baraka boki
Senior Member
- Sep 20, 2010
- 181
- 80
Basi ilikuwa katikati ya mwezi wa kumi na mbili mwaka jana pale kijana nilipoamua kutembelea maeneo ya jangwani sea breeze nikiwa na wenzangu kama wawili .Wakati nikiendelea kupata starehe ghafla macho yangu yakakutana na Mrembo mmoja basi naye akatabasamu mimi sikuonyesha interest ya kumshobokea wala nikaendelea kupiga story na wenzangu. Lakini baadaye nilipoenda kuoga katika swimming pool nikakutana na yule Mrembo nikamuuliza jina lake anaitwa Irene basi nikapiga naye story kidogo tukaagana na kupeana namba za simu. Basi tukaendelea kuwasiliana kama kawaida huku tukichat whatsApp nikimpigia simu tulikuwa tunaongea kama kawaida .Lakini juzi amenikatia mawasiliano simu apokei na message ajibu sijui kwa nini?.Kwa kuongezea huyu msichana sikumtongoza nilikuwa na buy time kwanza nimzoee kwanza taratibu.Wadau naomba ushauri nifanyaje maana huyu Mrembo amenikatia mawasiliano?