Ipi ilani bora Kati ya CCM na UKAWA

Ipi ilani bora Kati ya CCM na UKAWA

msubhe

JF-Expert Member
Joined
Nov 11, 2014
Posts
225
Reaction score
32
Wadau tunapoenda kwenye uchaguzi hebu tukubaliane kwa pamoja tuweke ushabiki pembeni kwa maslahi ya taifa letu. Ni ILANI IPI YENYE UBORA? Kati ya hizi mbili zipitie kisha toa jibu lako
 
Wadau tunapoenda kwenye uchaguzi hebu tukubaliane kwa pamoja tuweke ushabiki pembeni kwa maslahi ya taifa letu. Ni ILANI IPI YENYE UBORA? Kati ya hizi mbili zipitie kisha toa jibu lako

UKAWA siyo chama hi yo hawana Ilani! CDM haijaandaa ilani hivyo huwezi linganisha vitu ambavyo havipo. Subiri water ilani Yao.
 
Wadau tunapoenda kwenye uchaguzi hebu tukubaliane kwa pamoja tuweke ushabiki pembeni kwa maslahi ya taifa letu. Ni ILANI IPI YENYE UBORA? Kati ya hizi mbili zipitie kisha toa jibu lako

Ilani ya ukawa ni bora zaidi kwani imetambua na kuweka misingi ya haki na utu wa mwanadamu kuheshimiwa. mfano pensheni kwa wazee ambao kimsingi walivuja sana jasho katika ujenzi wa taifa lao tena katika mazingira magumu mno.....
 
Hivi bado tu kuna watu mnategemea jambo jema kutoka CCM???? Hawa CCM hawana jipya! Ni udanganyifu uleule miaka nenda rudi!
 
UKAWA siyo chama hi yo hawana Ilani! CDM haijaandaa ilani hivyo huwezi linganisha vitu ambavyo havipo. Subiri water ilani Yao.

Nalifahamu but nimetumia UKAWA kwa kuwa ni identity Yao CDM ni mwakilishi tu Pia haiondoi maana ya swali langu
 
Ilani bora ni ile inayozungumzia maadili ya ukongozi kukomesha rushwa na ufisadi
 
Ilani ya ukawa ni bora zaidi kwani imetambua na kuweka misingi ya haki na utu wa mwanadamu kuheshimiwa. mfano pensheni kwa wazee ambao kimsingi walivuja sana jasho katika ujenzi wa taifa lao tena katika mazingira magumu mno.....

Poa kwa ur views pamoja
 
Ukawa kazi yao ni kutekeleza sera zote zote nzuri hata kama zimetoka ccm ilani yao ni kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa ujumla na kuleta maendeleo kwa kasi ya ajabu sanjari na kuweka mfumo bora wa kuzuia ufisadi na ufujaji wa pesa za umma, kurejesha viwanda na kufufua viwanda na kujenga viwanda vipya vingi, kupanua soko la Ajila kwa nguvu zote, kufuta misamaha ya kodi isiyo na Tija kwa kwa kifupi Ukawa wanakuja kamaliza kero nyingi sugu.
 
Hivi bado tu kuna watu mnagmea jambo jema kutoka CCM???? Hawa CCM hawana jipya! Ni udanganyifu uleule miaka nenda rudi!

Dat wy tueleweshane ili watanzania wote tuchague kilicho bora
 
Ilani bora ni ile inayozungumzia maadili ya ukongozi kukomesha rushwa na ufisadi

Naona zote zimezungumzia rusha hebu fafanua kidogo ni ILANI IPI YENYE sera nzuri kwa Jambo hili la rushwa
 
Ukawa kazi yao ni kutekeleza sera zote zote nzuri hata kama zimetoka ccm ilani yao ni kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa ujumla na kuleta maendeleo kwa kasi ya ajabu sanjari na kuweka mfumo bora wa kuzuia ufisadi na ufujaji wa pesa za umma, kurejesha viwanda na kufufua viwanda na kujenga viwanda vipya vingi, kupanua soko la Ajila kwa nguvu zote, kufuta misamaha ya kodi isiyo na Tija kwa kwa kifupi Ukawa wanakuja kamaliza kero nyingi sugu.

Jambo jema kusikia hayo
 
hata hivyo vijana wa kukokopy na kupaste sahv wameshazidiwa hoja, sahivi nasikia Lumumba kuna fukuta kuhusu suala la tshirt so dizain kama wamezila vile

Umoja wa vijana wameporwa Tenda na Ruge wa clouds wameamua kususa lakini wenzao waliompa Tenda sasa wameshiba baada ya Ruge kuwamegea chao cha juu kwa kufanikisha Dili
 
Kiukweli ilani ya chadema ndio inayowafaa watanzania kwa kipindi hiki tulichonacho
 
Naona zote zimezungumzia rusha hebu fafanua kidogo ni ILANI IPI YENYE sera nzuri kwa Jambo hili la rushwa

Mfano Mahakama ndipo penye tatizo kubwa hapo panafaa pamulikwe kwa kufanya kazi kuanzia saa moja asubuhi hadi saa kumi na moja jioni wafanye kazi hadi jumamosi, mahakimu wawe wanachunguzwa nyendo zao kuwepo na kitengo cha Usalama kwenye Mahakama zote ili Haki zitendeke kukiwa na Haki popote maendeleo yatakuja kwa kasi kwani magumashi ni Adui wa Haki.
 
Ilani Bora ni ile Yenye Vipaumbele Vichache Vinavyotekelezeka upande mmoja na upande wa pili vyenye kuweza kugusa maeneo mtumbuka ya jamii yetu. WINGI WA VIPAUMBELE NI SAWA NA HAKUNA KIPAUMBELE, HAKUNA NIA DHABITI.

Ilani inayoangalia mahitaji ya maisha ya mwananchi na hasa katika shida ya makazi bora na hivyo kushinikiza uwekezaji katika sekta ya ardhi/nyumba inaweza zaidi kulipeleka taifa mahali pengine kwani itaongeza ajira na kuboresha mazingira ya kuishi hivyo kupunguza maradhi, itachochea utumiaji wa taaluma zote na hivyo kuchochea tija kwa elimu na mwisho wa siku kupigana na ujinga na njaa.

Ilani Mbaya ni ile iliyojengwa kwenye misingi ya kudhani taifa linaweza kustahimili ujenzi wa barabara kila mahali kwa sababu tu watu wanataka! Au kuhakikisha dawa hospitali za serikali kwa kuwa kwa sasa hivi faramsia binafsi zina dawa hali hospitali za uma hazina. Ilani za kuibagua sekta binafsi ni mufilisi.

Ilani bora ni ile inayoona taifa kwa mwono wa sisi sote kushiriki katika maendeleo, kukubali kuna maeneo ambayo yatasubiri mengine - yale yenye nafasi yawekeze na kupata ziada ambayo tutaitumia kwa yale ambayo hayakujaliwa malifhafi asilia...sio ya kudhania kuna Kaskazini na Kusini au vingine.
 
Back
Top Bottom