Is Lowassa still relevant? - I would say "No"

Mkuu MM, ulichokiandika kita-hold water endapo serikali yetu ingekuwa muumini mzuri wa utawala bora.....lakini bahati mbaya sana sivyo ilivyo!!! Kama ujuavyo, serikali ya CCM imejikabidhi yote kwa matajiri ambao sasa wakikohoa tu chama chote kinatikisika. Pengine hii ndio inampa ugumu Kikwete wa kufanya maamuzi magumu ndani ya chama. Kwa sasa chama *cha CCM kinaendeshwa kwa mfumo wa kamari (mfumo wa liwalo na liwe), no objectivity, no integrity, no ethics!!!

Katika mazingira kama haya bado LOWASA ana chances za kucheza karata zake vyema and possibility of*re-bouncing*back still exists!!!
Naweza kupendekeza kuwa Lowassa alikuwa na nafasi ya kujijenga upya baada ya kujiuzulu katika kashfa ya Richmond. Wakati ule alipojiuzulu alikuwa bado na umaarufu wa aina yake na umaarufu ambao ulilazimisha watu kugawanyika pande mbili kumhusu yeye. Nakumbuka walikuwepo watu ambao waliamini kabisa kuwa ni Lowassa aliyemjenga Kikwete na kuwa ni yeye kweli aliyekuwa mashine ya serikali. Maamuzi mbalimbali ambayo yalichukuliwa na serikali kati ya 2006 na 2008 yalimhusisha sana Lowassa kiasi kwamba haikuwa haki kumpa pongezi Kikwete bila kumpa pongezi waziri wake mkuu.

Anguko lake lilikuja kwenye suala la Richmond kama wengi tunavyojua. Nimerudi kuangalia mara kwa mara maelezo yake kwenye mahojiano yake na TVT (yanapatikana kwenye mwanakijiji's Channel - YouTube) na kumsikiliza zaidi ya mara hamsini sasa. Jinsi alivyolishughulikia suala lile hata kama ilikuwa ni kwa nia nzuri kiasi gani isingeweza kukubalika kwani alijipa madaraka ambayo hakuwa nayo. Na zaidi ni uamuzi wake wa kujiuzulu (kuzira) Uwaziri Mkuu kwa mtindo alioufanya ambao kwa kweli wengine japo tulitarajia lakini tulitarajia uwe ni kujiuzulu kwa kuwajibika siyo kwa kuzira.

Sasa kuanzia wakati ule wa kujiuzulu naamini umekuwa ni wakati wa majuto kwani yumkini amebakia kufikiria mara 1001 jinsi ambavyo angeweza kujitetea pale Bungeni bila kulazimika kujiuzulu. Siwezi kushangaa kuwa kama kuna majuto aliyonayo Lowassa ni jinsi alivyojiuzulu kwa haraka ili kuwapata kile alichokiita "a wish" ambayo wabaya walikuwa wanataka yaani "uwaziri mkuu". Nakumbuka maneno yake kuwa "I'm going to grant it".

Sasa, aliamua siyo tu kuzira lakini kuzira kabisa na mambo mengine. Ni wazi aliumizwa sana na tukio lile na watu waliokuwa karibu yake nao waliumia pamoja naye. Na wengi wameendelea kuonesha uaminifu kwake. Wamesimama naye na wameenda naye jangwani na hatimaye wamekuwa na matarajio kuwa wanaweza kurudi naye kwenye nchi imiminikayo maziwa na asali.

Tatizo ni kuwa Lowassa hawezi kurudia utukufu uliokwisha ondolewa. Alikuwa na nafasi ya kuurudia kama angefanya maamuzi sahihi baadaye. Na atakuwa na wakati mgumu zaidi kama atajikuta anachukuliwa hatua yoyote na Chama chake. Usalama wake ni kuweza kuzuia mashambulizi na kurudisha mashambulizi. Lakini endapo atajikuta anapewa "karipio kali" au uamuzi wowote adverse dhidi yake utakuwa ni mwisho wa nyota ya kisiasa ya Lowassa. Sidhani kama atakuwa na nafasi yoyote ya maana nje ya CCM. Isipokuwa kama ataweza kuondoka kweli na wabunge wengine ndani ya CCM ambao wanamtii na hivyo kusababisha a semi-parliamentary election.

Could Lowassa be a "come back kid"? I don't think so. Could he be a reckoning force? labda ndani ya CCM. Is he relevant for the political future of the country. AN EMPHATIC NO.
 
