Israel (muuaji)ameupenda zaidi mradi wa mabasi ya mwendo kasi

Stayfar

JF-Expert Member
Jan 11, 2016
1,067
2,222
Ni Mradi ulioanza kwa mbwembwe tukaahidiwa mambo mengi mazuri ikiwepo uzingatiwaji wa muda wa kukaa kituoni, tukawa tukionjeshwa matangazo ya kila kituo, ndani kulikuwa na Camera kuangalia wizi ndani ya bus, kulikuwa na ubao wenye taa, mbele na ubavuni ukionyesha mwelekeo wa gari na muda utakaotumika kufika vituoni, madereva walikuwa smart kwenye Uvaaji uniform hadi uendeshaji. Leo hii imefika mahali tunazitamani daladala zetu tulizikuwa tukiingilia madirishani.

Tumezikumbuka kwa sababu MwendoKasi haizingatii muda, ukikata ticket utakaa si chini ya lisaa kituoni ukisubiri bus lije ambapo hakuna tofauti na tulivyokuwa tukichelewesha kwenye foleni na daladala. Ukiingia ndani ya Mwendokasi ni kusukumana na kukanyagana

Ndani ya Mwendokasi kuona mtu mzima au mtoto akizimia kutokana na kukosa hewa kutokana na msongamano ni kitu cha kawaida kabisa. Ndani ya Mwendo kasi hakuna kutangaziwa vituo tena Kama zilivyokuja Kituoni abiria wamejaa kusubiri bus, dereva anawapita abiria gari ikiwa tupu kabisa, anaamua yeye ni wapi akachukue abiria.

Ndani ya bus la mwendo kasi kuna viti vimetengwa maalum kwa Wazee, wajawazito na Vilema, hakuna dereva anayeelewesha abiria kupisha hawa waliotengewa viti vyao. Madereva wa mabasi haya ni bora wale wa daladala zetu wanaendesha hovyohovyo kama wamebeba magunia ya mkaa au mikungu ya ndizi.

Ndiyo maana nasema Mradi huu unaenda kufa wakati wowote. Ushahidi ni jinsi mabasi mabovu walivyoyajaza vituoni yakiwa yameondolewa hadi matairi. Nenda Kimara, Kivukoni hadi Gerezani yamejazana utafikiri hizo stand ni Garage, hapo wananchi hatujashuhudia kule ndani ya yard yao pale jangwani.

Nitoe ushauri kwa serikali kuwarudishia wamiliki wa Daladala kazi yao. Serikali na Kisena mmeshindwa huu Mradi,hata Kama Kisena yupo Jela, tunajua serikali na yenyewe ni mbia kwenye huu Mradi.

Mnakwama wapi?.
 
Waziri yupo kimya kabisa.Kwenye reli anaongea,,ndege kila siku ipo mdomoni,Vyelezo kwake ndiyo habari ya kumfurahisha Rais,iia Mwendokasi hana habari nao
 
Sababu sisi wenyewe hatuwezi kujisimamia, nafikiri atafutwe mbia(mwenye ufahafu wa hii biashara) kutoka ulaya, yeye amiliki 60% na serikali 40%. Unaweza pata mishahara ya walimu wote kila mwezi kupitia huu mradi tu, Mawazo yangu tu.
 
Hili swaga la Mwandokazi kuna kitu kipo nyuna ya pazia(hidden agenda) ambayo haisemwi ama kwa makusud, bahati mbaya au its planed....

Ukitazama bila kwa upana sana unaona kuwa Lipo jambo kubwa linakuja, hebu jarbu tu kufikri kwa upana mpka leo serikal imezuia magar ya mwendo kasi bandalin kisa kodi( zingatia mradi huu serikal ni mwanahisa49%) kama sijakosea npo Tayar kurekabishwa.

KWA nn wasiruhusu magar yakafanya kazi kisha TRA wakawa wanakata pesa yao kila sk? Hlo nalo linahitaj tamko?au kusoma uchum kwa kiwango cha PhD?

Hebu fikria mfumo wa tiket ulivyo et nchi nzima tunashindwa kuoparate system ya mwendokas? Kad tu za mwendo kasi et zimekwama nazo cjui bandalin cjui uwanj wa ndege!!!

Kunamambo hat kuyawaza t yanatia kinyaa.. KWA nn mladi wa ferry(kigamboni) haujafel?

Mradi huu unakit kipo nyuma!!! NA NIKIKUKubwa sana, more than we think....
 
Tatizo kubwa tulilo nalo ni maintenance. We tizama katika kila jambo either tuwe tumefadhiliwa au tumelianzisha sisi wenyewe, linapokuja swala zima la maintenance kwa ajili ya sustainability ya mradi/ project huwa TUNAFELI VIBAYA SANA.
MUNGU atusaidie tu kwa kweli maana jinsi pesa za WALIPA KODI inavyochezewa huwa naona huruma sio siri.
 
Niliwahi kusema huo mradi ni kipimo tosha cha jinsi mradi wa ndege na reli ya sgr utakavyoishia.

Mkuu unaona mbali sana ,sio kila Mtu anaweza kufikiri hivi ulivyo fikiri.Huu mradi utakufa hata kama Raia wana tegemea Usafiri kufika wanapotaka kufika.

