Yusomwasha
JF-Expert Member
- Dec 5, 2014
- 2,092
- 844
Mkuu wa kuainisha maslahi ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kuwa Iran itaifuta Israel kwenye ramani ya dunia na hilo halina kipingamizi. Ameongeza pia kuwa Israel si taifa na hivyo linapaswa kuondolewa. Amesema kwamba Israel imefanya njama ya kuzuia mazungumzo ya nyuklia yasifikiwe lakini mazungumzo yamepata mafanikio makubwa.
Mazungumzo ya nyuklia yanatarajiwa kufikiwa leo ambapo Iran itaendelea kuzalisha nyuklia kama kawa na vikwazo vyote kuondolewa. Israel imetishia kuishambulia Iran kijeshi endapo mazungumzo yatafanikiwa.
Pia Rafsanjani amewataka watu duniani kote kujitokeza siku ya kimataifa ya quds ambayo ilianzishwa na Iran kwa lengo la kutetea Palestina.
Source: Radio Tehran
Mazungumzo ya nyuklia yanatarajiwa kufikiwa leo ambapo Iran itaendelea kuzalisha nyuklia kama kawa na vikwazo vyote kuondolewa. Israel imetishia kuishambulia Iran kijeshi endapo mazungumzo yatafanikiwa.
Pia Rafsanjani amewataka watu duniani kote kujitokeza siku ya kimataifa ya quds ambayo ilianzishwa na Iran kwa lengo la kutetea Palestina.
Source: Radio Tehran