Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Si hoja ya kikatiba Wala ya kisheria ni hoja ya fikra juu ya utekelezaji wa Yale ambayo hayajaandikwa na si kwamba yalisaulika kuandikwa bali ni magumu kuyaweka kwenye makaratasi.
Hakuna sehemu Katiba wala sheria inaposema wakuu wa vyombo wabadilishane kutoka na pande mbili za Muungano. Aidha hakuna sehemu ilipoandikwa Rais akitoka bara Makamu atoke Zanzibar ila tamadumu zimezoea kuweka usawa wa Muungano kwenye teuzi na chaguzi.
Kwa muktadha huo naomba kujua kwanini Wazanzibar ni wachache sana kwenye vyombo vya ulinzi hasa nafasi zinazotokana na uteuzi wa Rais?
Je si wakati muafaka sasa Mama Samia anapokwenda kupangua viongozi wa vyombo vyetu akateua baadhi ya wakuu wa taasisi hizi kutoka Zanzibar?
Jana nilifungua mjadala wa nafasi ya wanawake kwenye majeshi yetu, Leo nafungua mjadala wa nafasi ya Zanzibar kwenye uteuzi wa wakuu wa vyombo. Nafungua mjadala huu baada yakuona top officials wa vyombo vyetu wanatoka bara. Sijui wazenji labda mwamko wao kwenye vyombo ni mdogo au tatizo ni uwezo?
Tuone polisi chini ya Mzenji, Uhamiaji chini ya Mzenji, TISS chini ya Mzenji, JW pia.
Tunapojadili hoja Kama hizi zinatusaidia kujua aina ya mawazo ya kwenda nayo kwenye Katiba mpya endapo tutapata hii fursa. JF iwe moja ya sehemu zakuchukulia hoja za kitafiti kuijenga Tanzania tuitakayo.
WERIKAMU
Hakuna sehemu Katiba wala sheria inaposema wakuu wa vyombo wabadilishane kutoka na pande mbili za Muungano. Aidha hakuna sehemu ilipoandikwa Rais akitoka bara Makamu atoke Zanzibar ila tamadumu zimezoea kuweka usawa wa Muungano kwenye teuzi na chaguzi.
Kwa muktadha huo naomba kujua kwanini Wazanzibar ni wachache sana kwenye vyombo vya ulinzi hasa nafasi zinazotokana na uteuzi wa Rais?
Je si wakati muafaka sasa Mama Samia anapokwenda kupangua viongozi wa vyombo vyetu akateua baadhi ya wakuu wa taasisi hizi kutoka Zanzibar?
Jana nilifungua mjadala wa nafasi ya wanawake kwenye majeshi yetu, Leo nafungua mjadala wa nafasi ya Zanzibar kwenye uteuzi wa wakuu wa vyombo. Nafungua mjadala huu baada yakuona top officials wa vyombo vyetu wanatoka bara. Sijui wazenji labda mwamko wao kwenye vyombo ni mdogo au tatizo ni uwezo?
Tuone polisi chini ya Mzenji, Uhamiaji chini ya Mzenji, TISS chini ya Mzenji, JW pia.
Tunapojadili hoja Kama hizi zinatusaidia kujua aina ya mawazo ya kwenda nayo kwenye Katiba mpya endapo tutapata hii fursa. JF iwe moja ya sehemu zakuchukulia hoja za kitafiti kuijenga Tanzania tuitakayo.
WERIKAMU