Maji yakishamwagika hayazoleki, na majuto ni mjukuu, Lowassa alisha lobber step na ahesabu maumivu
Naweza kupendekeza kuwa Lowassa alikuwa na nafasi ya kujijenga upya baada ya kujiuzulu katika kashfa ya Richmond. Wakati ule alipojiuzulu alikuwa bado na umaarufu wa aina yake na umaarufu ambao ulilazimisha watu kugawanyika pande mbili kumhusu yeye. Nakumbuka walikuwepo watu ambao waliamini kabisa kuwa ni Lowassa aliyemjenga Kikwete na kuwa ni yeye kweli aliyekuwa mashine ya serikali. Maamuzi mbalimbali ambayo yalichukuliwa na serikali kati ya 2006 na 2008 yalimhusisha sana Lowassa kiasi kwamba haikuwa haki kumpa pongezi Kikwete bila kumpa pongezi waziri wake mkuu.

Anguko lake lilikuja kwenye suala la Richmond kama wengi tunavyojua. Nimerudi kuangalia mara kwa mara maelezo yake kwenye mahojiano yake na TVT (yanapatikana kwenye mwanakijiji's Channel - YouTube) na kumsikiliza zaidi ya mara hamsini sasa. Jinsi alivyolishughulikia suala lile hata kama ilikuwa ni kwa nia nzuri kiasi gani isingeweza kukubalika kwani alijipa madaraka ambayo hakuwa nayo. Na zaidi ni uamuzi wake wa kujiuzulu (kuzira) Uwaziri Mkuu kwa mtindo alioufanya ambao kwa kweli wengine japo tulitarajia lakini tulitarajia uwe ni kujiuzulu kwa kuwajibika siyo kwa kuzira.

Sasa kuanzia wakati ule wa kujiuzulu naamini umekuwa ni wakati wa majuto kwani yumkini amebakia kufikiria mara 1001 jinsi ambavyo angeweza kujitetea pale Bungeni bila kulazimika kujiuzulu. Siwezi kushangaa kuwa kama kuna majuto aliyonayo Lowassa ni jinsi alivyojiuzulu kwa haraka ili kuwapata kile alichokiita "a wish" ambayo wabaya walikuwa wanataka yaani "uwaziri mkuu". Nakumbuka maneno yake kuwa "I'm going to grant it".

Sasa, aliamua siyo tu kuzira lakini kuzira kabisa na mambo mengine. Ni wazi aliumizwa sana na tukio lile na watu waliokuwa karibu yake nao waliumia pamoja naye. Na wengi wameendelea kuonesha uaminifu kwake. Wamesimama naye na wameenda naye jangwani na hatimaye wamekuwa na matarajio kuwa wanaweza kurudi naye kwenye nchi imiminikayo maziwa na asali.

Tatizo ni kuwa Lowassa hawezi kurudia utukufu uliokwisha ondolewa. Alikuwa na nafasi ya kuurudia kama angefanya maamuzi sahihi baadaye. Na atakuwa na wakati mgumu zaidi kama atajikuta anachukuliwa hatua yoyote na Chama chake. Usalama wake ni kuweza kuzuia mashambulizi na kurudisha mashambulizi. Lakini endapo atajikuta anapewa "karipio kali" au uamuzi wowote adverse dhidi yake utakuwa ni mwisho wa nyota ya kisiasa ya Lowassa. Sidhani kama atakuwa na nafasi yoyote ya maana nje ya CCM. Isipokuwa kama ataweza kuondoka kweli na wabunge wengine ndani ya CCM ambao wanamtii na hivyo kusababisha a semi-parliamentary election.

Could Lowassa be a "come back kid"? I don't think so. Could he be a reckoning force? labda ndani ya CCM. Is he relevant for the political future of the country. AN EMPHATIC NO.
 
Naona ameshaanza kukutuma kuwaandaa wafuasi wa chadema kumkaribisha rasmi kwenye chama..

Mtakula mapishi yenu, just wait n see

Sio lazima kuchangia kila thridi unaweza kuwa msomaji tu na jinsia yako ya kike isibadilike kuwa ya kiume.
 
