia nina glanza inatatizo la kutetemeka steering na pia bomba la Moshi linakuwa na ukoko wa moshi. Nahisi kuna tatizo la ulaji mafuta pia. Ulishakumbana nalo hili tatizo?
 
wana jf,nina ist cc 1490,mileage 89000km,nilisafiri toka mza to dar,ikaanza tatizo la kutumia mafuta zaidi ya kawaida yake,ilikua inatumia 16km/litre lakini saiv inaenda hadi 8km/litre nimefanya yafuatayo lakin bado tatizo nimebadili engine oil na gearbox oil,nimetoa plugs nikaweka mpya,nimesafisha nozels,air filter na oil filter.Nisaidieni jamani nifanye nini zaidi ili irudi kama zamani? Nafirisika mie.

Kamanda hii ni ukiwa umewasha ac au bila ac? Mie nina ile ya 1290 inatafuna 10km/l na ac!!!! Ni sawa au nami namumung'wa?
 
Pole sana. IST inapotumia mafuta kama Land Cruiser 4.7 V8 basi kuna tatizo kubwa. Dawa hapa ni kuifanyia diagnosis ambayo itakuwezesha kugundua tatizo ni nini kuliko kufanya matengenezo au marekebisho ya kubahatisha.

mkuu, diagnosis ya uhakika inafanyika wapu kwa hapa dsm? so far naona kuna member mmoja hapo juu amesema anafanya
 
mkuu, diagnosis ya uhakika inafanyika wapu kwa hapa dsm? so far naona kuna member mmoja hapo juu amesema anafanya

Wajaribu MG Car Computer Diagnostic wako Oil Com, Magomeni Kagera (karibu na Mwembe Chai)
 
jamani mi nasikia nduvin autospares ni wayeyushaji na pia wana bei kubwa sana katika kufanya diagnosis ya gari,Je akina nani hapa dar ni wazuri kwa shughuli hyo?, na bei zao please
 
... Uzuri wa Overdrive Gear ni kwamba ina-save mafuta kwa sababu input shaft (Output shaft ya Engine) itakapozunguka mzunguko mmoja itapelekea matairi ya gari(through Propeller / Drive shaft) kuzunguka zaidi ya mzunguko mmoja (Assuming Axle Ratio ni 1:1) na hivyo kukufikisha unapokwenda kwa kutumia mafuta machache yatakayotumika kuzungusha engine mara mmoja tu tofauti na Underdrive Gears ambazo ili matairi yazunguke mzunguko mmoja ni lazima engine izunguke zaidi ya mzunguko mmoja (na hivyo mafuta kuchomwa mengi). ...
Thanks, it's logical na nakiri nimepata maarifa
 
Uliweka overdrive on kwenye gari inasaidia gari lisile mafuta? Naomba kujuzwa.
 
Back
Top Bottom