Usije ukarogwa hata siku moja kuamini kuwa kuna nchi itaifuta Israel kwenye uso wa dunia. watashangaa kuona wao ndio wanabaki magofu.
Jamani tujifunze kusoma between the lines na hii sio personal attack kwako mkuu
Hute .
Israel ina mabomu ya nyuklia zaidi ya 300, wana jeshi kabambe (nadhani ni la tatu au la nne kwa uwezo duniani), wana wafadhili wenye nguvu sana kama Marekani, Uingereza watakaowasaidia kijeshi au kwenye security council ya umoja wa mataifa. Kwa hiyo Israeli haiwezi kufutwa kijeshi hata siku moja.
Lakini Israel (kama a zionist nation) inaweza kufutika na nafikiri itafutika - na hiki nadhani ndicho wanachosema waIran.
Chukulia mfano mdogo wa hapa kwetu Afrika.
Afrika ya kusini ilikuwa ni
Apartheid Nation. Wale wenye nchi (weusi) na wale wenye mchanganyiko na weusi (colored) hawakufurukuta chini ya utawala wa makaburu. Lakini
international pressure ilipopanda na kuisusia Afrika ya kusini, uchumi ukawa unayumba na weupe wakakubali kwamba weusi ni sawa na wao na wanaweza kupiga kura.
Well, democracy is a bi-tch. Kutokana na wingi wa weusi, uchaguzi huru wa kwanza Africa kusini was not even a contest. Mandela alibeba karibuni kura zote. Sasa hivi weusi wako madarakani. Wanaweza wakawa wanajikanyaga na utawala wao mbovu lakini
SOUTH AFRICA IS NO LONGER AN APARTHEID REGIME controlled na makaburu kisiasa. Weusi wanatawala.
WaIsrael saa nyingine wanakuwa too clever by half. Babu yangu alikuwa anapenda sana msemo huu:
AKILI NYINGI HUPUNGUZA MAARIFA. Yafuatayo ni maelezo yanayofafanua usemi wangu huu.
Kutokana na International Law ya leo (UN-resolutions) ile nchi iliyokuwa Palestina hadi 1948 itagawiwa sehemu mbili kufuatia mipaka ya 1967. Sehemu moja itakuwa taifa la Israel na nyingine itakujakuwa taifa la Palestina. Sasa kwa sababu waIsrael hawakuwa na nia ya kuwapa waPalestina hii sehemu yao basi wamejenga na wanaendelea kujenga makazi yao kwenye haya maeneo ya waPalestina kwa mabavu.
Sasa hivi eneo lililobaki ni dogo sana na limekatwa vipande vipande kiasi cha kutoweza ku-establish taifa (contiguous state) la waPalestina. Kwa hiyo sasa hivi ile suluhu ya nchi mbili -
Palestina na
Israel haiwezikani tena. The only viable solution ni kuwafanya waPelistina wote (Gaza na West Bank) kuwa raia wa Israel na kuwe na nchi moja tu (sijui itaitwaje). Hiki kikitokea mchezo umekwisha.
Kwa kuwa waPalestina ni wengi kuliko waIsrael, na kama bado watajiita democracy, basi uchaguzi ukitokea lazima mPalestina atashinda kama
Prime minister wao. Hii itakuwa ukomo wa
Israel kujiita a Jewish/Zionist state. Yale yale ya Afrika kusini. Lakini ili hiki kitokee ni lazima dunia iisusie Israel (kama walivyowasusia Afrika kusini chini ya makaburu). Nadhani hii ndio maana ya maneno
"ISRAELI ITAFUTWA KWENYE RAMANI YA DUNIA".
I may be wrong - I am just saying.