Lowassa kwa kifupi atakua rais mbaya kuliko hata Kikwete for:

king of impunity-kwa siasa za kutojuana barabarani atamwajibisha nani katika serikali yake itayojaa marafiki na cronies?hizi mali walizonazo pamoja na wengine kama yeye watawajibishana vipi zaidi ya kulindana na kulinda kasystem kao haka ka ukwapuaji

Corrupt of the corrupt- waziri miaka 5 halafu una mali nyingi wakati haukuwa nazo miaka iliyopita kama ni biashara au mikopo (kama Sumaye) mbona hatujui na haviko wazi? hizi hela za kununua watu anatoa wapi.. kibaya zaidi ni fisadi anayeotesha mizizi ya ufisadi kwa kuchafua kila idara na mamlaka nchini kwa kupachika watu wake na kuhonga wengine ili aongeze nguvu zake binafsi yaani hata tukisema wameiba wengi ndani ya CCM wangapi wanachafua system zaidi ya Lowassa na uchafu wake huu wa kununua kila mtu katika chama na serikali? HAMNA ZAIDI YAKE na hii inamfanya kuwa ni fisadi mchafu kuliko wote (kuna hatari ya kuinstitutionalize corruption hapa Tanzania kama ataunda serikali yake)

Dispositioned arrogance-mzee mwanakijiji umeongea vizuri kusema "alizila" uwaziri mkuu eti kwa kuwa "alionewa" si tume ilimpa muda wa kujitetea na hadi kurudiwa kwa uchunguzi na tume huru mpya? yeye akakimbilia kujiuzulu kwa sababu tume "ilidiriki" kumtaja na spika na Rais "walimtosa" hii ni kujiona uko juu au una umuhimu kuliko wenzako haina tija kwa taifa tunataka mtu confident na arrogant in a +ve way kama MWalimu Nyerere au Moringe Sokoine na siyo huu upuuzi wa kuzila na kulalamika baadae.(huu udhaifu wa sulking and whining ni mzigo kwa taifa maskini) na ndiyo maana anazungukwa na vibaraka wenye uwezo finyu sana kuliko yeye ili ajione mkuu zaidi ili naliweka chini

A leader among the weak-crew yake haileweki ina malengo gani ya kitaifa zaidi ya kutekelza maagizo yake binafsi na hivyo kuonekana ni dhaifu

Overly ambitious and poor tactician- kujiwekea matarajio na kuyafikia ni vizuri lakini ukiyaweka mbali sana kuliko uwezo na mbinu mbovu ni uharibifu mkubwa wa maisha. angejiuzulu humbly bila vijembe wala kunuia vita ya chini chini kuwaharibia wengine, chama na serikali hadi kufika kila kukicha jambo lolote baya watu wanamfikiria yeye. angetulia kushirikiana na waengine na kujiuza vizuri hii vita inamcost.

Extremely self-interested individual-kwa ufisadi, na uroho wa madaraka..kama maelcela alikua na uroho wa madaraka hadi nyerere akamtungia kitabu na kutuambia tumuogope kama ukoma namuona baba wa taifa akirudia hilo hilo kwa mh lowassa kama angekua hai
 
Watu wanasahau tu kuwa hata EL akiingia madarakani allegiance yake ya kwanza itakuwa kwa wale waliomsaidia kuingia madarakani na kusimama naye. Atakuwa na mtandao square. Kitakachokuwa ni marudio ya utawala wa Kikwete na CCM haitakuwa na amani bado. Wenyewe wanasema Lowassa is not a unifying figure but a polarizing one...
 
Watu wanasahau tu kuwa hata EL akiingia madarakani allegiance yake ya kwanza itakuwa kwa wale waliomsaidia kuingia madarakani na kusimama naye. Atakuwa na mtandao square. Kitakachokuwa ni marudio ya utawala wa Kikwete na CCM haitakuwa na amani bado. Wenyewe wanasema Lowassa is not a unifying figure but a polarizing one...

Kazi ipo between now and 2015.
 
Watu wanasahau tu kuwa hata EL akiingia madarakani allegiance yake ya kwanza itakuwa kwa wale waliomsaidia kuingia madarakani na kusimama naye. Atakuwa na mtandao square. Kitakachokuwa ni marudio ya utawala wa Kikwete na CCM haitakuwa na amani bado. Wenyewe wanasema Lowassa is not a unifying figure but a polarizing one...
Swali lako la msingi lilikuwa is EL relevant? Ukajibu NO. Nilichelea kutoa maoni yangu ili nisije mhukumu EL bila ya hoja inayosimamia kile ninachokiamini, na yanayoendelea Dodoma sasa yananifungua vema.

