Ipi ilani bora Kati ya CCM na UKAWA

Ipi ilani bora Kati ya CCM na UKAWA

Mfano Mahakama ndipo penye tatizo kubwa hapo panafaa pamulikwe kwa kufanya kazi kuanzia saa moja asubuhi hadi saa kumi na moja jioni wafanye kazi hadi jumamosi, mahakimu wawe wanachunguzwa nyendo zao kuwepo na kitengo cha Usalama kwenye Mahakama zote ili Haki zitendeke kukiwa na Haki popote maendeleo yatakuja kwa kasi kwani magumashi ni Adui wa Haki.

Jambo jema ndugu coz tunaitaji maendeleo kwa Tanzania yetu
 
Ilani Bora ni ile Yenye Vipaumbele Vichache Vinavyotekelezeka upande mmoja na upande wa pili vyenye kuweza kugusa maeneo mtumbuka ya jamii yetu. WINGI WA VIPAUMBELE NI SAWA NA HAKUNA KIPAUMBELE, HAKUNA NIA DHABITI.

Ilani inayoangalia mahitaji ya maisha ya mwananchi na hasa katika shida ya makazi bora na hivyo kushinikiza uwekezaji katika sekta ya ardhi/nyumba inaweza zaidi kulipeleka taifa mahali pengine kwani itaongeza ajira na kuboresha mazingira ya kuishi hivyo kupunguza maradhi, itachochea utumiaji wa taaluma zote na hivyo kuchochea tija kwa elimu na mwisho wa siku kupigana na ujinga na njaa.

Ilani Mbaya ni ile iliyojengwa kwenye misingi ya kudhani taifa linaweza kustahimili ujenzi wa barabara kila mahali kwa sababu tu watu wanataka! Au kuhakikisha dawa hospitali za serikali kwa kuwa kwa sasa hivi faramsia binafsi zina dawa hali hospitali za uma hazina. Ilani za kuibagua sekta binafsi ni mufilisi.

Ilani bora ni ile inayoona taifa kwa mwono wa sisi sote kushiriki katika maendeleo, kukubali kuna maeneo ambayo yatasubiri mengine - yale yenye nafasi yawekeze na kupata ziada ambayo tutaitumia kwa yale ambayo hayakujaliwa malifhafi asilia...sio ya kudhania kuna Kaskazini na Kusini au vingine.

Ni kweli kabisa ndugu Kwani bila ushiriki wetu kwa pamoja hatuwezi kuwa na maendeleo genge tija
 
Mi katika ilani zote nashukuru wamezingatia elimu ingawa kwa namna tofauti ila ni Jambo jema Kwani elimu ndio ufunguo wa maendeleo
 
Umoja wa vijana wameporwa Tenda na Ruge wa clouds wameamua kususa lakini wenzao waliompa Tenda sasa wameshiba baada ya Ruge kuwamegea chao cha juu kwa kufanikisha Dili

ha ha ha mwisho wa siku kitaeleweka tu
 
Nawaomba wadau tutumie nafasi hii kufanya maamuzi ya busara kuliko kipindi chochote
 
ya ccm haina maana tena kwani hawaminiki, waliwahidi waislam then wakawatapeli , hawakuileta wakawazungusha, hivyo yao ni sawa karatasi ya gazeti hatuna haja nayo.
ya ukawa hata ikiwa ina mapungufu itarekebishwa kila tukisonga mbele
 
Wadau tunapoenda kwenye uchaguzi hebu tukubaliane kwa pamoja tuweke ushabiki pembeni kwa maslahi ya taifa letu. Ni ILANI IPI YENYE UBORA? Kati ya hizi mbili zipitie kisha toa jibu lako



Ilani haitusaidii kuitoa CCM madarakani. Ilani nzuri ni ya chama cha Jahazi lakini mwaka huu ni wa UKAWA na rais ni Lowasa. Ilani zitatusaidia nini wakati watekelezaji ni wale wale kwa sheria zile zile na ndio maana hata CCM hawahubiri ilani zao zaidi ya kusema yale yale waliyoyatangaza miaka nane iliyopita kuwa Lowasa ni Fisadi na wakashindwa kuitekeleza kwa kumkamata.

Sasa mwaka huu tunamtaka Lowasa waliyemshindwa ili yeye awakamate wao na kuwaaibisha kwa uongo wao.
Mwaka huu ni mwaka wa wanyonge waliopigwa mabomu na kudhalilishwa na waafrika wenzao kwenye taifa lao wote kwa kupitia mgongo wa CCM.

