Mungu ailaze roho ya marehem mahala pema peponi na kama tukitaka kutafakari tutapata dhambi bure iwe kweli au si kweli
Mungu ndo mwenye kujua na wanadamu ni wanyonge na hawana jinsi ya kuamua kufa au kutokufa kwani hata kama unavyosema alikataa kumtoa mama yake je angemtoa hao freemanson wangempa uhai wa kuishi milele? "KUFA NI LAZIMA NA NI HAKI YA KILA KILICHO HAI DUNIANI NA HAKUNA WA KUMNYANG'ANYA MTU/KIUMBE CHOCHOTE HAKI HIYO".
Na naomba kukujuza kuwa hakuna wa kukuzuia kufa hata kama uwe uko freemanson au hauko huko na kukumbuka MUNGU ndo anajua yupi afe lini na wapi na si freemanson na freemanson wenyewe wanakufa je wanakuwa wamekosa nini kuzuiwa na mkubwa wao wasife?"KILA AITWAYE NA MOLA WAKE HUITIKA NA HAKATAI KWANI NI HESHIMA KUITWA NAWE KUITIKA KWA UNYENYEKEVU AWE BINADAMU AU MAJINI"