Kwanza, nakubaliana nawe kuwa ni irrelevant na hata yeye anafahamu hilo.Tatizo la EL ni ile hali wanasaikolojia wanaiita 'state of denial'. Yeye anaamini kuwa amezaliwa kuwa rais hata kama ni wa Burkina Faso, Lesotho au Tonga na fiji ni lazima awe rais.
Nyerere alipomkataa alidhani ni mtu mmoja na hata watu milioni 30 wanapomkataa bado hatambui hilo! 'state of denial'.

Kwamba anaweza kuwa rais wa nchi hii hilo ni irrelevant, lakini kuna kitu relevant kuhusu EL ambacho hatukipi uzito. EL ame-determine kuwa rais, ni dtermination hiyo ndiyo iliyomfanya akatumia mapesa kuunda mtandao ili muda ukifika naye afike kileleni. Akawa PM na kujitahidi kununua watu wake kwa pesa alizozishuku Nyerere.

Akiwa PM akawa anafanya mambo kwa 'show off' kitu lkilichompatia sifa ya utendaji na ufuatiliaji. Ukweli unabaki pale pale kuwa hakuwa na utendaji wowote zaidi ya kuita wakuu wa wilaya , waganga wa vituo vya afya na walimu kujibu maswali hadharani.
Ni EL aliyekuwa kichaka cha akina RA na wenzake na hana historia ya kutetea masilahi ya umma.

Baada ya anguko kama PM kwa jaziba akijua linafungua njia ya kurudi magomeni na si Magogoni, EL hakukata tamaa. Ni mtu aliye determine na ghafla akajikita kwenye kupanga vijana UVCCM. Akarejea ngazi ya mkoa na kutaka kuwaweka akina Matilda ili kuendeleza mtandao.

Hilo nalo linaonekana kuwa gumu kama tunavyoshuhudia vugu vugu la Arusha hasa UVCCM.
Kashfa ya Richomnd ndiyo inamtia wazimu kufikia ndoto zake. Na kwa hilo anaona yeye ni loser and he has nothing to lose.
Akili yake inamtuma kuwa yeye kazaliwa kuwa Rais na ndiyo maana tunaona kageukia viongozi wa dini zote ili kutafuta pa kutokea. Tunamuona akijihusisha na shugHuli za kuzindua kwaya n.k.

Dodoma ndiko kunaonekana kungehitimisha safari yake na kwa vile ame-determine basi ameamua liwalo na liwe muhimu ni kuwa rais.
Tunaona alivyomuumbua mshirika wake kwa kumtaja katika sakata la Richomnd. Ni JK aliyewahi kusema hajui lolote kuhusu hao akina Richmond na Dowan( hata kutungiwa shairi, sijui mimi sijui'.)
Rekodi zinaonyesha aliwahi kusema hakuna mchezo mbaya Richmond.

Kama angeyasema ya leo ndani ya bunge akiwa PM tungemuelewa, kwa vile ameamua kufa na tai basi akae kimya.
Kitendo cha kumuumbua JK ni ushahidi kuwa EL ame-determine kutumia mbinu yoyote kuwa rais hata kama ni kuliangamiza taifa. Hapa ndipo ninasema bado ni relevant, kwani watu wanaweza kufyekana ili mradi tu yeye awe Rais.

Hata yeye kuungwa mkono na Sumaye ni ushirika wa kikabila kama alivyowahi kusema Ole Naiko kuwa wamasai wanaandamwa. Tunajua si mmasai lakini EL anaweza kuwa Mbondei au Msambaa endapo tu hilo litamhakikishia urais.

EL ana historia chafu sana isiyomruhusu kuwa hata mwenyekiti wa mtaa, bado anaamini kuwa anaweza kuwa rais.
Tatizo ninaloliona na linalonitisha ni jinsi EL anavyoweza kutumia mbinu chafu kuliangamiza taifa ili wae rais.
Kamnukuu JK akiwa Zbar kuwa' ...urais ni majaliwa ya mungu' akionyesha nia yake ya kuwa rais licha ya uchafu alionao .
Hii ni state of denial inayoweza kulivuruga taifa.

Na muhimu zaidi ni kuwa ameweza kuzuia NEC isimtie adabu, ushawishi wa nguvu aliyo nayo ndani ya chama.
Ukiongezea na determination yake huyu si mtu wa kupuuza. Anaweza asiwe rais wa halali lakini akawa rais kwa damu za wanadamu. Huyu ndiye ENL
 
Kwa kweli nimependa yaliyotokea Dodoma kwani yamethibitisha yale ambayo wengine tumehisi kwa muda mrefu. Wanatishana kwa kung'atana sasa wamebaki kutazamana! Atakayepepesa macho kwanza atakiona!
 