Tumeona Makonda na Nape a
Wakizawadiwa vyeo kwa kutukana na kudhalilisha wengine.
Huu ni mwaka wa kuleta usawa na utu. Kuwaachia wale waliodhulumiwa .
Mwaka wa kumwondoa mkoloni mweusi aliyeua na kutesa kwa miaka 50 ameleta madaraja kwa watanzania kwa muda mrefu. CCM ni tatizo kubwa hatubitaji sera tunataka Elimu bora kwa watoto wetu. Kama sio elimu dunia isingekua kijiji kwa Teknolojia . Wao CCM wanawekeza familia zao kwenye Elimu na mali lakini wanatuletea sera za kupambana na waiba madawa wakati wakuu wa sekta hizo ni watoto wao waliosoma. Bila Elimu hakuna maendeleo zaidi ya mabwana na watwana. Magufuli kwa kujua umuhimu wa Elimu alisoma tena akiwa waziri na kupata phd. Leo anadharau kipaumbele cha elimu.

Usawa kwanza sera baadae.
UKAWA na Lowasa ndio ukombozi na raha ya malofa oktoba kupumua.
Tunataka mtu wa kuunganisha watu sio kutugawa kwa makundi kwa manufaa ya CCM.
Ushindi wa Lowasa ni ushindi wa vyama vyote na watanzania wote.
Ushindi wa magufuli ni ushindi wa kakikundi kadogo ka watu ndani ya CCM kwa manufaa yao na familia zao kwa mgongo wa chama.
Tumeshtuka hatuichagui CCM wala Magufuli wala wabunge wao na madiwani wao.
 
Ilani bora iko ACT WAZALENDO PEKEE KWINGNE NI NPROPAGANDA TU, TAIFA KWANZA LEO NA KESHO!
 
ccm porojo kibao ilan ya chadema ina vpaumbele 6 ya ccm viko zaid ya ishirini
 
Dont read too much in an election manifesto!!!! Ilani ni kabrasha tu, maandishi ya kitaalamu ambayo kama hakuna nia ya makusudi ya utekelezaji haina maana YOYOTE! Kitu cha kuangalia hapa ni utashi wa kisiasa, dhamira safi na utii kwa umma wa kuyatekeleza yaliyoainishwa katika ilani hiyo. Kwa hiyo kwa kigezo hicho Mimi naipa "benefit of the doubt" ilani ya UKAWA kwa sababu they have everything to loose wasipoonyesha dhamira ya kuitekeleza kwa sababu wanatafuta kuaminiwa na wananchi tofauti na CCM ambao wamepata nafasi hiyo kwa miaka 50 iliyopita lakini kwao ni business as usual, bora liende, watatufanya nini?! Hawajisikii tena kuwajibika kwa wananchi, so they don't have to do anything to stay in power! Madarakani ni haki yao! Absolute power corrupts absolutely!

Wadau tunapoenda kwenye uchaguzi hebu tukubaliane kwa pamoja tuweke ushabiki pembeni kwa maslahi ya taifa letu. Ni ILANI IPI YENYE UBORA? Kati ya hizi mbili zipitie kisha toa jibu lako
 
Dont read too much in an election manifesto!!!! Ilani ni kabrasha tu, maandishi ya kitaalamu ambayo kama hakuna nia ya makusudi ya utekelezaji haina maana YOYOTE! Kitu cha kuangalia hapa ni utashi wa kisiasa, dhamira safi na utii kwa umma wa kuyatekeleza yaliyoainishwa katika ilani hiyo. Kwa hiyo kwa kigezo hicho Mimi naipa "benefit of the doubt" ilani ya UKAWA kwa sababu they have everything to loose wasipoonyesha dhamira ya kuitekeleza kwa sababu wanatafuta kuaminiwa na wananchi tofauti na CCM ambao wamepata nafasi hiyo kwa miaka 50 iliyopita lakini kwao ni business as usual, bora liende, watatufanya nini?! Hawajisikii tena kuwajibika kwa wananchi, so they don't have to do anything to stay in power! Madarakani ni haki yao! Absolute power corrupts absolutely!
nimekusoma ndugu thanx for dat
 
  • Thanks
Reactions: MTK
swala la kutekeleza hatuwezi kujua coz hawajaweza pewa nchi kuliko ccm ambao kwa miaka hamsini hazitekelezeki
kama ccm wamepewa kwa miaka 54 na nne utekelezaji ni hafifu inabidi tubadili chama kama magufuri mwenyewe anavyofanya pindi mkandarasi anaposhindwa kutekeleza majukumu yake, humfukuza na kuweka mkandarasi mwingine anayemwamini kuwa atafanya kazi vizuri zaidi
 
Back
Top Bottom