Israel yamuua Waziri mkuu wa Yemen

Israel yamuua Waziri mkuu wa Yemen

Mstahiki Mea

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2018
Posts
5,581
Reaction score
10,110
#HABARI Waziri Mkuu wa serikali ya Yemen inayoongozwa na Wahouthi na mawaziri wengine kadhaa wameuawa katika shambulio la Israel kwenye mji mkuu Sanaa, mkuu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Houthi amesema jana Jumamosi, likiwa ni shambulio la kwanza la aina hiyo kuua maafisa wakuu.

Wengine kadhaa walijeruhiwa katika shambulio la Alhamisi, Mahdi al-Mashat ameongeza bila kutoa maelezo. Katika taarifa yake ya ijumaa, Israel ilisema kuwa shambulio hilo la anga lilimlenga mkuu wa majeshi wa kundi linalofungamana na Iran, waziri wa ulinzi na maafisa wengine wakuu.

Ahmad Ghaleb al-Rahwi aliteuliwa kuwa waziri mkuu mwaka mmoja uliopita, lakini kiongozi mkuu wa serikali alikuwa naibu wake, Mohammed Miftah, ambaye aliteuliwa Jumamosi kutekeleza majukumu ya waziri mkuu. Rahwi alionekana kwa kiasi kikubwa kama mtu maarufu ambaye hakuwa sehemu ya ndani ya uongozi wa Houthi.

Alikuwa mshirika wa Rais wa zamani wa Yemen Ali Abdullah Saleh, ambaye Wahouthi walimtimua kutoka Sanaa mwishoni mwa 2014 na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa muongo mmoja, lakini baadaye wakaungana na kundi hilo. Yemen imegawanyika kati ya utawala wa Houthi huko Sanaa na serikali inayoungwa mkono na Saudia huko Aden tangu wakati huo.

Tangu vita vya Israel huko Gaza dhidi ya kundi la wanamgambo wa Palestina Hamas kuanza Oktoba 2023, Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran wameshambulia meli katika Bahari Nyekundu kwa kile wanachoeleza kuwa ni vitendo vya mshikamano na Wapalestina.

Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel Katz alisema jana Jumamosi kwamba shambulio hilo lilikuwa ni"pigo kubwa" dhidi ya WaHouth, akiongeza kuwa huu ni mwanzo tu. #EastAfricaTV
 
#HABARI Waziri Mkuu wa serikali ya Yemen inayoongozwa na Wahouthi na mawaziri wengine kadhaa wameuawa katika shambulio la Israel kwenye mji mkuu Sanaa, mkuu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Houthi amesema jana Jumamosi, likiwa ni shambulio la kwanza la aina hiyo kuua maafisa wakuu.

Wengine kadhaa walijeruhiwa katika shambulio la Alhamisi, Mahdi al-Mashat ameongeza bila kutoa maelezo. Katika taarifa yake ya ijumaa, Israel ilisema kuwa shambulio hilo la anga lilimlenga mkuu wa majeshi wa kundi linalofungamana na Iran, waziri wa ulinzi na maafisa wengine wakuu.

Ahmad Ghaleb al-Rahwi aliteuliwa kuwa waziri mkuu mwaka mmoja uliopita, lakini kiongozi mkuu wa serikali alikuwa naibu wake, Mohammed Miftah, ambaye aliteuliwa Jumamosi kutekeleza majukumu ya waziri mkuu. Rahwi alionekana kwa kiasi kikubwa kama mtu maarufu ambaye hakuwa sehemu ya ndani ya uongozi wa Houthi.

Alikuwa mshirika wa Rais wa zamani wa Yemen Ali Abdullah Saleh, ambaye Wahouthi walimtimua kutoka Sanaa mwishoni mwa 2014 na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa muongo mmoja, lakini baadaye wakaungana na kundi hilo. Yemen imegawanyika kati ya utawala wa Houthi huko Sanaa na serikali inayoungwa mkono na Saudia huko Aden tangu wakati huo.

Tangu vita vya Israel huko Gaza dhidi ya kundi la wanamgambo wa Palestina Hamas kuanza Oktoba 2023, Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran wameshambulia meli katika Bahari Nyekundu kwa kile wanachoeleza kuwa ni vitendo vya mshikamano na Wapalestina.

Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel Katz alisema jana Jumamosi kwamba shambulio hilo lilikuwa ni"pigo kubwa" dhidi ya WaHouth, akiongeza kuwa huu ni mwanzo tu. #EastAfricaTV
Si kweli.Mayahudi yameanza "polopaganda" zao.Mtu imara kama yule hauwawi kizembe.
 
Tatizo Israeli inashindwa kujua hata ukiuua Raisi wao,hao jamaa watakuja wengine tu ,maana toka utotoni vizazi vyao vinarisishwa vita!
Hamas wameuua viongozi wao wote lakini bado jamaa wanapumuliwa !
 
#HABARI Waziri Mkuu wa serikali ya Yemen inayoongozwa na Wahouthi na mawaziri wengine kadhaa wameuawa katika shambulio la Israel kwenye mji mkuu Sanaa, mkuu wa Baraza Kuu la Kisiasa la Houthi amesema jana Jumamosi, likiwa ni shambulio la kwanza la aina hiyo kuua maafisa wakuu.

Wengine kadhaa walijeruhiwa katika shambulio la Alhamisi, Mahdi al-Mashat ameongeza bila kutoa maelezo. Katika taarifa yake ya ijumaa, Israel ilisema kuwa shambulio hilo la anga lilimlenga mkuu wa majeshi wa kundi linalofungamana na Iran, waziri wa ulinzi na maafisa wengine wakuu.

Ahmad Ghaleb al-Rahwi aliteuliwa kuwa waziri mkuu mwaka mmoja uliopita, lakini kiongozi mkuu wa serikali alikuwa naibu wake, Mohammed Miftah, ambaye aliteuliwa Jumamosi kutekeleza majukumu ya waziri mkuu. Rahwi alionekana kwa kiasi kikubwa kama mtu maarufu ambaye hakuwa sehemu ya ndani ya uongozi wa Houthi.

Alikuwa mshirika wa Rais wa zamani wa Yemen Ali Abdullah Saleh, ambaye Wahouthi walimtimua kutoka Sanaa mwishoni mwa 2014 na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa muongo mmoja, lakini baadaye wakaungana na kundi hilo. Yemen imegawanyika kati ya utawala wa Houthi huko Sanaa na serikali inayoungwa mkono na Saudia huko Aden tangu wakati huo.

Tangu vita vya Israel huko Gaza dhidi ya kundi la wanamgambo wa Palestina Hamas kuanza Oktoba 2023, Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran wameshambulia meli katika Bahari Nyekundu kwa kile wanachoeleza kuwa ni vitendo vya mshikamano na Wapalestina.

Waziri wa Ulinzi wa Israel Israel Katz alisema jana Jumamosi kwamba shambulio hilo lilikuwa ni"pigo kubwa" dhidi ya WaHouth, akiongeza kuwa huu ni mwanzo tu. #EastAfricaTV

Asalaleeeeeeeeeeh..... Hawa jamaa wakimtaka demu hawamkosi.

Webabu Ritz Adiosamigo mwanakulitaka mwanakulipata. Jamaa wameanza tena tujishike vizuri.
 
Wa Houthis ndiyo wanajua maana ya amani kweli ?!.

Myu asiye muislaamu hapo mashariki ya kati. Inatakiwa awe na moyo wa ki Yahudi. Vinginevyo huwezi ku survive
Wayahudi hawajui maana ya neno pea
 
Back
Top Bottom