6 Pack
JF-Expert Member
- Apr 17, 2022
- 1,826
- 4,076
Niaje waungwana
Baada ya kipigo cha makombora madogo tu yalioshindwa kuzuiwa na nchi zaidi ya 8 zinazojifanya super power duniani, Israel imeamua sasa kujibu kipigo hicho kwa kupanga mipango ya kwenda kuvamia mji wa watoto, wanawake na wazee wasiojiweza ili kuhadaa umma na kuitoa dunia katika ajenda yake iliyoshindwa ya kulipiza kisasi kwa Iran ambalo ni taifa babe, lenye nguvu na uwezo wa kijeshi kuliko taifa lolote huko Mashariki ya kati.
Inasemekana baada ya kipigo cha Iran kwa Israel ambacho kimeleta heshima na utulivu katika eneo hilo, ndugu Netanyahu waziri mkuu wa Israel akataka apate uungaji mkono wa jeshi na silaha kutoka kwa Marekani na washirika wake wengine ili na yeye akajitutumue kubweka kwa watemi wa eneo (Iran) ila washirika wakiongozwa na Marekani wakagoma kutoa jeshi na silaha, wakihofia usalama zaidi wa nchi hiyo (Israel), endapo itataka kuthubutu kuendelea kuvimbishiana misuli na dubwasha (Iran) linaloipa silaha za bure hata Russia ambayo ni super power namba 2 duniani.
Kama wengi tunavyojua kwamba Israel bila Marekani na Uingereza ni sawa sawa na mbwa asiekuwa na meno, kamwe haiwezi kupambana na nchi yoyote mpaka ipate support ya silaha na jeshi. Kwahiyo Netanyahu akaamua afyate mkia. Sasa baraza la mawaziri na uongozi hafifu wa jeshi lao wamekaa, wakaona ili kufuta aibu, ni bora kuivamia Rafah na kumalizia hasira zao huko kwa watoto, kina mama na wazee, ili kuhamisha magoli na kupelekea watu kuanza kujadili kipigo cha Rafah badala ya kile cha Israel kutoka kwa Iran.
Hawa jamaa (Israel) akili ya mipango wanayo, sema akili ya silaha na kijeshi ndo hawana, yani mpaka wapewe na nchi za magharibi.
Baada ya kipigo cha makombora madogo tu yalioshindwa kuzuiwa na nchi zaidi ya 8 zinazojifanya super power duniani, Israel imeamua sasa kujibu kipigo hicho kwa kupanga mipango ya kwenda kuvamia mji wa watoto, wanawake na wazee wasiojiweza ili kuhadaa umma na kuitoa dunia katika ajenda yake iliyoshindwa ya kulipiza kisasi kwa Iran ambalo ni taifa babe, lenye nguvu na uwezo wa kijeshi kuliko taifa lolote huko Mashariki ya kati.
Inasemekana baada ya kipigo cha Iran kwa Israel ambacho kimeleta heshima na utulivu katika eneo hilo, ndugu Netanyahu waziri mkuu wa Israel akataka apate uungaji mkono wa jeshi na silaha kutoka kwa Marekani na washirika wake wengine ili na yeye akajitutumue kubweka kwa watemi wa eneo (Iran) ila washirika wakiongozwa na Marekani wakagoma kutoa jeshi na silaha, wakihofia usalama zaidi wa nchi hiyo (Israel), endapo itataka kuthubutu kuendelea kuvimbishiana misuli na dubwasha (Iran) linaloipa silaha za bure hata Russia ambayo ni super power namba 2 duniani.
Kama wengi tunavyojua kwamba Israel bila Marekani na Uingereza ni sawa sawa na mbwa asiekuwa na meno, kamwe haiwezi kupambana na nchi yoyote mpaka ipate support ya silaha na jeshi. Kwahiyo Netanyahu akaamua afyate mkia. Sasa baraza la mawaziri na uongozi hafifu wa jeshi lao wamekaa, wakaona ili kufuta aibu, ni bora kuivamia Rafah na kumalizia hasira zao huko kwa watoto, kina mama na wazee, ili kuhamisha magoli na kupelekea watu kuanza kujadili kipigo cha Rafah badala ya kile cha Israel kutoka kwa Iran.
Hawa jamaa (Israel) akili ya mipango wanayo, sema akili ya silaha na kijeshi ndo hawana, yani mpaka wapewe na nchi za magharibi.