Iringa: Lowassa akabidhiwa tuzo ya heshima

Haswa

Member
Apr 19, 2013
67
15



Kaimu Meya wa manispaa ya Iringa Vitus Mushi (kushoto) akisalimiana
na waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa baada ya kutua uwanja wa ndege wa Nduli Iringa

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Teresia Mahongo akimpokea Lowassa

Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Iringa mwanahabari Tumain Msowoya akisalimiana na LOwassa

IMG_2091.jpg

;">
kada wa CCM Bw Lazaro akisalimiana na Lowassa


Mfanyakazi wa radio Overscomers Fm Adela kivamba akisalimia na Lowassa

Mbunge wa jimbo la Mufindi Kusini Mendrady Kigola akijitambulisha mbele ya Lowassa


Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akitoa neno mbele ya
Lowassa kwa kuwataka viongozi wa serikali kujisahihisha
kuwa mambo yanavyokwenda sivyo yanavyotakiwa kwenda

Mbunge wa jimbo la Mwibara Kangi Lugola pacha wa Filikunjombe akinena jambo

Askofu wa OPC Iringa Dkt Boaz Sollo akimkabidhi tuzo ya heshima waziri
mkuu mstaafu Edward Lowassa leo katika ukumbi wa St Dominic-PICHA ZOTE NA
FRANCIS GODWIN MZEE WA MATUKIO DAIMA
 
Naona Kiswahili kinanipiga CHENGA wanasema LOWASSA kafunika IRINGA; Sasa sijui kufunika ndio nini... Sababu hata KINANA na NAPE walifunika MOROGORO...

Sijui Wanafunika nini???

** MBONA Anakwenda kwenye DINI hivi? ni wa kuogopa!!!
 
Naona Kiswahili kinanipiga CHENGA wanasema LOWASSA kafunika IRINGA; Sasa sijui kufunika ndio nini... Sababu hata KINANA na NAPE walifunika MOROGORO...

Sijui Wanafunika nini???

** MBONA Anakwenda kwenye DINI hivi? ni wa kuogopa!!!
Sio kwamba anaogopa, bali anatumia dini kama mbeleko ya kumpeleka Ikulu baada ya kubaini kuwa hana sifa hata chembe.
 
Bwana Yesu akaingia hekaluni akakuta wanyang'anyi na majambazi wameligeuza nyumba ya mungu kuwa gulio la kuuzia na kununua bidhaa za wizi akawakemea akawafukuza! Je lowossa kugeuza nyumba za ibaada kuwa sehemu kujitafutitia utakaso kwa WIZI aliyo ufanya kwa watanzania anastahili kupata tuzo au ana sitahili kuombewa ili mungu amsamehe ujambazi wake aliyo ufanya? Je hao wanaoshangilia wanampenda au ni kwa sababu ya tamaa ya pesa ndiyo inawafanya wawe watumwa wa hilo FISADI?
 
Sielewi protokali zipoje...LOWASSA kaja kuchangia kanisa la boaz sasa CCM apa inaingiaje?
 
Waislam wamempa tuzo na pia Wakristo wamempa tuzo ya mchango wake uliotukuka kwa jamii. Lowassa ni chaguo la Mungu. Nani wa kumzuia 2015 urais?
 
Back
Top Bottom