Kwa kweli nimependa yaliyotokea Dodoma kwani yamethibitisha yale ambayo wengine tumehisi kwa muda mrefu. Wanatishana kwa kung'atana sasa wamebaki kutazamana! Atakayepepesa macho kwanza atakiona!

MMKJ
Sema tu hivi, EL ndio njia nyeupe 2015, hana mpinzani, the guy is not an ordinary/ average fighter lol.....
 
I would say YES, he is a kingpin wa siasa za ki ccm, just watch out all of his enemies within the party are running undercover!
 
Naweza kusema kuwa Lowasa is still relevant kwa sababu ya mrithi wake Pinda. Tangu Lowasa ajiuzulu tunaona ni jinsi gani Serikali chini ya Pinda imepwaya na imeshindwa kufanya maamuzi mengi madogo madogo ambayo Pinda anayaona kuwa ni mazito,, yes Lowasa is still a hero when it comes to taking difficult and right decisions, the rest remain a mystery...
Nashanga, hakuna aliyejua kuwa Lowassa ni mtendaji mzuri na mchukuaji wa maamuzi magumu mpaka yeye mwenyewe alipojinadi hivyo tena akilenga kumpiga kijembe rafiki yake JK. Kutoka hapo watu wamekuwa kama kasuku ... ana maamuzi magumu...... maamuzi magumu .................................... Ndilo tatizo la nchi hii. Huitaji kazi kubwa kupandikiza mawazo kwenye vichwa vya Wadanganyika.
 
EL atakuwa relevant kama tutakubali Katiba itakayotokana na mswada uliopitishwa na Bunge majuzi. Kama tutaendelea na huo mchakato tutakachokipata ni 'change without change.' Kwa hiyo mgombea wa CCM atendelea kupeta tu kwa sababu hatuwezi kufanya uchaguzi ulio huru na wa haki katika mazingira hayo. Tunayoshuhudia Dodoma ni ushahidi wa nguvu za EL ndani ya CCM. Sichelei kusema kuwa katika CCM EL ana nguvu kumzidi hata Kikwete. Uwezekano wa kupitishwa kuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM ni mkubwa. Salama yetu ni Katiba mpya ambayo ni mpya kweli kweli. Vinginevyo, tumekwisha.
 
EL hafai kabisa kuwa kiongozi wa nchi hii. Siyo mdokozi kama wengine wanavyompamba bali ni kati ya MAFISADI wakubwa wa nchi hii akishirikiana na rafiki yake RA. Jana kwenye NEC, EL alisema kwamba yeye kwenye RICHMOND alikuwa anafanya maelekezo aliyokubaliana na Rais au maelekezo aliyopewa na Rais -Boss wake.

Kwa hiyo ukiangalia swala la RICHMOND utagundua kwamba wote EL na Boss wake la kwao lilikuwa moja. Na kama mnakumbuka Mwakyembe alivyosema bungeni baada ya akina EL kujitetea na kulialia kwamba wameonewa na Tume ya Mwakyembea, Mwakyembe alisimama Bungeni na kusema kwamba kama kuna mtu wamemuonea watowe ushahidi (uthibitisho) na yeye na kamati yake watajiuzulu ubunge au kama hawajaonewa mbona wanalalamika? Vilevile alisema walikuta madudu mengi sana kwenye RICHMOND na kama wangeyasema yote serikali nzima ingeanguka akiwemo na Mkuu wa Kaya. Alisema wametumia busara kutoyasema hayo ili kuepusha machafuko nchini kama serikali nzima ingejiuzulu.

Sababu hii ndiyo inamfanya mwenyekiti wa CCM anasuasua kwenye mkakati wa kujivua gamba aliouanzisha yeye na sasa kesi kishawauzia wasaidizi wake akina Nape (Vuvuzela) na Chiligati. JK hajawahi kufanya maamuzi yoyote makubwa na kuyasimamia.
 
kwa mtazamo tu EL ni Rais Mtarajiwa au Sumaye CDM ikiwa watamsimamisha EL basi tupunguze kasi ya kampain maana Urais ni wetu Slaa atakuwa Rais na Zito waziri Mkuu , kafurila atarudi CDM awe waziri wa Fedha.
 
duhhhhh!!!!!!!!,kazi ipo,ina maana nchi hii haina mgombea mwingine zaidi ya EL?
 
Back
Top Bottom