Ipi ilikuvutia enzi hizo?

Ipi ilikuvutia enzi hizo?

mqdefault.jpg


Ni sheeda aise
 
picha za zamani ni za zamani tu hizo sasa hivi siziangalii nipo na James bond na kama hizo eti mtu mmoja anaua watu mia
shenzz kabisa eti ndio komando kipensi nachukia nilikuwa nadanganywa

Kule kudanganywa ndio ulikuwa uhondo wenyewe, nilikuwa naacha hadi kula siku kibanda umiza wakionyesha muvi za the hard way, no retreat no surrender, super ninja ya alexander low, inter the dragoni n.k muvi za kiindi ndio kabisaa unapita Avalon pale unasoma kava then mtaani unasimulia utafikiri umeiona
 
delta_force-1986.jpg

Hili picha sio mchezo Norris pikipiki yake inatema sana makombora, mbele na nyuma. Ndani ya Beirut hiyo Norris na wenzake wanaenda kuwaokoa mateka. Wakina Mama wote wanaachiwa na Magaidi, Magaidi wanabaki na wakina baba.

Ebwana hili picha sio mchezo na kile kinanda Norris kila akifanya mashambulizi kinanda nacho kinasindikiza
 

Attachments

  • MV5BMTUzMzg4MTg2M15BMl5BanBnXkFtZTYwNDM4OTk4._V1_SX300.jpg
    MV5BMTUzMzg4MTg2M15BMl5BanBnXkFtZTYwNDM4OTk4._V1_SX300.jpg
    12.1 KB · Views: 171
51VFW%2BxwMWL._SX200_.jpg

Hili picha sio mchezo Damme akiwa jeshini anaomba ruhusa ya kwenda kuhudhuria msiba wa mkewe cha ajabu jeshini wanamkatalia inabidi Damme atoroke jeshini kuhudhuruia mazishi. Baada ya kufanikiwa kutoroka Damme akiwa mtaani anakutana na Mniga(Kigulu) anakuwa rafiki yake wa karibu tatizo Kigulu akawa anamtumia Damme awe anaenda maukumbi ya kupigana ili apate pesa za kuwekeana dau(kamali) nje. Na Damme alikuwa anawatandika sana.

Kigulu anavyopenda upambe inafikia kumlazimisha Damme akutane na Mama mmoja tajiri sana amdhamini Damme kwenye mapambano
 
Daaaa enzi hizo kwa bolingo...yaani kuanzia ghana,majengo,mbata,sokomatola,nonde,machinjion, itiji,mabatini,simike mpk ushuani jacaranda kucheki muvi ni kwa bolingovtu
 
arnold-schwarzenegger-commando.jpeg

Komando John na mwanae Jenny. Hili picha ni hatari sana nalipenda mno.

Komando John anapewa amri na Magaidi ya kwenda kumuua Rais wa kisiwa fulani(jina la kisiwa silifahamu). Anapewa amri hiyo chini ya sharti moja ambalo amuue huyo Rais huku wao Magaidi wakiwa wanamshikilia Jenny(binti wa Komando John) na ili Komando John ampate binti yake lazima atekeleze sharti. Kitu kilichomlazimu Komando John atekeleze amri ya Magaidi, wakamkatia tiketi Komando John wakampa na msindikizaji mmoja ambae atakuwa nae safarini mpaka atakapofika hapo kisiwani.

Komando John ile bomba linaanza kunyanyuka akata aende chooni wahudumu wa kwenye bomba wakamzuia ikabidi atulie kwanza, ikabidi Komando John aombe mto na Blanket kutoka kwa muhudu, muhudumu akamletea mto na Blanket, Komando John alichofanya akamnyonga shingo(msindikizaji) akamuegamisha na mto kisha akachukua blanket akamfunika kwa utulivu akalishusha na Kofia(pama la msindikizaji) kwenye paji la uso. Kisha Komando John akamuomba muhudumu "tafadhali rafiki yangu amechoka sana kwahiyo msimsumbue mwacheni apumzike".

Baada ya hapo Komando John akaingia chooni akapachua pachua akafikia kwenye mizigo akaendelea kupachua pachua hadi akafika lilipo tairi la ndege kisha Komando John akajirusha huku bomba likiwa hewani akaangukia kwenye kibwawa.

Nitajaza ukurasa hili picha tamu sana, ngoja niishie hapa
 
ushawahi kukutana na changamoto za deki chafu, au kuna kipande mkanda hauonyeshi...
Bila shaka mlikuwa nacho kidubwasha cha kuriwaindia mikanda ili msiichoshe deki. Tena mnapewa na amri na wazazi kama wanaondoka na kuwaacheni peke enu mnasisitizwa kanda zenu mkiriwaindi tumieni kidubwasha hicho. Maisha haya
 
Back
Top Bottom