Swali wadau: Huyu Juma Mwapachu na Bakari Mwapachu wana undugu wa aina yeyote?
MIAKA 50 iliyopita, Septemba 17, mwaka 1962, Hamza Kibwana Bakari Mwapachu, baba yake na Harith Bakari Mwapachu, Rahma Mwapachu, Juma Volter Mwapachu, Wendo Mtega Mwapachu, Tunu Mwapachu na Jabe Jabir Mwapachu, alifariki dunia mkoani Dar es salaam. Alifariki katika umri mdogo wa miaka 49, wakati huo alikuwa Katibu Mkuu Msaidizi katika Wizara ya Mambo ya Ndani.
Akiwa amezaliwa Tanga, marehemu Hamza alisoma elimu yake ya shule ya msingi na sekondari mkoani Tanga baada ya darasa la nne, wakati huo ikiwa ni elimu ya sekondari ya kiwango cha juu Tanganyika.
Baada ya hapo alisomea mafunzo ya utabibu, katika Shule (Hospitali) ya Uganga ya Sewa Haji, mkoani Dar es Salaam na kuhitimu cheti cha mganga msaidizi, mwaka 1935. Mwaka 1937 alipelekwa kuwa mwalimu wa shule ya uganga mkoani Mwanza iliyokuwa ikifundisha wafanyakazi wasaidizi wa uganga. Akiwa Mwanza alikutana na Juliana Volter ambaye alifunga naye ndoa mwaka 1938.
Akiwa mwenye malengo makubwa ya kufanikiwa, alijiunga na Chuo cha Makerere, mwaka 1943 kusomea stashahada ya udaktari. Wakati huo, Makerere hawakuwa wakitoa shahada ya aina yoyote.
Kama historia ilivyojionyesha, Hamza na Julius Nyerere walijiunga na Chuo cha Makerere wakati huo na kuanzisha safari yao ya urafiki wa karibu pamoja na uhusiano kisiasa, bila kujali tofauti ya umri wa miaka tisa kati yao.