Wamejaza Usalama jazzband huko kutafuta kiini lkn mambo ni yale yale.Huu mradi umegeuka kero na kuongeza Stress za Watu kila wanapofikiria kwenda kuutumia。
 
Tatizo kubwa tulilo nalo ni maintenance. We tizama katika kila jambo either tuwe tumefadhiliwa au tumelianzisha sisi wenyewe, linapokuja swala zima la maintenance kwa ajili ya sustainability ya mradi/ project huwa TUNAFELI VIBAYA SANA.
MUNGU atusaidie tu kwa kweli maana jinsi pesa za WALIPA KODI inavyochezewa huwa naona huruma sio siri.

Miradi mingi ya serikali huwa haiendeshwi kwa ufanisi, mambo ya kuleta uzalendo uchwara kwenye miradi inayopaswa kujiendesha kibiashara ni kosa kubwa. Serikali inapaswa kuendesha miradi kama mbio za mwenge, uchaguzi nk, nje ya hapo ni kutaka kuleta vichekesho tu.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Hili swaga la Mwandokazi kuna kitu kipo nyuna ya pazia(hidden agenda) ambayo haisemwi ama kwa makusud, bahati mbaya au its planed....

Ukitazama bila kwa upana sana unaona kuwa Lipo jambo kubwa linakuja, hebu jarbu tu kufikri kwa upana mpka leo serikal imezuia magar ya mwendo kasi bandalin kisa kodi( zingatia mradi huu serikal ni mwanahisa49%) kama sijakosea npo Tayar kurekabishwa.

KWA nn wasiruhusu magar yakafanya kazi kisha TRA wakawa wanakata pesa yao kila sk? Hlo nalo linahitaj tamko?au kusoma uchum kwa kiwango cha PhD?

Hebu fikria mfumo wa tiket ulivyo et nchi nzima tunashindwa kuoparate system ya mwendokas? Kad tu za mwendo kasi et zimekwama nazo cjui bandalin cjui uwanj wa ndege!!!

Kunamambo hat kuyawaza t yanatia kinyaa.. KWA nn mladi wa ferry(kigamboni) haujafel?

Mradi huu unakit kipo nyuma!!! NA NIKIKUKubwa sana, more than we think....
Umewaza vizuri kabisa mkuu, yaani haiwezekani mambo kila uchao yanaenda hovyo huduma mbovu, magari yanahitilafu kibao halafu hatua za madhubuti zinazochukuliwa yaani ni kimyaaa. Na kingine yale magari hayakuja mapya .Tusipoangalia hata SGR itakuja kuwa majanga bora ya mwendokasi tusubiri.
 
Hili swaga la Mwandokazi kuna kitu kipo nyuna ya pazia(hidden agenda) ambayo haisemwi ama kwa makusud, bahati mbaya au its planed....

Ukitazama bila kwa upana sana unaona kuwa Lipo jambo kubwa linakuja, hebu jarbu tu kufikri kwa upana mpka leo serikal imezuia magar ya mwendo kasi bandalin kisa kodi( zingatia mradi huu serikal ni mwanahisa49%) kama sijakosea npo Tayar kurekabishwa.

KWA nn wasiruhusu magar yakafanya kazi kisha TRA wakawa wanakata pesa yao kila sk? Hlo nalo linahitaj tamko?au kusoma uchum kwa kiwango cha PhD?

Hebu fikria mfumo wa tiket ulivyo et nchi nzima tunashindwa kuoparate system ya mwendokas? Kad tu za mwendo kasi et zimekwama nazo cjui bandalin cjui uwanj wa ndege!!!

Kunamambo hat kuyawaza t yanatia kinyaa.. KWA nn mladi wa ferry(kigamboni) haujafel?

Mradi huu unakit kipo nyuma!!! NA NIKIKUKubwa sana, more than we think....
Well said.....
 
Hamna mradi wa CCM wenye mafanikio.
Ndege Ni hasara, mwendokasi kimeo, yaani shaghalabaga, uwanja wa Taifa ushageuka gofu, Ni aibu
TANESCO nayo haijawahi kupata faida hata mwaka mmoja tangu ianze.

Serikali ya Tz haijawahi kuanzisha mradi wowote wa biashara ukatengeneza faida. ATCL, SGR, TANESCO, MWENDOKASI, POSTA, TTCL, vyote vitategemea ruzuku ya serikali. Usidanganyike na magawio ya kiinimacho. Shirika linatoa gawio la bilioni 100 kwa serikali halafu inaiomba serikali iipatie trilioni 1.
 
Labda niwaambie tu, rais mnamsingizia mengine!!


Huyo makonda mzee wa kiki ameshindwa kufuatilia hizi kero za mwendo kasi za kila siku???

Wakuu wa wilaya mradi unako pita wanashindwa kufuatilia kero za mwendo kasi??



Wakurugenzi wa halmashauri wanao husika na mradi huu wamesha chukua hatua gani???



Wabunge wa eneo la mradi wamesha fanya jitihada gani???



Shida nchi ishakuwa ya kiki tu, hakuna nidhamu na uwajibikaji nje ya makamera, na watu kushinda maofisini wakitumia internet ya ofisi kudownload movies tu!!!!
 
Back
Top Bottom