Irene mbona umenichunia kijana mwenzio. ..

Irene mbona umenichunia kijana mwenzio. ..

baraka boki

Senior Member
Joined
Sep 20, 2010
Posts
181
Reaction score
80
Basi ilikuwa katikati ya mwezi wa kumi na mbili mwaka jana pale kijana nilipoamua kutembelea maeneo ya jangwani sea breeze nikiwa na wenzangu kama wawili .Wakati nikiendelea kupata starehe ghafla macho yangu yakakutana na Mrembo mmoja basi naye akatabasamu mimi sikuonyesha interest ya kumshobokea wala nikaendelea kupiga story na wenzangu. Lakini baadaye nilipoenda kuoga katika swimming pool nikakutana na yule Mrembo nikamuuliza jina lake anaitwa Irene basi nikapiga naye story kidogo tukaagana na kupeana namba za simu. Basi tukaendelea kuwasiliana kama kawaida huku tukichat whatsApp nikimpigia simu tulikuwa tunaongea kama kawaida .Lakini juzi amenikatia mawasiliano simu apokei na message ajibu sijui kwa nini?.Kwa kuongezea huyu msichana sikumtongoza nilikuwa na buy time kwanza nimzoee kwanza taratibu.Wadau naomba ushauri nifanyaje maana huyu Mrembo amenikatia mawasiliano?
 
Rudi tena Jangwani...au hamia White Sands, Giraffe, Belinda n.k huenda utampata huko...

Pia kama una namba yake ya simu maana yake unaweza kujua jinale kamili, tumia jina hilo kumsaka mitandao ya kijamii ka FB n.k
 
ndo jamii forum ilipofika sasa....mwingine msichana akicheka atakuja kuuliza mbona mrembo wangu anacheka nifanyeje...?
 
Hv siku hiz wanafunzi hawafui na kunyoosha nguo za shule jumapili?

Shule si zinafunguliwa kesho au mpk tar 15?
 
wala usiikurubie zina hakika zina ni uchafu na njia mbaya(quran 17:32)
 
Irene wa kwanza alining'ata kidole shule ya msingi,wa pili alinisingizia mimba,wa tatu alivunja kioo cha gari nikiwa nimempakia shem wangu akijua ni demu wangu,wa nne kanifukuza kazi...wote irene hawa...samahani lakini,ni kumbukumbu binafsi hazihusiani na uzi huuuu
 
ndo jamii forum ilipofika sasa....mwingine msichana akicheka atakuja kuuliza mbona mrembo wangu anacheka nifanyeje...?

Mkuu we acha tu watu wanapost vitu vya ajabu sana..
 
Back
Top Bottom